Sunday 25 August 2013

OPERESHENI YA KUONDOA POLISI WASIOFAA

Na Benjamin Masese, Dar es Salaam WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi ametembeza panga kali ndani ya Jeshi la Polisi na kuwafukuza kazi maofisa wanne huku baadhi yao wakivuliwa vyeo vyao. Maofisa hao ni wale waliohusika kushiriki kwa namna moja au nyingine katika matukio yaliyotokea mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro na Kigoma na kulalamikiwa vikali na wananchi. Akizungumza na Waandishi wa habari Da r es Salaam jana alisema askari hao ni wale waliohusika kutumia gari la kutuliza Ghasia (FFU) kubeba bangi mkoani Arusha na Kilimanjaro Tukio jingine ni lile la askari mkoani Morogoro kutumia fuvu la binadamu kumbambikizia mfanyabishara kwa lengo la kupata fedha, mauaji ya mfanyabishara wa Wilaya ya Kasulu yalifanywa na askari polisi. Tukio la Bangi Dk. Nchimbi alisema katika sakata la tukio la bangi amemvua madaraka yote aliyokuwa nayo Mkuu wa Kikosi cha FFU Mkoa wa Arusha, Mrakibu wa Polisi, Ramadhan Giro kwa kosa la kushindwa kusimamia kikamilifu askari na maofisa walio chini yake na kusababisha kutoke tukio hilo. Pia amemsimamisha kazi Ispekta Isaac Manoni na kushitakiwa kijeshi kwa kosa la kutumiwa kumtorosha mtuhumiwa ambaye ni polisi Edward Mwakabonga aliyekuwa dereva wa gari la FFU kitendo kilicholifedhehesha jeshi hilo. “Katika tukio hilo kitendo cha Inspekta Salum Kingu wa kikosi cha FFU Mkoa wa Kilimanjaro kubaki kwenye gari mita 80 kutoka ilipo nyumba ya mtuhumiwa Edward alipopelekwa Moshi kukabishi vifaa vya jeshi letu kimechangia, hivyo tumempa onyo kali la kuwa makini na utendaji wake. “Pia Inspekta Mikidadi Galilima kutotimiza wajibu wake ipasavyo katika kumshauri Mkuu wa FFU Mkoa wa Arusha juu ya ukaguzi na usimamizi wa rasilimali na kujaribu kuficha ukweli wa tukio, nimempa onyo kali Inspekta Galilima. “Katika tukio hilo nimempandisha cheo ASP Francis Duma aliyekuwa kiongozi wa askari 14 katika kupambana kulikamata gari la FFU lililobeba bangi na kuwa Mrakibu wa Polisi,askari wengine 14 nimegiza Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP, Said Mwema kuwapandisha vyeo kwa sababu wapo ngazi yake,”alisema. Tukio la fuvu Dk. Nchimbi alisema amewavua madaraka yote waliyonayo Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Mvomero, Inspekta Jamal Ramadhan na Mkuu wa Kituo cha Polisi Dumila, Inspekta Juma Mpamba kutokana na kuonyesha udhaifu mkubwa katika utendaji kazi wa kushindwa kuwasimamia askari wake na kushindwa kuwakamata matapeli na hawalifu ambao ni vinara. Dk. Nchimbi alisema kabla ya tukio la askari watatu kushirikiana na raia wawili kumbambikizia fuvu la binadamu mfanyabishara Samson Mwita, Inspekta Ramadhan alikuwa na taarifa za mpango wa tukio hilo la askari wake kushirikiana na rai kufanya kufanya hivyo lakini hakumtaarifa Inspekta Mpamba. Alisema askari wote waliohusika na tukio hilo ambao ni Sajeti Pasua Mohamed, Sajeti Sadick Madodo Koplo Nuran Msabaha wamefukuzwa kazi na kushitakiwa kwa uhalifu waliotenda sambamba na raia wawili ambao ni Rashid Hamisi na Adamu Peter. Kupiga na kuua raia Dk. Nchimbi alisema Disemba 25 mwaka jana askari wa kituo kidogo cha polisi cha Heru Ushingo kilichopo Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma kwa pamoja walimpiga raia ambaye ni marehemu sasa Gasper Sigwavumba na kumweka mahabusu bila msaada wowote wa matibabu. Alisema katika tukio marehemu alipasuka bandama kutokana na kipigo hicho na kuongeza kwamba upelelezi mbovu uliofanywa chini ya usimamizi wa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kasulu, ASP Daniel Bendarugaho kesi ya mauaji iliweza kuondolewa mahakamani. Dk. Nchimbi alisema wakati kesi inaondolewa mahakamani askari waliohusika ambao ni Koplo Abraham Peter na PC Simon Sunday walikuwa wamefukuzwa kazi na kuwa huru jambo ambalo lilizua malalamiko. “Kutokana na ASP Bendarugaho kutokuwa makini katika kusimamia upelelezi wa jalada husika la kesi hiyo ya mauaji tunavua madaraka na upelelezi unaanza upya ili haki itendeke,”alisema. “Operesheni ya kulisafisha jeshi hilo itaendelea hadi litakapokuwa safi, leo hii wananchi wamekata tama kabisa na jeshi la polisi ukimwambia kitu chochote juu ya polisi haamini. “Kwa kipindi nitakachokuwa naongoza wizara hii, nitalisafisha na Watanzania watarudisha imani kwa polisi, katika matukio haya matatu askari waliohusika moja kwa moja wamefukuzwa kazi na kushitakiwa. “Haya ni matokeo ya uchunguzi uliofanywa na timu niliyoiunda ambapo Mwenyekiti wake alikuwa Mkurugnezi Mkuu wa Idara ya masuala ya Malalamiko Makao Makuu, Augostine Shio.

BOMBA LA GESI KUTANDAZWA LEO.26/8/2013



Bomba la gesi ya Mtwara kutandazwa leo
Na Benjamin Masese, aliyekuwa Lindi
BOMBA la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam, linaanza kutandazwa leo likianzia mkoani Lindi.
Kutokana na hali hiyo, Serikali imeonya kwamba, yeyote atakayethubutu kuharibu miundombinu ya bomba hilo, atachukuliwa hatua.
Taarifa hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alipofanya ziara ya kukagua, ubora wa vifaa, rasilimali watu na  maandalizi ya miundombinu ya kutandaza bomba hilo.
Wakati wa ziara hiyo ya siku moja, alikuwapo pia Balozi wa China nchini, Lu Youging, viongozi mbalimbali wa Serikali na viongozi wa kampuni zinazotandaza bomba hilo.
Profesa Muhongo alisema ameridhishwa na maandalizi yanavyokwenda, kwa kuwa kuna vifaa vya kisasa na imara.
Kesho kutwa (leo), utandazaji wa bomba unaanza rasmi na kwa maandalizi niliyoshuhudia, nina imani mradi huu utakamilika kabla ya Desemba mwaka 2014.
“Naomba Watanzania wawe na imani kubwa na watoe ushirikiano kwani utandazaji wa bomba utafanyika katika pande zote mbili, kwa maana ya nchi kavu na baharini.
“Mradi huu ni wa gharama kubwa na kama mnakumbuka, tulikopa fedha kutoka Benki ya Exim ambazo ni Dola za Marekani bilioni 1.2 kwa masharti nafuu.
“Pamoja na kwamba nia yetu ni nzuri, kuna baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya nchi hii, nataka kuwahakikishia Watanzania wote, kwamba usalama wa miundombinu hii utakuwa shwari na kama mtu anataka kushughulikiwa na Serikali, basi ajaribu kuihujumu atakiona cha mtema kuni.
“Hapa tumeshuhudia Watanzania 45 walioanza kupata ajira kama madereva, vibarua, kampuni za usafirishaji, huu ni mwanzo tu na ikifika sehemu ya kuhitaji watu wenye utaalamu, wataajiriwa wenye utaalamu,” alisema Profesa Muhongo.
Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, mabomba yanayotandazwa ni ya aina mbili yakiwamo ya inchi 36 na uzito wa tani tano na yenye inchi 24 yakiwa na tani tatu ambayo alisema kwa ujumla wake yatadumu kwa miaka 30 na kama yakitunzwa vizuri yatadumu hadi miaka 70.
“Tunataka ifikapo mwaka 2016, tuwe na umeme wa megawati 3000 na mwingine wa ziada wa utakaokuwa ukiuzwa nje ya nchi ikiwamo Kenya ambayo imeleta maombi ya kuuziwa megawati 1000,” alisema.
Pamoja na kufanya ziara hiyo juzi, Profesa Muhongo alisema itakuwa ni endelevu na itakuwa ikihusisha waandishi wa habari.
Naye, Balozi Youging, alisema gesi ni kitega uchumi kizuri ambacho kinaweza kuwaondoa Watanzania katika umasikini.
“China ni moja ya nchi iliyonufaika na gesi na ndio maana raia wake ni wataalamu wa nishati hiyo, naamini upatikanaji wa gesi hapa Tanzania, utasaidia Watanzania kuondokana na matumizi ya mkaa na kuni.
Kwa upande wake, Meneja Mradi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania, Mhandisi Baltazari Thomas, alisema hadi sasa watu 163 wamepata  ajira katika awamu ya kwanza na kati ya hao Watanzania ni 68.
 Mwisho.
Rufaa dhidi ya Zombe kusikilizwa leo
Na Kulwa Mzee, Dar es Salaam
MAOMBI ya Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) ya kuongezewa muda wa kukata rufaa dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na askari wenzake wanane walioachiwa huru katika shtaka la mauaji, yanatarajiwa kusikilizwa leo.
Maombi hayo yanatarajiwa kusikilizwa katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam mbele ya Jaji Aloyisius Mujuluzi.
Katika shauri hili, DPP aliwasilisha maombi ya kuomba kuongezewa muda wa kukata rufaa, baada ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, kutupilia mbali rufaa ya awali kwa sababu ilikuwa na makosa ya kisheria.
Rufaa hiyo ilitupwa baada ya kubaini kuwapo kwa dosari katika hati ya kusudio la kukata rufaa na mahakama kukataa kuamuru makosa yaliyojitokeza yafanyiwe marekebisho.
“Kusudio la kukata rufaa ndio linatengeneza rufaa yenyewe, kwa kuwa kuna makosa, hakuna rufaa iliyopo mahakamani, kama makosa yangejitokeza katika rufaa yenyewe, Mahakama ingeweza kutoa maelekezo ya kufanyiwa marekebisho, rufaa inatupwa, Jamhuri ina haki ya kuwasilisha rufaa nyingine nje ya muda, baada ya kuomba kufanya hivyo,” alisema Mwenyekiti wa Jopo la Majaji Watatu, Edward Rutakangwa.

Majaji wengine waliokuwa wakisikiliza rufaa hiyo kabla ya kutupwa ni Jaji Mbarouk Mbarouk na Bethuel Mmila ambao awali walipoketi kwa ajili ya kuanza kusikiliza rufaa iliyokatwa na DPP kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, ziliibuka hoja za dosari katika hati ya kusudio la kukata rufaa.

Zombe na wenzake walikuwa wakikabiliwa na kesi ya mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini wakazi wa Mahenge Morogoro pamoja na dereva teksi mmoja.

Kabla ya jopo la mawakili wa Serikali lililokuwa linamwakilisha DPP ambao ni Mawakili wa Serikali Wakuu, Edwin Kakolaki, Vitalis Timon, Prudence Rweyongeza na Mawakili Revocatus Mtaki na Alexander Mzikila, halijaanza kuwasilisha hoja zao za kukata rufani, Jaji Mbaraouk alilihoji jopo hilo kuhusu dosari hiyo.

“Mahakama inataka kujiridhisha juu ya kinachosomeka katika hati ya kusudio la kukata rufaa, ambayo inasema mnapinga hukumu iliyotolewa na Jaji Massati wa Mahakama ya Rufaa. Sasa hii inakuja kwetu kama marejeo au mapitio," alihoji Jaji Mbarouk.

Hata hivyo, Wakili Timon, alikiri kuhusu dosari hiyo na hivyo kuiomba Mahakama kuwaruhusu kufanya marekebisho na kisha kuendelea kusikiliza rufaa hiyo.

Jaji Rutakangwa alihoji upande wa Jamhuri kuwa hati hiyo ina dosari, kwa kuwa inaonyesha wanakata rufaa kupinga hukumu ya Jaji wa Mahakama ya Rufaa, wakati hajawahi kukaa kusikiliza shauri hilo kwa kuwa si sahihi.

Ombi la mawakili wa Serikali la kuomba kufanyia marekebisho hati hiyo, lilipingwa vikali na mawakili wanaowawakilisha Zombe na wenzake ambao ni Richard Rweyongeza, Majura Magafu na Dennis Msafiri.

Katika shauri hili, mbali na Zombe, wajibu rufani wengine ni polisi Christopher Bageni, Ahmed Makele, Jane Andrew, Koplo Emmanuel Mabula, Michael Shonza, Abeneth Saro, Rajabu Bakari na Festus Gwasab.

Serikali ilikata rufaa hiyo kupinga hukumu iliyotolewa Agosti 17, 2008 na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.

 mwisho.


Nyavu haramu za Sh milioni 150 zateketezwa

Na Ahmed Makongo, Bunda

NYAVU haramu 3,280 zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 150, zimekamatwa wilayani Bunda, mkoani Mara na kuteketezwa kwa moto.

Nyavu hizo ziliteketezwa jana kwa usimamizi wa Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Joshua Mirumbe.

Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, Mirumbe alisema kuwa nyavu hizo ambazo ni pamoja na makokolo ya kuvulia sangara, nyavu zenye matundu madogo, timba na makokolo ya dagaa, zimekamatwa na vyombo vya dola kutokana na msako unaoendelea wilayani hapa.

Alisema kuwa msako huo unashirikisha askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), polisi, mgambo pamoja na maofisa wa idara ya uvuvi.

Alisema operesheni hiyo aliianzisha mwenyewe na kwamba itakuwa endelevu kwa kuwa lengo lake ni kutokomeza wavuvi haramu wilayani hapa.
Ili kuhakikisha uvuvi haramu unakomeshwa wilayani hapa, aliwataka viongozi wa Serikali za vijiji, kata na Vikundi vya Ulinzi wa Rasilimali za Ziwa Victoria (BMU), kuhakikisha wavuvi haramu wanakamatwa.

Alisema kama uvuvi haramu utaendelea katika baadhi ya maeneo, kitakachofuata ni kukamatwa kwa viongozi wa maeneo utakakokuwa ukifanyika uvuvi huo.

“Hatua ifuatayo ni kukamata viongozi wa Serikali za vijiji na kata na wale wa BMU ambao tutakuta kwenye maeneo yao kunaendeshwa shughuli za uvuvi haramu,” alisema Mirumbe.

Aliwaonya viongozi hao kutojihusisha na shughuli za uvuvi haramu, kwa kuwa inasemekana baadhi yao wanafadhili wavuvi hao.

Naye, Ofisa Uvuvi wa Wilaya ya Bunda, Stephen Ochieng, alisema nyavu hizo zilikamatwa katika Tarafa za Kenkombo na Nansimo ambako ndiko uvuvi haramu ulikoota mizizi.

Aliongeza kwamba, wapo wavuvi haramu ambao wamekuwa wakitumia sumu na kwamba uvuvi huo unahatarisha afya za wananchi pamoja na kuua viumbe hai wa majini.

Aidha alitumia fursa hiyo kuwaomba viongozi wa wilaya jirani zilizoko kwenye ziwa Victoria, kudhibiti wavuvi haramu, kwani unapofanyika msako katika Wilaya ya Bunda, baadhi ya wavuvi hao hukimbilia katika wilaya hizo.

Mwisho.






Thursday 15 August 2013

LWAKATARE HOI

Polisi, Dk. Slaa jino kwa jino

Na Benjamin Masese, Dar es Salaam

WAKATI Jeshi la Polisi likiendelea kumng’ang’ania  Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare kwa tuhuma za kupanga njama za kudhuru watu, imedaiwa kuwa afya ya kiongozi huyo imezidi kudhoofika.

Tuesday 13 August 2013

TUJADILIANE LEO

Hivi kulingana na matukio haya yanayotokea ya ukatili kwa raia, wizi, utekaji na masuala kama hayo yanaashiria nini? tujadili, tafadhali unapochangia hapa toa hoja sio kushambulia mtu kwa itikadi na dini zako.

UKATILI HUU MPAKA LINI TANZANIA?


Mama akipigwa na mume wake baada ya kutofautina
Baba akimdhibiti mke wake kwa kumkata mapanga baada ya kuona ngumi, mateke na fimbo havikutosha
 
Na Benjamin Masese, Dar es Salaam

UKATILI wa kijinsia ni jambo kubwa kwenye ajenda za haki  za binadamu kimataifa.Ukatili unaweza kuwapata wanaume na wanawake lakini mara nyingi wanawake na watoto ndio waathirika wakubwa.

Hali hii imetokana  na mifumo mbalimbali iliyopo na uhusiano wa kijinsia ulivyo katika jamii zetu hapa nchini ambapo kundo moja hujiona ni bora kuliko kundi lingine.

Kwa miaka mingi wanaume wamechukuliwa kuwa katika daraja la juu kuliko mwanamke nah ii imejionyesha na kuendelea kuonekana wazi katika  nyanja zote za kijamii, kiutamaduni, kisiasa na kiuchumi.

Mazoea hayo yamejengwa tangu zamani huku kukiwa na ngazi za kifamilia hadi kitaifa jambo ambalo ni hatari katika jamii nyingi Barani Afrika na sehemu nyingine duniani.

Kutokana na hali hiyoilivyo mpaka sasa, kuna haja kubwa ya kutoa elimu juu ya ukatili katika jamii zetu hususani vijijini kunakotokea kila siku vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake.

Bila Serikali, taasisi, mashirika na wadau wengine wanapaswa kuungana pamoja na ili kuwaelimisha jamii juu ya kupambana na kuzuia ukatili wa kijinsia ili kuleta mabadiliko katika jamii.

Sote tunatambua kwamba ukatili ni kitendo chochote anachofanyiwa binadamu na kumsababishia maumivu au athari kimwili, kiakili au kisaikolojia.Kumekuwapo na vitendo vya ukatili vingi tena vya kukusudia, kulazimisha, kutisha au kugofya dhidi ya wanawake kutaka kufanya jambo au tendo la ngono bila hiari yao.

Binadamu yeyote anaweza kufanyiwa ukatili wa aina tano  ukitegemea  na utamaduni na historia  ya jamii husika. Mara nyingi ukatili huo hufanyika kati ya wanandoa wa wapenzi lakini wanawake mara nyingi wamekuwa wakisumbuliwa zaidi na ukatili wa kijinsia katika uhusianohuo.

Moja ya ukatili ni ule wa kimwili ambao mtu hufanyiwa kitendo ambacho kinaumiza mwili na madhara yake huonekana moja kwa moja  na wakati mwingine mtendewa ukatili anaweza kuhisi maumivu bila mtu mwingine kutambua kuwa amefanyiwa ukatili wa kimwili.

Baadhi ya mifano ya ukatili wa kimwili ni pamoja na vipigo, shambulio la kimwili, kuchomwa moto, matumizi ya silaha, kuvutwa nywele, kusukuma, kunyonga mkono au mguu, kupigwa kichwani na kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu yoyote ya mwili.

Pia  upo ukatili wa kisaikolojia ambao mtu anatendewa  na unamsababishia maumivu kiakili, kihisia huku mtenda kutotambua mwenzake anaathirika, mfano matusi kwa njia ya maneno au ishara yenye lengo la kudhalilisha, vitisho na kutishia kufanya fujo, maneno ya kufehedhesha, kudharau, kutishia kutoa siri, kuingiliwa faragha, kutishiwa kuuawa na mengine mengi.

Vile vile kuna ukatili wa uhusiano wa kingono ambao huambatana  na vitendo vinavyohusiana na masuala ya ngono, kwa mfano unyanyasaji wa kijinsia, kujamiiana kwa maharimu, ubakaji ndani ya ndoa, ulawiti, utekaji na usafirishaji  wa wanawake au wanaume na watoto kwa ajili ya ngono na vitendo vingine vya namna hiyo.

Upo ukatili wa kiuchumi ambao humnyima fursa za kiuchumi mwanamke au mwanaume katika kujiongezea kipato na kuchangia katika maendeleo.Aina  hiyo ya ukatili huwapata wanawake kutokana na hali yao ya kuwa tegemezi kwa wenzi wao.

Kitendo cha wanawake kuwa tegemezi kwa wanaume kimekua kinawaathiri sana kwani wanakosa kauli katika mali za familia na kutoshirikishwa kwenye maamuzi ya maendeleo.

Pia kuna ukatili unaotokana na tamaduni au mila potofu zetu hapa nchini ambazo zinakinzani na haki za binadamu jambo linalochangia kuwapo kwa vitendo vya ukatili. Baadhi ya ukatili wa mila potofu ni pamoja na ndoa za kushurutisha za utotoni, kutakasa wajane, kurithi wajane, utekeaji, matambiko ya kingono kwa watoto, miiko ya chakula na ukatili utokanao na mahari.

Kutokana na  uendelezaji wa vitendo vya ukatili nchini, kituo cha Msaada wa Sheria  kwa Wanawake Tanzania (WLAC)  kimeamua kuanzisha kampeni ya kupinga vitendo hivyo na kutoa msaada wa kisheria kwa wanawake  ili kuleta usawa  wa kijinsia Tanzania.

Taasisi ya WLAC  ni shirika lisilo la Serikali lililoanzishwa mwaka 1994 chini ya sheria ya makampuni sura ya 212 na pia limekuwa likiendeleza shughuli  za kitengo cha msaada wa sheria  SUWATA kilichoanzishwa mwaka 1989.

Kati ya madhumuni ya WLAC ni kutoa msaada wa sheria ju ya masuala yanayowakabili wanawake kama ndoa, mirathi, mikataba, biashara, ajira, uwakilishi mahakamani na huduma nyingine zinazofanana na hizo.

Pia imekuwa katika harakati za kujenga mtandao wa mashirika pamoja na taasisi zenye mwelekeo unaofanana na WLAC na kuratibu kwa pamoja shughuli za uhamasishaji umma kuhusu haki za wanawake na watoto.

Si jambo la kificho kwani wanawake wamekuwa katika changamoto kubwa hasa pale wanapokuwa katika ajira rasmi na hata zisizokuwa rasmi, baadhi yao wamekuwa  wakikosa nafasi za kufanya kazi mahali walipoomba kazi auhata katika ngazi ya familia kutokanana sababu mbalimbali.

Katika maeneo ya kazi, uzoefu unaonyesha wazi kuna kazi za wanawake na kazi za wanawake, wanawake waliobahatika kupata ajira wengi utawakuta nafsi za chini zaidi kama mapokezi, uhudumu wa ofisi, kazi za usafi na katibu mukhatsi.

Wakati mwingine baadhi ya wanawake wamelazimika kuingia katika uhusiano wa kimapenzi na wakuu wao wa kazi ili kupata mahitaji yao.Wanawake wa namna hiyo huishia kwenye migogoro na waume zao au wapenzi wan a hatimaye uhusiano huo huharibika kabisa na kufukuzwa kazi.

Kazi zinazohitaji mwanamke kusafiri sana, kufanya kazi muda mrefu, wakati wa usikuau zinazohusisha kukutana na watu mbalimbali mara nyingi zimesababisha migogoro katika ndoa.

Hata hivyo wanawake wengi wamekosa fursa ya kujishughulisha ili kuongeza pato la familia, ambapo kwa wale waliobahatika kupata ajira zisizo rasmi wengi wao wanaishi kwa masharti na kutokuwa huru na wanapata mapato yanatokanayo nakazi wanayofanya.

Suala la ukatili lina upana wake ambapo upo ukatili wa kijinsia unaotokana na lugha ambapo maneno mbalimbali yamekuwa yakitumika kumwelezea mwanamke ambayo uhalisia wake ni ukatili wa kijinsia.

Maneno hayo yamekuwa yakitolewa katika kuelezea maumbile na tabia ya baadhi ya wanawake, matumizi ya lugha hiyo kwa sehemu kubwa huchangia kuonyesha mfumo dume ambao ndio unaotawala maisha ya watu ya kila siku. Matumizi ya lugha yanadhihirisha dhana potofu kwamba kundi la wanaume lina nguvu na ni bora kuliko wanawake.

Asilimia kubwa na mazoea yaliyopo sasa ni kwamba neno mwanamke amekuwa akichukuliwa ni kama chombo cha kumstarehesha mwanaume, mfano kuna maneno ya kama changundoa, sahani ya babu, namba nane, twiga na mengine kam hayo ambayo huonesha kuwa mwanamke ni dhaifu kuliko mwanaume.

Maneno mengine yanayoendana na hayo wakati mwingine yanaweza kutolewa dhidi ya wanaume, kwa mfano bushoke, dume la mbegu lakini yote yameelekzwa kwa wanawake kumuonyesha mwanaume ni bora.

Hata hivyo upo ukatili katika vyombo vya habari na matangazo ya kibiashara, mfumo wa habari na utoaji wa habari zenyewe umekuwa ukionesha taswira ya mwanamke kama chombo cha kumburudisha mwanaume, mfano matangazo, picha na mziki hutumiwa  na kuonyesha  wanawake kama sehemu ya matangazo ya biashara.




Kutokana na hali hiyo hivi karibuni WLAC kupitia wanasheria wake waliandaa semina iliyohusisha  wanawake na wanaume  wanaojiita wanabadiliko kutoka mikoa ya Dar es Salaam na Pwani na kutoa elimu juu ya mambo kadhaa ya ukatili wa kijinsia nchini unaotokea katika nyanja mbalimbali ndani ya jamii.

Wanasheria wa WLAC waliokuwa wanatoa elimu kwa wanabadiliko ni pamoja na Lilian Lwanga na Hildegard Msina ambao walitoa ushahidi jinsi wanawake wanavyoteseka ndani ya ndoa zao pamoja na kunyang’anywa urithi wa mme wake mara anapofariki na kuacha familia.

Kwa upande Lwanga alibainisha kwamba katika utafiti walioufanya katika kadhaa nchini wamebaini asilimia 75 ya wananawake walio ndani ya ndoa hawana uhuru wa kijitawala katika maisha yao ya kila siku kutokana na kufanyiwa vitendo vya ukatili na wenzi wao.

Pia anasema walibaini wanaume wengi vijijini wamekuwa wakivunja ndoa zao au kuwatelekeza wake wao baada ya kujifungua watoto wenye vichwa vikubwa, midomo ya sungura na wengine wa namna ambapo aliitaka Serikali kuchukuliwa hatua za kisheria ili kukomesha hali ya ubaguzi, unyanyasaji na ukatili dhidi ya wanawake.


WLAC imeamua kuendesha kampeni maalum ijulikanayo kwa jina la TUNAWEZA kwa wanamabadiliko ili kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji nchini ambavyo vinaonekanakuwa jambo la kawaida katika  jinsia ya kike.

 Lwanga anasema msaada wa kisheria unaotolewa na WLAC umekuwa na mafanikio makubwa  kwani umeweza kuwasaidia wanawake kwa kuwawakilisha makahamani hadi  kurudishiwa nyumba walizokuwa wamenyang’anywa na ndugu wa marehemu kama urithi.

Anasema katika utafti wao mikoani wamebaini wanawake bado wananyanyaswa, wanapigwa na waume  lakini  hawako tayari kuwasema kwenye vyombo vya dola na kuongeza wameshuhudia ndoa nyingi zimevunjika kwa sababu ya mtoto kuzaliwa na kichwa kikubwa au mdomo wa wazi yaani wa sungura.

Lwanga anasema tatizo la watoto kukimbilia mjini na kuwa kuombaomba linatokana na ndoa kuvunjika, elimu ndogo kwa akina mama ya kutojua sheria zinazowapa haki yao, umasikini na mila potofu.

Anasema asilimia kubwa ya wananchi hasa wa vijini wanaishi kwa kuzingatia mila zao, hawajui  mabadiliko yaliyopo, wananyanyaswa kwa njia ya ngono, kiuchumi, kishambulio na kisaikolojia lakini hawajui namna ya kujisaidia kisheria kwani tangu awali Serikali haijaweka misingi ya kuwalinda wananwake na kuwapa uhuru.

Pamoja na mambo mengi ya unyanyasaji wa wanawake, Lwanga anaitaka Serikali kuacha mazoea ya kutegemea asasi, mashirika na ufadhili wa mataifa makubwa ya nje kuja nchini kutatua matatizo yanayowakabili wananchi wake badala yake inapaswa kupeleka elimu vijijini hususani katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.


Lwanga anasema kwamba ukatili unaofanywa dhidi ya wanawake nchini hauwezi kuvumiliwa ambapo anawataka  wanawake kuwafikisha wanaume kwenye vyombo vya dola aple wanapotendewa vitendo vya unyanyasaji.

Anasema binadamu yeyote anapofanyiwa ukatili  humsababishia kuwa na maumivu au athari kimwili, kiakili na kisaikolojia ambapo mwanamke anapofanyiwa ukatili huo athari kubwa kuliko mwanaume.

Anasema hivi sasa WLAC kwa kushirikiana na wakuu wa utekelezaji wa kampeni ya TUNAWEZA  wamedhamiria  kufikisha elimu ya ukatili wa kijinsia kwa watu 1,600,000 ifikapo mwaka 2013 ikiwa lengo ni kupunguza vitendo hivyo kwa wanawake ambavyo vimeonekana ndani ya jamii ni vitu vya kawaida.

Lwanga anasema madhumuni ya WLAC ni kutoa msaada wa sheria juu ya masuala yanayowakabili wanawake kama ndoa, mirathi, mikataba, kusimamia kesi mahakamani, kuendesha semina, ziara za mafunzo na kuhamasisha umma kuhusu haki za wanawake na watoto.

Pamoja na mambo mengi , wanasheria wa WLAC waliahidi kuendelea kutoa msaada wa kisheria mikaoni bure kwa wanawake na watoto ikiwa lengo ni kuleta usawa wa kijinsia Tanzania.

Hivyo sasa wakati umefika kwa Seriakli kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha vitendo vya unyanyasaji kijinsia vinakomeshwa haraka, pia vitendo vilivyoibuka hivi karibuni vya mateka kwa watu wanaopigania haki zao havipaswi kufumbiwa macho.

Tunapaswa kutambua kwamba katika hali halisi binadamu wote wamezaliwa huru huru na wote ni sawa mbele ya sheria hivyo hakuna mwenye haki ya kumfanyia mwenziwe ukatili wa aina  yoyote.

Vitendo hivi vinapofanyika ni kinyume cha sheria na mikataba mbalimbali ya haki za binadamu ambayo Tanzania imekuwa ikiisaini ili kushirikiana na mataifa makubwa kupambana na vitendo hivyo, sasa ni mwito kwa serikali kutekeleza mikataba hiyo kwa vitendo na sio maneno tupu. Maoni benjaminmasese@yahoo.com, 0655/0769-688300


MWISHOOO  





Wakina mama wa kabila la Wangoreme wakifurahi wakati wa sherehe


 
A Rwandan women's group celebrates the arrival of their cows from the charity Send a Cow. Sent in by BBC News website reader Kirstine Dunhill
 

Kabila la wangoreme na wakurya mkoani Mara wanavyokuwa wakisherekea shehehe za, harusi, kutahiriwa au kukeketwa. (chanzo. BBC Swahili)

DAR CITY 2013

Mwandishi wa Habari wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Dar es Salaam City Press Club (DCPC),Benjamin Masese (kulia) akiwa na mdogo wake , Boniphace Wanka (IFM)

Monday 12 August 2013

SERENGETI ILIVYOVAMIWA VIJIJI VYAKE



HISTORIA YA WANGOREME

Na Benjamin Masese, Dar es Salaam
MKOA  wa Mara ni miongoni mikoa ya Tanzania Bara ambapo  mji wa Musoma  ndipo makaoa makuu ya mkoa huo.
Mara imepakana na mikoa ya Mwanza na Shinyanga  upande wa Kusini, Arusha upande wa Kusini-Mashariki, Kagera  upande wa Magharibi mwa Ziwa  Nyanza au Viktoria na Kenya upande wa mashariki.
Idadi ya wakazi ni zaidi ya milioni mbili na makabila ni mengi kuliko mikoa yote ya Tanzania ispokuwa Jiji la Dar es Salaam.
Baadhi ya makabila yaliyopo Mkoa wa Mara ni wajaruo, wajita, waruri, wazanaki, wakabwa, wakiroba, wasimbati, wangoreme, wakwaya, waikoma, wanata, waisenye, waikizu, wasizaki, wasukuma, wataturu ne mengine wengi.

Kuna wilaya ya saba ambazo ni Bunda, Serengeti, Tarime, Rorya, Butiama, Musoma Mjini na Musoma Vijijini.
Katika makala ya leo nitazungumzia kabila wa Wangoreme wanaoishi Wilaya ya Serengeti. Wangoreme wametokea Carogos nchini Ghana miaka mingi iliyopita.
Kabila la Wangoreme na Waikoma  mzazi wao ni mmoja aliyejulikana kwa jina la Sabayaya Wandira ambaye ni miongoni mwa msafara wa mtandao uliokuwa ukitoka Misri kupitia Somalia hadi Kenye ambapo waliingilia Mto Mara na kuweka makazi yao Serengeti.
Msafara mwingine wa kabila wa Wangoreme iliingia Serengeti kupitia njia ya Mkoa wa Manyara na baadhi yao kuweka makazi yao hapo.
Vijiji vya kabila la Wangoreme vilivyoitengeneza Wilaya ya Serengeti  ni Mugumu,Ikorongo, Borenga, Nyiboko, Buchanchari, Nyansurumunti, Mto Mara (Ghitende), Wigero, Baranga, Sirori Simba, Remng’orori , Mikomariro.
Vingine ni Mto Msamo-Tirina, Manchemwero, Nyankomogo, Issenye, Rigicha, Wegete, Nata, Rubana na kuunganisha tena Mugumu ambapo ndipo makao Makuu ya Wilaya ya Serengeti.

Lakini Vijiji hivyo vimevamiwa  na kabila la Wakurya wenye asili koo ya waasi kwa upande Magharibi, upande wa Kusini pamevamiwa na Waikizu na Waisenye na upande wa Magharibi wamevamia wakurya halisi kutoka Kenye na Tarime.
Pamoja na uvamizi huo lakini kabila la Wangoreme wameungana na kabila la Waikizu, Wanata na Waisenye na kuwa kitu kimoja tofauti na Wakurya wenye tabia tofauti ya ukatili na wizi wa mifugo.
Miiko ya Wangoreme

Mtu aliyeua mwenzake- Kabila la Wangoreme wamekuwa na miiko yao kulingana na tukio lenyewe, kwa mfano mtu aliyeua mwenzake ukiachia masuala ya kisheria, mara nyingi ukoo wa pande zote mbili hukaa na kukubaliana fidia ambayo ni idadi ya ng’ombe kuanzia saba na mbuzi au kondoo saba.
Baada ya fidia hiyo hufanyika matambiko fulani ambayo huashiria kusameheana  na kushiriki kula chakula pamoja.
Mwanamke aliyeshindwa kujifungua- Mwanamke aliyeshindwa kujifungua mtoto akiwa ndani ya ndoa au nje ya ndoa (ukiacha masuala ya kiafya), mara nyingi huadhibiwa kwa kupakwa majivu kama mchawi.
Mbali ya majivu hayo hunyolewa nywele kwa kutumia aidha chupa, wembe,mkasi na kisu huku akikatwa au kung’atwa kichwani  na kufanyiwa vidonda vya makusudi, pia huanza kufanya kazi kabla ya kupona.
Kuoa-Katika suala la kuoa au kuolewa mara nyingi wazazi wa kijana  ndio wanaochagua binti wa kuoa wakati upande wa binti wazazi hufuatilia historia ya jina na wazazi wao kama wana sifa ya kuwa ndugu wa kuoana.
Idadi halisi wanawake wa kuona ni kuanzia wawili hadi wadi wanne inategemea utajiri wa mtu mwenyewe na wingi wa shughuli zake.
Baada ya kuoana, marafiki wa pande zote mbili walisiosimamia ndoa hiyo hufanyiwa matambiko ya kupakwa mafuta ya ng’ombe usomi  ikiwa ni laana ya kutoibiana wala  kutembea na mke wa mwenzie.
 Mahali za kuoa mwanamke enzi za mababu zetu ilikuwa ni ng’ombe 80-60, enzi za baba zetu 50-30 lakini hadi sasa  20-6 ambapo thamani ya ng’ombe mmoja sasa ni Sh 300,000- 500,000.
 Wanawake kuoana ‘nyumba ntobhu’
Suala la wanawake kuoana ni jambo ambalo linafanywa na Kabila la Wangoreme na Wakurya, hii hufanyika pale aidha mwanamke anapojifungua watoto wote wa kike na kuolewa wote.
Pia hutokea pale mwana mke anapokuwa ndani ya ndoa lakini haukufanikiwa kupata mtoto  hata mmoja ambapo hulazimika kuoa mke mwenzake na kumpa uhuru wa kuzaa na mtu yeyote au kumchagulia mwanaume ndani ya familia au ukoo wake.
Lengo kuu la mke kuoa mke mwenzake ni kupata mtoto wa kiume ili kuendeleza ukoo wake na kusimamia mali zake alizonazo.

Hukumu ya Wangoreme-Ukiweka pembeni sheria, hukumu kubwa ya Wangoremaikiwa umefanya kosa kisha unakana  kukusanywa vitu vinavyoaminiwa ni hatari kwa afya yako na kulazimishwa kuviruka, pia kuna fuvu la kichwa cha binadamu ‘ekehore’ ambalo huwekwa maji machafu ya nguo zako na kunyweshwa.
Kukeketwa/kutahiriwa-Enzi za mababu wetu kijana au binti kutahiriwa-kukeketwa ni miaka 18-25 kwa kutumia kisu na wembe lakini kutokan na mabadiliko ya teknolojia jinsia ya kike imepigwa marufuku.
Pamoja na kupigwa marufuku bado ukeketaji unaendelea kwa jinsia ya kike na vitendo hivyo hufanyika kati ya umri mwaka mmoja hadi mitano kwani imani ni kupunguza hamu ya kujamiliana. Pia Wangoreme wanaamini kuoa mwanamke ambaye hajakekeketwa ni kuleta mkosi au haramu nyumbani.
Mapigano ya ukoo-Awali kulikuwa na mapigano ya koo na koo ambapo yalimalizwa kabisa kwa kuanzisha utaratibu kubadilisha watoto katika pande mbili jambo hilo husimamiwa na mabalozi wa nyumba kumi.
Ni kwamba kama mwanamke amejifungua watoto zaidi ya watatu anachukuliwa na kukabidhiwa koo nyingine hivyo upande wa pili kitendo ambacho kimewafanya kuwa kitu kimoja yaani ndugu wa damu.
Chakula,ufugaji-Asili ya Wangoreme ni wafugaji wa wanyama aina ya ng’ombe, mbuzi, kondoo, kuku na ndege aina ya kuku, bata, njiwa ambapo viumbe hivyo hutumika kama kitoweo, kitega uchumi.
Pia mazao yanayolimwa na Wangoreme ni mahindi, mtama, mihogo, viazi vitamu, maboga, ulezi ambapo zao kuu la  biashara ni pamba, ufuta, karanga  na Tumbaku.

Mboga halisi ya Wangoreme ni majani ya kunde,maharage, mlenda, msusa, mchicha na wakati wa kubadilisha au kuwapo kwa mgeni ni dagaa, nyama, samaki  na vitoweo vingine.
Masharti katika Chakula.
Miiko ya wangoreme ni kwamba wamefanya mgawanyo katika suala la nyama, kwanza vijana wametengewa kula kidali, wanawake wametengewa kula shingo, bibi miguu na baba na wazee wengine moyo na mgongo.
Ikibainika mmoja amekula sehemu ya nyama ya kundi fulani inaweza kuleta ugomvi mkubwa na hata aliyekula atakwenda kuinunua dukani na atashitakiwa kwenye vikao vya familia.

Mgeni wa heshima anapotembela rafiki yake anachinjwa mbuzi, ng’ombe au kuku lakini moja ya sharti ni kwamba kama amechinjiwa yeye lazima ale filigisi na asipoiona mezani atasusa kula.
Nguo- Asili ya nguo za kabila la Wangoreme enzi hizo zilikuwa ni ngozi za wanyama hasa mbuzi na swala  ambapo zilikuwa zinaambwa na kuondolewa nywele zote na aliyeruhusiwa kuzivaa ni kijana mwenye umri miaka 18 na kuendelea lakini baada ya nguo kuja walianza kuvaa hadi leo.
Silaha-Silaha kubwa  ya kabila la Wangoreme ni upinde na mikuki ambapo mafunzo ya kutumia zana hizo hufanyika wakati wa jando.
Ili kuhakikisha umekuwa hodari na mtaalamu wa silaha hizo lazima vijana hao wanaagizwa hifadhini kuwainda wanayama na kuleta nyama nyumbani.
Msiba,wizi- Wakati wa msiba, watu wote wa jirani na ndugu hujumuika pamoja kushiriki mazishi.
 Lakini mzee anapofariki asiyekuwa na mali mara nyingi anazikwa kama alivyozaliwa na ili kuepusha kuzikwa hivyo huwa na utaratibu wa kuweka mtoto wake wa kike rehani kwa mtu mwenye uwezo ili ampe ng’ombe ya kushughulikia msiba.
Mtoto anapokuwa mkubwa ataolewa na kijana wa yule aliyetoa msaada kwa familia ya marehemu aidha kwa kuongeza mahali nyingine au ile ya awali inategemea na wakati uliopo.
Kwa upande wizi unapotokea ndani ya kabila la Wangoreme lazima itapigwa baragumu ikiashiria hatari na watu wote huondoka nyumbani na upinde, mikuki  wakiwa tayari kwa lolote.
Nyumba, Vitanda-Nyumba za asili za Kabila la Wangoreme ni msonge ambazo zinajengwa na miti lakini kwa upende wa mwezekaji nyasi hutafutwa mtaalamu ili kuzuia maji ya mvua yasiingie ndani.
Kwa upande wa vitanda vya asili ni kuunganishs miti kwa mfani wa kitanda cha kisasa lakini panapotakiwa kuweka change inaambwa ngozi ya ng’ombe.
Nyimbo
Pia nyimbo zao za asili ni zeze na ngoma aina ya mbegete, kinanda, lukana ambapo zinapopigwa huchezeshwa mabega huku wanawake  na wanaume husogeleana kwa kukusana vifua.
Maoni -O769 688300 
================

MIPAKA YA VIJIJI ITATUGHARIMU BAADAYE

 


Mapigano ya mipaka ya majimbo yazuka Mara
*RC aizuia tume ya wizara
*Asema ilienda kinyemela
*Wassira, Dk. Kebwe wanena
*Mipaka yang’olewa
*Wananchi waahidi kumwaga damu

Na Benjamin Masese, Dar es Salaam
MAJIMBO  matatu ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mara yameingia katika mvutano  mkali wa kugombea mipaka yao  huku dalili za wazi za wananchi kushika mapanga, mishale na upinde zikianza kuonekana.
Mipaka hiyo ni  ile inayotenganisha Wilaya ya Musoma Vijijini, Serengeti, Bunda  ambayo inahusisha vijiji vya Sirori Simba(Musoma Vijijini), Remng’orori (Serengeti) na Mekomariro (Bunda).
Mgogoro wa mipaka hiyo ulianza kuibuika kwa mara ya kwanza mwaka 1978 lakini  hakuna suluhisho lililopatikana licha ya mikutano kadhaa kufanyika ikiwahusisha viongozi ngazi ya mkoa.

Waliovamia maeneo ya mipaka hiyo ni  wafugaji, wakulima huku wakianza kuweka makazi ya kudumu na shughuli za kijamii ambapo pande zote  zikidai yuko Wilaya yake.
Dalili za kuanza mapigano hayo zilianza kuonekana mwanzoni mwa mwezi huu baada ya wananchi wa Wilaya ya Musoma Vijijini kung’oa mabango  ambapo wananchi wa Wilaya ya Bunda wao wakichimba mitaro na kuweka alama za mipaka inayowatenganisha  na Wilaya ya Serengeti na Bunda huku wakitoleana vitisho.
DC Serengeti
Akizungumza na MTANZANIA juzi kwa njia ya simu, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Joshua  Mirumbe alikiri kuwapo na mgogoro huo huku akisema kuwa umeanza kushughulikiwa na ngazi zote.
“Ni kweli upo mgogoro huo naohusisha wilaya tatu lakini kutokana na uzito wa suala hilo tayari tume imetoka Makao Makuu ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuja kushughulikia mipaka hiyo.
“Hivi tunavyozungumza viongozi ngazi ya mkoa, wilaya, kata, tarafa, vijiji wanashirikiana pamoja kuhakikisha kila mmoja anapata haki yake bila kuingia katika mapigano,”alisema kwa ufupi.

RC Mara
Akizungumza jana kwa njia simu, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Gabriel Tupa alikiri kuwapo na mgogoro huo huku akiwaomba wananchi kutoingia kwenye mapigano ya wao kwa wao kwa kuwa athari yake ni kubwa.
“Mgogoro huu ni mkubwa na ndio maana watalaam kutoka makao makuu ya Wizara ya Ardhi wameletwa ikiwa lengo ni kupata suluhisho lisilopendelea upande mmoja.
“Hasira za wananchi zilitokana na watalaam hao kwenda kwa wananchi bila kuwa na wakuu wa wilaya zote tatu huku wakitumia jina langu kwamba nimewaagiza.
“Kwa kweli walikosea na ndio maana nimewasimamisha kwanza na kuwaagiza wakuu wa wilaya wazungumze nao kwa kuwapa elimu na kuwashauri watoe ushirikiano ili wote kwa pamoja tupate suluhisho la kudumu.
“Kikubwa ninachosema  ni kwamba uamuzi wa mgogoro huu upo mikononi mwao lakini kama wamejiandaa  na mapiganoya mikuki, mishale na mapanga ni kuongeza tatizo.
“Nawasihi watoe ushirikiano kwa kuwa kamati zote zitaundwa  na wao ambapo watatoa historia yote ya mipaka kwa tume ya wizara ili kupata taswira halisi, pia nawaomba wananchi kuwa na subira hadi tume itakapokamilisha kazi yake,”alisema.
Mwenyekiti Remng’orori
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Remg’orori, Justen Mgaya Baritile alisema  mgogoro huo umedumu kwa miaka mingi.
Baritile alisema kuwa mipaka iliyokuwa ikitambulika tangu enzi hizo ni ile ya mwaka 1978 lakini umekuwa ukisusua kupata suluhisho la kudumu.

Alisema baada ya mgogoro huo kuibuka tena mwaka 1996 kulifanyika mkutano katika eneo hilo la mipaka iliyohusisha viongozi wote ngazi ya mkoa, wilaya na wananchi wa pande zote tatu hazikuafikiana.
Licha ya kutoafikiana katika mkutano huo, maafisa watendaji wa kata inadaiwa walisaini makubaliano hayo bila wananchi kuiridhia.
Baritile alisema kuwa mgogoro huo tena uliibuika mwaka 2002 ambapo  kulifanyika mkutano eneo hilo hilo na kuhudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Thomas Loi Sabaya (wakati huo), Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Hawa Mchopa ambaye pia alihudhuria kama Kaimu Mkuu wa mkoa wa Mara.
Alisema mkutano huo ulikaa  Februari 28 ,2002 ambapo walipendekeza kuwa mpaka wa Bunda na Serengeti utapita kuanzia mto mwikoma, Nyagubesi, Nyabetunguri, mlima bikaili hadi jiwe moja, Kewaiwai, Bonde la mtemi Makongoro hadi Mto Tirina.
Mpaka kati ya Serengeti na Musoma Vijiji walipendekeza kupita Kijiji cha Sirori Simba eneo la  Bonde la Nyagubesi, Nyabetunguri, mlima Buruta hadi palipowekwa vibao vya Tanroad barabarani kama ishara ya mwisho  wa jimbo la Musoma Vijijini.
 
Alisema kuwa licha ya kukubaliana lakini mgogoro huo uliendelea kufukuta na kulazimika tena kukaa mkutano Desemba 12, 2002 na kuhudhuria na viongozi wa ngazi kuanzia mkoa hadi kijiji ambapo waliwatumia wazee maarufu na wa kale ili kutoa historia.
Hata hivyo taarifa
Kwa Mwenyekiti (0786480194) wa Kijiji cha Sirori Simba, Alexander Makile Nyangalesi alisema kuwa maamuzi yatakayotolewa na tume yatakuwa ni sahihi.

Wassira
Kwa upande wa Mbunge wa Jimbo la Bunda (CCM), Steven Wassira alikiri kuwapo na mgogoro huo huku akienda mbali na kusema unahusisha wilaya nne yaani Serengeti, Bunda, Butiama na Msoma Vijijini.
Wassira ambaye ni Waziri wa Ofisi ya Rais, alisema migogoro yote ya wilaya hizo inahusu mipaka ambayo inapaswa kutenganisha Serengeti na Bunda, Serengeti na Musoma Vijijini na Butiama na Bunda.
Wasira alisema kuwa mipaka ya Wilaya ya Serengeti, Bunda na Butiama inahusisha vijiji vya Mikomariro, mahanga na Ikizu ambapo upande Musoma Vijijini na Serengeti unahusisha kijiji cha Sirori Simba na Remng’orori.
Pamoja na ufafanuzi wake, alisema mipaka hiyo itapata muafaka kwa kurejea historia ya tangu watawala  wa ‘machifu’ walivyokuwa wakitawala.
Wassira alipinga vikali juu ya tuhuma dhidi yake kwamba  anawatumia  matajiri  wa jimbo lake kuendeleza mapambano ya kumega ardhi ya Serengeti.
“Sina nia ya kuchukua ardhi ya Serengeti, hayo ni mawazo potofu ya wenye nia mbaya na mimi,kwanza kwenye jimbo langu sina matajiri na wananchi wangu ni wa hali ya kawaida.
“Kwanza mipaka ya wilaya hizo iliwekwa wakati mimi nikiwa Mkuu wa Wilaya, sasa kama nilikuwa na nia hiyo ningetumia mwanya huo, suala la watu kunichafua kwenye mitandao ya kijamii ni ijinga, tushirikiane kupata muafaka,”alisema.
Dk. Kebwe
Kwa upande wa Mbunge wa Serengeti, Dk. Kebwe Steven Kebwe alisema kwa ufupi kwamba ana imani na tume itamaliza mgogoro huo.
Kuhusu tuhuma za wananchi wakewakidai kushindwa kuitetea ardhi yao, alisema kuwa hatua ya tume kwenda eneo hilo ni jitihada zake na vikao vyote vya RCC kilichokaa Oktoba 17,2012 aliwatetea wananchi juu ya mipaka hiyo.

MWISHO