Monday, 9 September 2013

MTANDAO WA WIZI WA FEDHA HALMASHAURI

  IMEGUNDULIKA kuwapo na mtandao hatari nchini unaohusisha Hazina na Halmashauri mbalimbali kuchota mamilioni ya fedha huku wakiziandikia kutumika katika miradi ya maendeleo. Mtandao huo ambao umeelezwa kuwahusu viongozi ngazi ya juu wa Hazina na Halmashauri umekuwa ukiongeza fedha za ziada kati ya Sh. Milioni 500 hadi 600 kwenye fedha halali za miradi ya maendeleo zilizoidhinishwa kisheria na Bunge. Tayari mtandao huo umedaiwa kufanikiwa kuidhinisha mamilioni ya fedha katika Halmashauri tatu ambazo ni Mbarali, Korogwe Mjini na Mvomero. Hayo yalielezwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Rajab Mohamed Mbarouk alipokuwa akifanya majumuisho ya vikao vya kamati yake. Mbarouk alisema kumeibika mtandao hatari wa kujichotea fedha za Serikali kwa kusingizia zinakwenda Halmashauri lakini zinapofikishwa huko zinawarudia wenyewe. “Hii nchi sio masikini na hakuna sababu ya kusikia eti miradi imekwama kwa sababu ya fedha kukosa, katika vikao vyetu tumebaini kwamba Hazina na Halmashauri nchini zinashirikiana kula fedha za Serikali. “Mfano halisi ni huu Halmshauri ya Mbarali katika mahesabu yamahitaji yao yote walitakiwa kupewa Sh. milioni 70 lakini Hazina walipeleka Sh. milioni 700. “Fedha hizo zinapofikishwa kule zinaidhinishwa kupokelewa Sh. milioni 70 zilizokuwa zikihitajika zile zilioongezwa zinazrudi mikononi mwa mtandao huo ambao ni katika Hazina na Halmashauri. “Halmashauri ya Mbarali imekuwa imekuwa ikipata hati chafu mpaka leo ninavyoongea hapa katika kuboroga kwenye mahesabu yao ya fedha wanazopokea na jinsi wanavyozitumia. “Kama unataka kuona mtandao huo umeota mizizi mikubwa, tumebaini utakaswaji wa fedha umefanyika Halmashauri ya Korogwe Mjini Sh.milioni 500 huku mahitaji yao yakiwa chini ya Sh. milioni 100. “Hivyo hivyo utakaswaji huo umefanyika Halmshauri ya Mvomero kwa kupelekea Sh. milioni 500 ambapo mahitaji yao hayakuwa yanafikia kiasi hicho, kama wana kamati tumechukizwa na utoroshwaji wa fedha hizo na tutalifikisha bungeni kwa hatua zaidi. “Cha ajabu unakuta viongozi wanaohusika katika Halmashauri hizo wanapofanya utakaswaji huo wanawahi kuhama, mfano halisi ni aliyekuwa Mhasibu wa Halmshauri ya Mvomero,Nassoro Mkwanda ambaye hivi sasa yupo Halmshauri ya Kiteto kwa cheo hicho hicho,”alisema. Mbarouk alisema kama mtandao huo hautadhibitiwa haraka taifa litaendelea kufilisika na maendeleo ndani ya jamii yakikwama ambapo athari yake ni uchumi kushikiliwa na wachache huku kundi kubwa ni masikini. Mkurugenzi Kiteto amwaga machozi Awali ya yote, Kamati ya LAAC ilikutana na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kupitia mahesabu yao ambapo ilikubaini ubadhirifu mkubwa wa fedha kitendo kilimfanya Mkurugenzi halmashauri hiyo, Jane Mutagurwa kulia ndani ya kikao. Kugundulika kwa ubadhiri katika Halmshauri hiyo kulimfanya Mwenyekiti wa LAAC, Mbarouk kuagiza polisi kufika hapo ili kuwaweka chini ya ulinzi baada ya kikao kumalizika. Kamati ilibaini Halmashauri ya Kiteto imepoteza Sh. milioni 500 ambazo ambazo ni mapato ya kodi za mazao kutoka kwa vyama vya ushirika. Ilibainika fedha hizo zilichukuliwa na wakala wa ukusanyaji wa ushuru huo kwa idhini ya Halmashauri hilo kwa mkataba wao lakini wakotomea bila kuzikabidhi. Katika mahojiano kati ya wabunge wa kamati ya LAAC na viongozi wa Halmashauri hiyo ilibainika kuwa kuna magari mawili ya Serikali yenye usajili wa STK hayajulikani yalipo na anayeyamiliki licha ya kuonekana kwenye vitabu vyao ni mali zao. Pia ilibainika kuwa Sh. milioni 179 zimeanzwa kulipwa kwa watumishi wanaoidai Halmashauri hiyo lakini hawajulikani kwa majina wala idara zao. Vile vile imegundulika kwamba Halmashauri hiyo imekutumia Sh.milioni 34 zilizotokana na mauzo ya mahindi ya msaada wa njaa iliyoikumba Wilaya ya Kiteto na hazijawahi kurudishwa Ofisi ya Waziri Mkuu. Ubadhirifu mwingine uliopatikana katika Halmashauri hiyo ni ujenzi wa jiko la kisasa lililogharimu Sh. milioni 25 lakini limeshindwa kutumika na badala wameligeuza kuwa nyumba ya mwalimu huku taarifa zao zikieleza vitu vyote vimekwekwa kumbe ni uongo. Hata hivyo ilibainika mamilioni ya fedha yanayotengwa na Serikali kwemnda miradi mbalimbali ya maendeleo vijijini na mfuko wa kuwawezesha wanawake na vijana hayawafikii ipasavyo. Ilibainika miradi mingi ya ujenzi wa shule za msingi na Sekondari ikiwani ya Kiperesi ikishindwa kukamilika huku fedha zilizotengwa zikiwa zimetolewa kitendo ambacho kiliwafanywa wajumbe wa LAAC kupendekeza kuvunjwa kwa Halmshauri hiyo. Wakati Mkurugenzi, Mutagurwa alipotakiwa kutoa majibu ubadhiri huo alipatwa na wasiwasi na kigugumizi kueleza wazi na kuanza kulia. Viongozi wengine waliokuwa wamsaidia kujibu hoja ni Ofisa Mipango wa Halmashauri hiyo,Rabson Magesa, Mwenyekiti wa Halshauri ya Wilaya ya Kiteto, Mainge Lemalali na viongozi wengine ambao ilionekana kumsukimia mkurugenzi wao. Kutokana na kutokuwapo na majibu sahihi, Mbarouk alimua kuwatoa nje viongozi wengine ispokuwa Mkurugenzi ili kuhoji peke yake ambapo ilibainika kwamba viongozi waliomzunguka wanamhujumu huku jamii ya wamasai wakimdharau ni jinsia yake ya kike. Mbarouk aliamua kusiktisha mpango wa kumweka chini ya ulinzi wa polisi baada ya kuelezwa hivyo na kuamua kuunda kamati ndogo ya kuchunguza ubadhirifu na hali halisi ilivyo Kiteto. Pia alipewa muda wa kuhajikisha fedha pamoja na gari mbili zinapatikana kabla ya Disemba 31, mwaka huu ingawa aliomba kuongezewa muda hadi Juni 2014 kitendo kilichopingwa vikali. MWISHO.

No comments:

Post a Comment