Monday 9 September 2013

MTANDAO WA WIZI WA FEDHA HALMASHAURI

  IMEGUNDULIKA kuwapo na mtandao hatari nchini unaohusisha Hazina na Halmashauri mbalimbali kuchota mamilioni ya fedha huku wakiziandikia kutumika katika miradi ya maendeleo. Mtandao huo ambao umeelezwa kuwahusu viongozi ngazi ya juu wa Hazina na Halmashauri umekuwa ukiongeza fedha za ziada kati ya Sh. Milioni 500 hadi 600 kwenye fedha halali za miradi ya maendeleo zilizoidhinishwa kisheria na Bunge. Tayari mtandao huo umedaiwa kufanikiwa kuidhinisha mamilioni ya fedha katika Halmashauri tatu ambazo ni Mbarali, Korogwe Mjini na Mvomero. Hayo yalielezwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Rajab Mohamed Mbarouk alipokuwa akifanya majumuisho ya vikao vya kamati yake. Mbarouk alisema kumeibika mtandao hatari wa kujichotea fedha za Serikali kwa kusingizia zinakwenda Halmashauri lakini zinapofikishwa huko zinawarudia wenyewe. “Hii nchi sio masikini na hakuna sababu ya kusikia eti miradi imekwama kwa sababu ya fedha kukosa, katika vikao vyetu tumebaini kwamba Hazina na Halmashauri nchini zinashirikiana kula fedha za Serikali. “Mfano halisi ni huu Halmshauri ya Mbarali katika mahesabu yamahitaji yao yote walitakiwa kupewa Sh. milioni 70 lakini Hazina walipeleka Sh. milioni 700. “Fedha hizo zinapofikishwa kule zinaidhinishwa kupokelewa Sh. milioni 70 zilizokuwa zikihitajika zile zilioongezwa zinazrudi mikononi mwa mtandao huo ambao ni katika Hazina na Halmashauri. “Halmashauri ya Mbarali imekuwa imekuwa ikipata hati chafu mpaka leo ninavyoongea hapa katika kuboroga kwenye mahesabu yao ya fedha wanazopokea na jinsi wanavyozitumia. “Kama unataka kuona mtandao huo umeota mizizi mikubwa, tumebaini utakaswaji wa fedha umefanyika Halmashauri ya Korogwe Mjini Sh.milioni 500 huku mahitaji yao yakiwa chini ya Sh. milioni 100. “Hivyo hivyo utakaswaji huo umefanyika Halmshauri ya Mvomero kwa kupelekea Sh. milioni 500 ambapo mahitaji yao hayakuwa yanafikia kiasi hicho, kama wana kamati tumechukizwa na utoroshwaji wa fedha hizo na tutalifikisha bungeni kwa hatua zaidi. “Cha ajabu unakuta viongozi wanaohusika katika Halmashauri hizo wanapofanya utakaswaji huo wanawahi kuhama, mfano halisi ni aliyekuwa Mhasibu wa Halmshauri ya Mvomero,Nassoro Mkwanda ambaye hivi sasa yupo Halmshauri ya Kiteto kwa cheo hicho hicho,”alisema. Mbarouk alisema kama mtandao huo hautadhibitiwa haraka taifa litaendelea kufilisika na maendeleo ndani ya jamii yakikwama ambapo athari yake ni uchumi kushikiliwa na wachache huku kundi kubwa ni masikini. Mkurugenzi Kiteto amwaga machozi Awali ya yote, Kamati ya LAAC ilikutana na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kupitia mahesabu yao ambapo ilikubaini ubadhirifu mkubwa wa fedha kitendo kilimfanya Mkurugenzi halmashauri hiyo, Jane Mutagurwa kulia ndani ya kikao. Kugundulika kwa ubadhiri katika Halmshauri hiyo kulimfanya Mwenyekiti wa LAAC, Mbarouk kuagiza polisi kufika hapo ili kuwaweka chini ya ulinzi baada ya kikao kumalizika. Kamati ilibaini Halmashauri ya Kiteto imepoteza Sh. milioni 500 ambazo ambazo ni mapato ya kodi za mazao kutoka kwa vyama vya ushirika. Ilibainika fedha hizo zilichukuliwa na wakala wa ukusanyaji wa ushuru huo kwa idhini ya Halmashauri hilo kwa mkataba wao lakini wakotomea bila kuzikabidhi. Katika mahojiano kati ya wabunge wa kamati ya LAAC na viongozi wa Halmashauri hiyo ilibainika kuwa kuna magari mawili ya Serikali yenye usajili wa STK hayajulikani yalipo na anayeyamiliki licha ya kuonekana kwenye vitabu vyao ni mali zao. Pia ilibainika kuwa Sh. milioni 179 zimeanzwa kulipwa kwa watumishi wanaoidai Halmashauri hiyo lakini hawajulikani kwa majina wala idara zao. Vile vile imegundulika kwamba Halmashauri hiyo imekutumia Sh.milioni 34 zilizotokana na mauzo ya mahindi ya msaada wa njaa iliyoikumba Wilaya ya Kiteto na hazijawahi kurudishwa Ofisi ya Waziri Mkuu. Ubadhirifu mwingine uliopatikana katika Halmashauri hiyo ni ujenzi wa jiko la kisasa lililogharimu Sh. milioni 25 lakini limeshindwa kutumika na badala wameligeuza kuwa nyumba ya mwalimu huku taarifa zao zikieleza vitu vyote vimekwekwa kumbe ni uongo. Hata hivyo ilibainika mamilioni ya fedha yanayotengwa na Serikali kwemnda miradi mbalimbali ya maendeleo vijijini na mfuko wa kuwawezesha wanawake na vijana hayawafikii ipasavyo. Ilibainika miradi mingi ya ujenzi wa shule za msingi na Sekondari ikiwani ya Kiperesi ikishindwa kukamilika huku fedha zilizotengwa zikiwa zimetolewa kitendo ambacho kiliwafanywa wajumbe wa LAAC kupendekeza kuvunjwa kwa Halmshauri hiyo. Wakati Mkurugenzi, Mutagurwa alipotakiwa kutoa majibu ubadhiri huo alipatwa na wasiwasi na kigugumizi kueleza wazi na kuanza kulia. Viongozi wengine waliokuwa wamsaidia kujibu hoja ni Ofisa Mipango wa Halmashauri hiyo,Rabson Magesa, Mwenyekiti wa Halshauri ya Wilaya ya Kiteto, Mainge Lemalali na viongozi wengine ambao ilionekana kumsukimia mkurugenzi wao. Kutokana na kutokuwapo na majibu sahihi, Mbarouk alimua kuwatoa nje viongozi wengine ispokuwa Mkurugenzi ili kuhoji peke yake ambapo ilibainika kwamba viongozi waliomzunguka wanamhujumu huku jamii ya wamasai wakimdharau ni jinsia yake ya kike. Mbarouk aliamua kusiktisha mpango wa kumweka chini ya ulinzi wa polisi baada ya kuelezwa hivyo na kuamua kuunda kamati ndogo ya kuchunguza ubadhirifu na hali halisi ilivyo Kiteto. Pia alipewa muda wa kuhajikisha fedha pamoja na gari mbili zinapatikana kabla ya Disemba 31, mwaka huu ingawa aliomba kuongezewa muda hadi Juni 2014 kitendo kilichopingwa vikali. MWISHO.

WALEMAVU WANAVYOTESEKA DAR ES SALAAM

Siri nzito ya walemavu wanavyoteseka Dar.

 INASIKITISHA na kuleta huzuni ndani ya moyo wako pale unapojikuta unawapoteza wazazi wako wote huku ukikosa msaada kutoka kwa ndugu wa karibu na kuamua kujiunga na kundi la ombaomba barabarani. Baadhi ya watu wanao kuwa wakiomba msaada hasa wale walemavu wa viungo mbalimbali wa mwili wamekuwa wakileta huzuni kwa wapiti njia kutokana na ulemamavu wao ambao ni mipango ya Mungu. Sote ni mashahidi kuwa baadhi ya walemavu wa mikono, miguu, vipofu na viungo vingine wakiomba msaada kwa madereva, watembea kwa miguu na kwenye ofisi za Serikali na binafsi na maeneno mengine. Lakini wapo wengine ambao hawana tatizo lolote lakini wameamua kuingia katika kundi hilo jambo ambalo limekuwa likizua maswali ya kwamba kwanini wasijishughulishe na biashara ndogondogo. MTANZANIA Jumatatu ilifanya mahojiano na mlemavu mmoja wa miguu yote ambaye amekuwa akitembea mithili ya mnyama mwenye miguu minne wakati akiomba msaada katika kituo cha daladala Ubungo. Mlemavu huyo aliyejitambulisha kwa jina la Yusuph Said (24) mzaliwa wa Kijiji cha Mikese mkoani Morogoro anaeleza maisha anayoishi eneo la Manzese Darajani jijini Dar es Salaam ambayo ni hatari kwa usalama wa uhai wake. Said ambaye alisoma Shule ya Msingi Kitega na baadaye kujiunga na Sekondari ya Mikese zote za mkoani Morogoro anaeleza kwamba alikimbiwa na ndugu zake baada ya wazazi wake wote kufariki 2000 kutokana na maradhi mbalimbali. Akizungumza kwa huzuni ya kuwapoteza wazazi wake ambao walikuwa wanamlea kulingana na hali yake ya ulemavu alijikuta akikosa mtu wa kukaa naye kitendo kilichomfanya kukimbilia kwa shangazi yake Muhombola Salum. Said anasema alikimbilia kwa shangazi yake baada ya ndugu zake wa kuzaliwa tumbo moja kumkimbia na kuanzisha maisha yao maeneo mengina huku shughuli zao kubwa ni kuchoma mkaa porini. Anasema maisha kwa shangazi yake yalizidi kuwa magumu kutokana na kutokuwa na uwezo kwani uhakika wa kula kila siku haukuwapo ambapo alishindwa kuvumilia njaa na kukimbilia Dar es Salaam baada ya kupata taarifa kuwa walemavu wanapata msaada barabarani kwa kuombaomba. Hakika, ukimtazama Said hali yake ni vigumu kuvumilia kumsikiliza au kumwangalia kwani mwili wake unaonekana kutooga siku nyingi, nguo chafu, shuka analojifunika chafu ana anatembea nalo muda wote kwa kuhofia kumwibia. Pia inadhihirisha kabisa ameanza kuathirika kisaikolojia kutokana na mazingira anayoishi na inathihirisha wazi ameanza kutumia dawa za kulevya. Said ambaye alikataa kuweka wazi vitendo wanavyofanyiwa walemavu wanaoishi eneo la Manzese Dar es Salaam nyakati za usiku kwa kuhofia maisha yakwe, anasema anatamani kurudi nyumbani lakini anashindwa wapi atafikia. “Pale Manzese kuna masela wengi sana, wanatufanyia mambo mengi lakini siwezi kuyataja hapa naogopa na ndio maana sisi walemavu tumejitenga na banda letu. “Hii ni shuka ninayojifunika natembea nayo muda wote kwa ukiachaa unaibiwa, kuoga kwangu au kufua nguo hizi mara nyingi ninasubiri mvua inaponyesha. “Mimi nilikuwa nalelewa na wazazi wangu bila kutekeseka na walikuwa wameninunulia baiskeli lakini walipofariki iliharibika na hakuna aliyenitengenezea lakini nashukuru hadi leo naishi kwa msaada wa watu. “Ukiamua kuwahoji wapiga watu tunaolala nje watakueleza mambo mengi sana, kuna vituko tunafanyiwa sio kwmaba tunapenda ni kwa sababu huna jinsi,”anasema kwa masikitiko. Said anasema kwamba kutokana na kukaa kituoni tena juani kwa kuomba pesa abiria, madereva na makondakta amekuwa akiugua kila siku lakini baada ya kupata kiasi hutenga kwa kula chakula na kununua dawa la kutuliza maumivu. Anasema kwamba anahofia kwenda hospitali kutibiwa kwa kile alichodai hatapewa fursa ya kupata matibabu kwa sababu ya pesa na hali yake ilivyo. Anasema kwa siku inaweza kupata Sh 5,000 lakini kutokana na mazingira anayoishi hazitoshi na kuongeza kwmaba pengine hunyang’anywa na masela nyakati za usiku. Anaeleza kwamba mbali ya kunyang’anywa fedha pia kupokonywa simu jambo ambalo linamfanya kutonunua simu, nguo au kutunza fedha za ziada. Anasema kutokana na hali hiyo hulazimika kuchimba shimo na kufukia baadhi ya fedha zake anazopata kutoka kwa watu wanaoguswa na hali yake. Said aliwataja baadhi ya ndugu wa kuzaliwa ni pamoja na Oluka, Salum, Hiari, Shukuru na Hamis ambao wapo porini wakiendesha shughuli zao za kukata miti na kuchoma mkaa mkoani Morogoro. Pamoja na mambo ya Said lakini ombi lake kubw ani kuiomba Serikali kumsaidia baiskeli ya kutembelea au kumpeleka katika kituo chochote za kulelea watu wasio na uwezo. Said anasema mbali ya kumpeleka kituoni, anaomba msaada wa fedha ili kuanzisha biashara ndogo ambazo anaweza kusifanya kwa kutumia mikono ambayo haina ulemavu wowote. Ni dhahiri kwamba Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto inapaswa kutambua matatizo yanayowapata watu wanaojihusisha na ombaomba barabarani. Inagawa ni vigumu Serikali kuwachukua watu wote walio mitaani na kuwatunza lakini kuja haja ya kuchukulia uzito kwa watu wenye ulemavu hata kwa kuwapeleka katika vituo vya kulelea watu wasio na uwezo. Si kwamba walemavu wote wanapenda kukaa kwenye vituo hivyo la hasha, bali wengine wanataka kupata msaada wa fedha ili kuanzisha biashara ambayo wanaweza kuifanya kulingana na mazingira yao. Pia Serikali inapaswa kuweka wazi juu ya huduma kwa walemavu katika hospitali za umma ili waweze kupata huduma bure kwa sababu ya hali zao ambazo haziwawezeshi kupata kipato cha kujikimu, hii itasaidia pale wanapougua walemavu waweze kupata matibabu kwa sababu wana haki sawa. Walemavu wanapoachwa bila kupewa huduma ni moja ya sehemu ya kuwafanyia ukatili. Sote tunafahamu ukatili ni vitendo vya makusudi vinavyofanywa na mtu au kikundi dhidi ya mtu, watu wengine ambavyo huwa na madhara ya kimwili, kiakili na jisaikolojia. Dhana hii haimanishi kuuawa kwa binadamu pekee bali ukatili unaweza kujitokeza katika sura tofauti na maneno mbalimbali kama ukatili wa nyumbani, kiuchumi, kimila na desturi katika makabila, mahusiano ya kimapenzi, usafirishaji haramu wa binadamu, vitisho na matumizi ya kutumia nguvu. Hivyo watu walio barabarani wakiomba msaada wa kusaidia wapo katika kundi la ukatili wa kiuchumi ndio uliowafanya kuingia barabarani kujipatia riziki zao. Kwa mujibu wa Said amesema kwamba nyakati za usiku hufanyiwa vitendo vya ajabu ambavyo hakuta kuvieleza wazi, lakini kwa akili ya kawaida inadhihirisha kundi hilo linateseka sana . Ukatili unaweza kutoka katika kundi lolote ndani ya juamii ikiwa ni kwa mwanamke, mwanaume, mvulana, msichana au mototo. Ili kutambua madhara ya ukatili wa kijinsia kwa walengwa hao ni muhimu kufanya linalowezekana kuhakikisha vitendo hivyo vinatokomezwa kuanzia ngazi ya familia hadi taifa kuona kila binadamu ana haki katika hali yoyote ile. Ingawa mateso wanayopata walemavu barabarani jamii imekuwa ikiyachukulia pengine ni uamuzi wa mtu kupenda kuingia katika kundi hilo lakini sivyo ilivyo bali inalazimu kutokana na hali halisi ya maisha. Umefika wakati sasa wizara, idara, taassi na kampuni binafsi kuona kundi la walemavu ni moja ya watu wanaopaswa kusaidiwa katika kila hali kwa sababu hayo ni mapenzi ya Mungu. Pia vitendo vya baadhi ya familia kuwatelekeza watoto wanaozaliwa kwa ulemavu au kupata ulemavu wakiwa watu wakubwa ni jambo la kikatili , ni vema mlemavu akadhaminiwa kama ilivyo kwa wengine. Maoni 0769 688 300

UWEZO WA NAIBU SPIKA BUNGENI

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema uwezo wa Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai katika kuongoza Bunge unahatarisha amani, kuvunjika mshikamano na umoja wa kitaifa uliopo sasa kutokana na kutokuwa na mtazamo mpana wa kufikiri. Pia kimesema kuna ajenda ya chini chini inayoendelezwa na baadhi ya mawaziri, wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na kiti cha Spika katika kuhujumu malengo na nia ya Rais Kikwete kuwa na katiba mpya ifikapo 2015. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba alisema kitendo cha Ndugai kuamuru polisi kumtoa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe ni cha aibu na kidikteta. Profesa Lipumba alisema kuna baadhi ya viongozi Serikali (hawakuwataja) wanaojionesha wanamsaidia Rais Kikwete lakini ndani ya moyo wao wana ajenda za siri za kumhujumu. Alisema kuwa viongozi hao wamekuwa wakitumia udhaifu wa Ndugai kwa kumshawishi kufanya kile wanachoona kinafaa kwa lengo la kukandamiza upinzania na kuhmhujumu Rais bila yeye kujua. Alisema kuwa hivi Sasa Tanzania inakabiliwa na changamoto za matamshi hasi yanayotolewa na viongozi na asasi za Rwanda baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa ushauri wenye mantiki kwa Rais wa Rwanda, Paul Kagame kukutana na waasi wa kikundi FDRL kitendo ambacho kimeleta hali ya sintofahamu. Pia alisema kuwa kitendo cha baadhi ya nchi za Afrika Mashariki kufanya vikao vyao na kuitenga Tanzania huku wakizungumzia namna ya kuinua uchumi wao, kitendo ambacho kinamweka Rais Kikwete katika changamoto kubwa. Alisema kuwa kitendo cha kiti cha Spika hasa kinapokaliwa na Ndugai kimekuwa kikiendesha Bunge kwa kupendelea Serikali kwa kadri kinavyoweza huku kikizima hoja za upinzani kwa makusudi. “Kuna njama za wazi zinafanywa na kiti cha Spika kwa kutelekeza maoni ya wananchi na kupendelea ya Chama Cha Mapiunduzi (CCM), kwa upande wa Zanzibar hawakushirikishwa vizuri na hata wabunge wa CUF wanasema hawakushirikishwa. “Moja ya njama za wazi ni ile ya wabunge 166 wa bunge la katiba wanaoipaswa kupendekezwa na taasisi mbalimbali na kuteuliwa na Rais, sisi CUF kinasikitishwa na mchakato unavyoendeshwa na jinsi uteuzi unavyopendekezwa. “Hii katiba mpya itakuwa ni ya CCM sio ya Watanzania, na ombi la wabunge wa CUF ni kutaka muswada urudishwe kwa wananchi na kamati ijadili upya. “ CUF inaendelea na juhudi za kuwasiliana na viongozi wa vyama vingine ili kuweka mkakati wa pamoja na kukabiliana na hujuma dhidi ya mchakato wa kupata katiba mpya na kuimarisha umoja wa kitaifa,”alisema. Profesa Lipumba alisema kuwa kitendo cha Ndugai kumnyima nafasi Mbowe kinadhihirisha ni mpango mkakati wa kuminya hoja za upinzani na kutumia nguvu kumtoa nje ya Bunge hakikubaliki na amevunja sheria. Profesa Ibrahimu alihoji kwamba angesimama Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, je asingepewa nafasi ya kusikilizwa na kuongeza kwamba baadhi ya Wabunge wa CUF akiwamo Mozza Abeid walivuliwa hijabu zao kitendo ambacho ni udhalilishaji.

Sunday 25 August 2013

OPERESHENI YA KUONDOA POLISI WASIOFAA

Na Benjamin Masese, Dar es Salaam WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi ametembeza panga kali ndani ya Jeshi la Polisi na kuwafukuza kazi maofisa wanne huku baadhi yao wakivuliwa vyeo vyao. Maofisa hao ni wale waliohusika kushiriki kwa namna moja au nyingine katika matukio yaliyotokea mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro na Kigoma na kulalamikiwa vikali na wananchi. Akizungumza na Waandishi wa habari Da r es Salaam jana alisema askari hao ni wale waliohusika kutumia gari la kutuliza Ghasia (FFU) kubeba bangi mkoani Arusha na Kilimanjaro Tukio jingine ni lile la askari mkoani Morogoro kutumia fuvu la binadamu kumbambikizia mfanyabishara kwa lengo la kupata fedha, mauaji ya mfanyabishara wa Wilaya ya Kasulu yalifanywa na askari polisi. Tukio la Bangi Dk. Nchimbi alisema katika sakata la tukio la bangi amemvua madaraka yote aliyokuwa nayo Mkuu wa Kikosi cha FFU Mkoa wa Arusha, Mrakibu wa Polisi, Ramadhan Giro kwa kosa la kushindwa kusimamia kikamilifu askari na maofisa walio chini yake na kusababisha kutoke tukio hilo. Pia amemsimamisha kazi Ispekta Isaac Manoni na kushitakiwa kijeshi kwa kosa la kutumiwa kumtorosha mtuhumiwa ambaye ni polisi Edward Mwakabonga aliyekuwa dereva wa gari la FFU kitendo kilicholifedhehesha jeshi hilo. “Katika tukio hilo kitendo cha Inspekta Salum Kingu wa kikosi cha FFU Mkoa wa Kilimanjaro kubaki kwenye gari mita 80 kutoka ilipo nyumba ya mtuhumiwa Edward alipopelekwa Moshi kukabishi vifaa vya jeshi letu kimechangia, hivyo tumempa onyo kali la kuwa makini na utendaji wake. “Pia Inspekta Mikidadi Galilima kutotimiza wajibu wake ipasavyo katika kumshauri Mkuu wa FFU Mkoa wa Arusha juu ya ukaguzi na usimamizi wa rasilimali na kujaribu kuficha ukweli wa tukio, nimempa onyo kali Inspekta Galilima. “Katika tukio hilo nimempandisha cheo ASP Francis Duma aliyekuwa kiongozi wa askari 14 katika kupambana kulikamata gari la FFU lililobeba bangi na kuwa Mrakibu wa Polisi,askari wengine 14 nimegiza Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP, Said Mwema kuwapandisha vyeo kwa sababu wapo ngazi yake,”alisema. Tukio la fuvu Dk. Nchimbi alisema amewavua madaraka yote waliyonayo Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Mvomero, Inspekta Jamal Ramadhan na Mkuu wa Kituo cha Polisi Dumila, Inspekta Juma Mpamba kutokana na kuonyesha udhaifu mkubwa katika utendaji kazi wa kushindwa kuwasimamia askari wake na kushindwa kuwakamata matapeli na hawalifu ambao ni vinara. Dk. Nchimbi alisema kabla ya tukio la askari watatu kushirikiana na raia wawili kumbambikizia fuvu la binadamu mfanyabishara Samson Mwita, Inspekta Ramadhan alikuwa na taarifa za mpango wa tukio hilo la askari wake kushirikiana na rai kufanya kufanya hivyo lakini hakumtaarifa Inspekta Mpamba. Alisema askari wote waliohusika na tukio hilo ambao ni Sajeti Pasua Mohamed, Sajeti Sadick Madodo Koplo Nuran Msabaha wamefukuzwa kazi na kushitakiwa kwa uhalifu waliotenda sambamba na raia wawili ambao ni Rashid Hamisi na Adamu Peter. Kupiga na kuua raia Dk. Nchimbi alisema Disemba 25 mwaka jana askari wa kituo kidogo cha polisi cha Heru Ushingo kilichopo Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma kwa pamoja walimpiga raia ambaye ni marehemu sasa Gasper Sigwavumba na kumweka mahabusu bila msaada wowote wa matibabu. Alisema katika tukio marehemu alipasuka bandama kutokana na kipigo hicho na kuongeza kwamba upelelezi mbovu uliofanywa chini ya usimamizi wa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kasulu, ASP Daniel Bendarugaho kesi ya mauaji iliweza kuondolewa mahakamani. Dk. Nchimbi alisema wakati kesi inaondolewa mahakamani askari waliohusika ambao ni Koplo Abraham Peter na PC Simon Sunday walikuwa wamefukuzwa kazi na kuwa huru jambo ambalo lilizua malalamiko. “Kutokana na ASP Bendarugaho kutokuwa makini katika kusimamia upelelezi wa jalada husika la kesi hiyo ya mauaji tunavua madaraka na upelelezi unaanza upya ili haki itendeke,”alisema. “Operesheni ya kulisafisha jeshi hilo itaendelea hadi litakapokuwa safi, leo hii wananchi wamekata tama kabisa na jeshi la polisi ukimwambia kitu chochote juu ya polisi haamini. “Kwa kipindi nitakachokuwa naongoza wizara hii, nitalisafisha na Watanzania watarudisha imani kwa polisi, katika matukio haya matatu askari waliohusika moja kwa moja wamefukuzwa kazi na kushitakiwa. “Haya ni matokeo ya uchunguzi uliofanywa na timu niliyoiunda ambapo Mwenyekiti wake alikuwa Mkurugnezi Mkuu wa Idara ya masuala ya Malalamiko Makao Makuu, Augostine Shio.

BOMBA LA GESI KUTANDAZWA LEO.26/8/2013



Bomba la gesi ya Mtwara kutandazwa leo
Na Benjamin Masese, aliyekuwa Lindi
BOMBA la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam, linaanza kutandazwa leo likianzia mkoani Lindi.
Kutokana na hali hiyo, Serikali imeonya kwamba, yeyote atakayethubutu kuharibu miundombinu ya bomba hilo, atachukuliwa hatua.
Taarifa hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alipofanya ziara ya kukagua, ubora wa vifaa, rasilimali watu na  maandalizi ya miundombinu ya kutandaza bomba hilo.
Wakati wa ziara hiyo ya siku moja, alikuwapo pia Balozi wa China nchini, Lu Youging, viongozi mbalimbali wa Serikali na viongozi wa kampuni zinazotandaza bomba hilo.
Profesa Muhongo alisema ameridhishwa na maandalizi yanavyokwenda, kwa kuwa kuna vifaa vya kisasa na imara.
Kesho kutwa (leo), utandazaji wa bomba unaanza rasmi na kwa maandalizi niliyoshuhudia, nina imani mradi huu utakamilika kabla ya Desemba mwaka 2014.
“Naomba Watanzania wawe na imani kubwa na watoe ushirikiano kwani utandazaji wa bomba utafanyika katika pande zote mbili, kwa maana ya nchi kavu na baharini.
“Mradi huu ni wa gharama kubwa na kama mnakumbuka, tulikopa fedha kutoka Benki ya Exim ambazo ni Dola za Marekani bilioni 1.2 kwa masharti nafuu.
“Pamoja na kwamba nia yetu ni nzuri, kuna baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya nchi hii, nataka kuwahakikishia Watanzania wote, kwamba usalama wa miundombinu hii utakuwa shwari na kama mtu anataka kushughulikiwa na Serikali, basi ajaribu kuihujumu atakiona cha mtema kuni.
“Hapa tumeshuhudia Watanzania 45 walioanza kupata ajira kama madereva, vibarua, kampuni za usafirishaji, huu ni mwanzo tu na ikifika sehemu ya kuhitaji watu wenye utaalamu, wataajiriwa wenye utaalamu,” alisema Profesa Muhongo.
Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, mabomba yanayotandazwa ni ya aina mbili yakiwamo ya inchi 36 na uzito wa tani tano na yenye inchi 24 yakiwa na tani tatu ambayo alisema kwa ujumla wake yatadumu kwa miaka 30 na kama yakitunzwa vizuri yatadumu hadi miaka 70.
“Tunataka ifikapo mwaka 2016, tuwe na umeme wa megawati 3000 na mwingine wa ziada wa utakaokuwa ukiuzwa nje ya nchi ikiwamo Kenya ambayo imeleta maombi ya kuuziwa megawati 1000,” alisema.
Pamoja na kufanya ziara hiyo juzi, Profesa Muhongo alisema itakuwa ni endelevu na itakuwa ikihusisha waandishi wa habari.
Naye, Balozi Youging, alisema gesi ni kitega uchumi kizuri ambacho kinaweza kuwaondoa Watanzania katika umasikini.
“China ni moja ya nchi iliyonufaika na gesi na ndio maana raia wake ni wataalamu wa nishati hiyo, naamini upatikanaji wa gesi hapa Tanzania, utasaidia Watanzania kuondokana na matumizi ya mkaa na kuni.
Kwa upande wake, Meneja Mradi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania, Mhandisi Baltazari Thomas, alisema hadi sasa watu 163 wamepata  ajira katika awamu ya kwanza na kati ya hao Watanzania ni 68.
 Mwisho.
Rufaa dhidi ya Zombe kusikilizwa leo
Na Kulwa Mzee, Dar es Salaam
MAOMBI ya Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) ya kuongezewa muda wa kukata rufaa dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na askari wenzake wanane walioachiwa huru katika shtaka la mauaji, yanatarajiwa kusikilizwa leo.
Maombi hayo yanatarajiwa kusikilizwa katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam mbele ya Jaji Aloyisius Mujuluzi.
Katika shauri hili, DPP aliwasilisha maombi ya kuomba kuongezewa muda wa kukata rufaa, baada ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, kutupilia mbali rufaa ya awali kwa sababu ilikuwa na makosa ya kisheria.
Rufaa hiyo ilitupwa baada ya kubaini kuwapo kwa dosari katika hati ya kusudio la kukata rufaa na mahakama kukataa kuamuru makosa yaliyojitokeza yafanyiwe marekebisho.
“Kusudio la kukata rufaa ndio linatengeneza rufaa yenyewe, kwa kuwa kuna makosa, hakuna rufaa iliyopo mahakamani, kama makosa yangejitokeza katika rufaa yenyewe, Mahakama ingeweza kutoa maelekezo ya kufanyiwa marekebisho, rufaa inatupwa, Jamhuri ina haki ya kuwasilisha rufaa nyingine nje ya muda, baada ya kuomba kufanya hivyo,” alisema Mwenyekiti wa Jopo la Majaji Watatu, Edward Rutakangwa.

Majaji wengine waliokuwa wakisikiliza rufaa hiyo kabla ya kutupwa ni Jaji Mbarouk Mbarouk na Bethuel Mmila ambao awali walipoketi kwa ajili ya kuanza kusikiliza rufaa iliyokatwa na DPP kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, ziliibuka hoja za dosari katika hati ya kusudio la kukata rufaa.

Zombe na wenzake walikuwa wakikabiliwa na kesi ya mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini wakazi wa Mahenge Morogoro pamoja na dereva teksi mmoja.

Kabla ya jopo la mawakili wa Serikali lililokuwa linamwakilisha DPP ambao ni Mawakili wa Serikali Wakuu, Edwin Kakolaki, Vitalis Timon, Prudence Rweyongeza na Mawakili Revocatus Mtaki na Alexander Mzikila, halijaanza kuwasilisha hoja zao za kukata rufani, Jaji Mbaraouk alilihoji jopo hilo kuhusu dosari hiyo.

“Mahakama inataka kujiridhisha juu ya kinachosomeka katika hati ya kusudio la kukata rufaa, ambayo inasema mnapinga hukumu iliyotolewa na Jaji Massati wa Mahakama ya Rufaa. Sasa hii inakuja kwetu kama marejeo au mapitio," alihoji Jaji Mbarouk.

Hata hivyo, Wakili Timon, alikiri kuhusu dosari hiyo na hivyo kuiomba Mahakama kuwaruhusu kufanya marekebisho na kisha kuendelea kusikiliza rufaa hiyo.

Jaji Rutakangwa alihoji upande wa Jamhuri kuwa hati hiyo ina dosari, kwa kuwa inaonyesha wanakata rufaa kupinga hukumu ya Jaji wa Mahakama ya Rufaa, wakati hajawahi kukaa kusikiliza shauri hilo kwa kuwa si sahihi.

Ombi la mawakili wa Serikali la kuomba kufanyia marekebisho hati hiyo, lilipingwa vikali na mawakili wanaowawakilisha Zombe na wenzake ambao ni Richard Rweyongeza, Majura Magafu na Dennis Msafiri.

Katika shauri hili, mbali na Zombe, wajibu rufani wengine ni polisi Christopher Bageni, Ahmed Makele, Jane Andrew, Koplo Emmanuel Mabula, Michael Shonza, Abeneth Saro, Rajabu Bakari na Festus Gwasab.

Serikali ilikata rufaa hiyo kupinga hukumu iliyotolewa Agosti 17, 2008 na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.

 mwisho.


Nyavu haramu za Sh milioni 150 zateketezwa

Na Ahmed Makongo, Bunda

NYAVU haramu 3,280 zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 150, zimekamatwa wilayani Bunda, mkoani Mara na kuteketezwa kwa moto.

Nyavu hizo ziliteketezwa jana kwa usimamizi wa Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Joshua Mirumbe.

Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, Mirumbe alisema kuwa nyavu hizo ambazo ni pamoja na makokolo ya kuvulia sangara, nyavu zenye matundu madogo, timba na makokolo ya dagaa, zimekamatwa na vyombo vya dola kutokana na msako unaoendelea wilayani hapa.

Alisema kuwa msako huo unashirikisha askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), polisi, mgambo pamoja na maofisa wa idara ya uvuvi.

Alisema operesheni hiyo aliianzisha mwenyewe na kwamba itakuwa endelevu kwa kuwa lengo lake ni kutokomeza wavuvi haramu wilayani hapa.
Ili kuhakikisha uvuvi haramu unakomeshwa wilayani hapa, aliwataka viongozi wa Serikali za vijiji, kata na Vikundi vya Ulinzi wa Rasilimali za Ziwa Victoria (BMU), kuhakikisha wavuvi haramu wanakamatwa.

Alisema kama uvuvi haramu utaendelea katika baadhi ya maeneo, kitakachofuata ni kukamatwa kwa viongozi wa maeneo utakakokuwa ukifanyika uvuvi huo.

“Hatua ifuatayo ni kukamata viongozi wa Serikali za vijiji na kata na wale wa BMU ambao tutakuta kwenye maeneo yao kunaendeshwa shughuli za uvuvi haramu,” alisema Mirumbe.

Aliwaonya viongozi hao kutojihusisha na shughuli za uvuvi haramu, kwa kuwa inasemekana baadhi yao wanafadhili wavuvi hao.

Naye, Ofisa Uvuvi wa Wilaya ya Bunda, Stephen Ochieng, alisema nyavu hizo zilikamatwa katika Tarafa za Kenkombo na Nansimo ambako ndiko uvuvi haramu ulikoota mizizi.

Aliongeza kwamba, wapo wavuvi haramu ambao wamekuwa wakitumia sumu na kwamba uvuvi huo unahatarisha afya za wananchi pamoja na kuua viumbe hai wa majini.

Aidha alitumia fursa hiyo kuwaomba viongozi wa wilaya jirani zilizoko kwenye ziwa Victoria, kudhibiti wavuvi haramu, kwani unapofanyika msako katika Wilaya ya Bunda, baadhi ya wavuvi hao hukimbilia katika wilaya hizo.

Mwisho.






Thursday 15 August 2013

LWAKATARE HOI

Polisi, Dk. Slaa jino kwa jino

Na Benjamin Masese, Dar es Salaam

WAKATI Jeshi la Polisi likiendelea kumng’ang’ania  Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare kwa tuhuma za kupanga njama za kudhuru watu, imedaiwa kuwa afya ya kiongozi huyo imezidi kudhoofika.

Tuesday 13 August 2013

TUJADILIANE LEO

Hivi kulingana na matukio haya yanayotokea ya ukatili kwa raia, wizi, utekaji na masuala kama hayo yanaashiria nini? tujadili, tafadhali unapochangia hapa toa hoja sio kushambulia mtu kwa itikadi na dini zako.

UKATILI HUU MPAKA LINI TANZANIA?


Mama akipigwa na mume wake baada ya kutofautina
Baba akimdhibiti mke wake kwa kumkata mapanga baada ya kuona ngumi, mateke na fimbo havikutosha
 
Na Benjamin Masese, Dar es Salaam

UKATILI wa kijinsia ni jambo kubwa kwenye ajenda za haki  za binadamu kimataifa.Ukatili unaweza kuwapata wanaume na wanawake lakini mara nyingi wanawake na watoto ndio waathirika wakubwa.

Hali hii imetokana  na mifumo mbalimbali iliyopo na uhusiano wa kijinsia ulivyo katika jamii zetu hapa nchini ambapo kundo moja hujiona ni bora kuliko kundi lingine.

Kwa miaka mingi wanaume wamechukuliwa kuwa katika daraja la juu kuliko mwanamke nah ii imejionyesha na kuendelea kuonekana wazi katika  nyanja zote za kijamii, kiutamaduni, kisiasa na kiuchumi.

Mazoea hayo yamejengwa tangu zamani huku kukiwa na ngazi za kifamilia hadi kitaifa jambo ambalo ni hatari katika jamii nyingi Barani Afrika na sehemu nyingine duniani.

Kutokana na hali hiyoilivyo mpaka sasa, kuna haja kubwa ya kutoa elimu juu ya ukatili katika jamii zetu hususani vijijini kunakotokea kila siku vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake.

Bila Serikali, taasisi, mashirika na wadau wengine wanapaswa kuungana pamoja na ili kuwaelimisha jamii juu ya kupambana na kuzuia ukatili wa kijinsia ili kuleta mabadiliko katika jamii.

Sote tunatambua kwamba ukatili ni kitendo chochote anachofanyiwa binadamu na kumsababishia maumivu au athari kimwili, kiakili au kisaikolojia.Kumekuwapo na vitendo vya ukatili vingi tena vya kukusudia, kulazimisha, kutisha au kugofya dhidi ya wanawake kutaka kufanya jambo au tendo la ngono bila hiari yao.

Binadamu yeyote anaweza kufanyiwa ukatili wa aina tano  ukitegemea  na utamaduni na historia  ya jamii husika. Mara nyingi ukatili huo hufanyika kati ya wanandoa wa wapenzi lakini wanawake mara nyingi wamekuwa wakisumbuliwa zaidi na ukatili wa kijinsia katika uhusianohuo.

Moja ya ukatili ni ule wa kimwili ambao mtu hufanyiwa kitendo ambacho kinaumiza mwili na madhara yake huonekana moja kwa moja  na wakati mwingine mtendewa ukatili anaweza kuhisi maumivu bila mtu mwingine kutambua kuwa amefanyiwa ukatili wa kimwili.

Baadhi ya mifano ya ukatili wa kimwili ni pamoja na vipigo, shambulio la kimwili, kuchomwa moto, matumizi ya silaha, kuvutwa nywele, kusukuma, kunyonga mkono au mguu, kupigwa kichwani na kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu yoyote ya mwili.

Pia  upo ukatili wa kisaikolojia ambao mtu anatendewa  na unamsababishia maumivu kiakili, kihisia huku mtenda kutotambua mwenzake anaathirika, mfano matusi kwa njia ya maneno au ishara yenye lengo la kudhalilisha, vitisho na kutishia kufanya fujo, maneno ya kufehedhesha, kudharau, kutishia kutoa siri, kuingiliwa faragha, kutishiwa kuuawa na mengine mengi.

Vile vile kuna ukatili wa uhusiano wa kingono ambao huambatana  na vitendo vinavyohusiana na masuala ya ngono, kwa mfano unyanyasaji wa kijinsia, kujamiiana kwa maharimu, ubakaji ndani ya ndoa, ulawiti, utekaji na usafirishaji  wa wanawake au wanaume na watoto kwa ajili ya ngono na vitendo vingine vya namna hiyo.

Upo ukatili wa kiuchumi ambao humnyima fursa za kiuchumi mwanamke au mwanaume katika kujiongezea kipato na kuchangia katika maendeleo.Aina  hiyo ya ukatili huwapata wanawake kutokana na hali yao ya kuwa tegemezi kwa wenzi wao.

Kitendo cha wanawake kuwa tegemezi kwa wanaume kimekua kinawaathiri sana kwani wanakosa kauli katika mali za familia na kutoshirikishwa kwenye maamuzi ya maendeleo.

Pia kuna ukatili unaotokana na tamaduni au mila potofu zetu hapa nchini ambazo zinakinzani na haki za binadamu jambo linalochangia kuwapo kwa vitendo vya ukatili. Baadhi ya ukatili wa mila potofu ni pamoja na ndoa za kushurutisha za utotoni, kutakasa wajane, kurithi wajane, utekeaji, matambiko ya kingono kwa watoto, miiko ya chakula na ukatili utokanao na mahari.

Kutokana na  uendelezaji wa vitendo vya ukatili nchini, kituo cha Msaada wa Sheria  kwa Wanawake Tanzania (WLAC)  kimeamua kuanzisha kampeni ya kupinga vitendo hivyo na kutoa msaada wa kisheria kwa wanawake  ili kuleta usawa  wa kijinsia Tanzania.

Taasisi ya WLAC  ni shirika lisilo la Serikali lililoanzishwa mwaka 1994 chini ya sheria ya makampuni sura ya 212 na pia limekuwa likiendeleza shughuli  za kitengo cha msaada wa sheria  SUWATA kilichoanzishwa mwaka 1989.

Kati ya madhumuni ya WLAC ni kutoa msaada wa sheria ju ya masuala yanayowakabili wanawake kama ndoa, mirathi, mikataba, biashara, ajira, uwakilishi mahakamani na huduma nyingine zinazofanana na hizo.

Pia imekuwa katika harakati za kujenga mtandao wa mashirika pamoja na taasisi zenye mwelekeo unaofanana na WLAC na kuratibu kwa pamoja shughuli za uhamasishaji umma kuhusu haki za wanawake na watoto.

Si jambo la kificho kwani wanawake wamekuwa katika changamoto kubwa hasa pale wanapokuwa katika ajira rasmi na hata zisizokuwa rasmi, baadhi yao wamekuwa  wakikosa nafasi za kufanya kazi mahali walipoomba kazi auhata katika ngazi ya familia kutokanana sababu mbalimbali.

Katika maeneo ya kazi, uzoefu unaonyesha wazi kuna kazi za wanawake na kazi za wanawake, wanawake waliobahatika kupata ajira wengi utawakuta nafsi za chini zaidi kama mapokezi, uhudumu wa ofisi, kazi za usafi na katibu mukhatsi.

Wakati mwingine baadhi ya wanawake wamelazimika kuingia katika uhusiano wa kimapenzi na wakuu wao wa kazi ili kupata mahitaji yao.Wanawake wa namna hiyo huishia kwenye migogoro na waume zao au wapenzi wan a hatimaye uhusiano huo huharibika kabisa na kufukuzwa kazi.

Kazi zinazohitaji mwanamke kusafiri sana, kufanya kazi muda mrefu, wakati wa usikuau zinazohusisha kukutana na watu mbalimbali mara nyingi zimesababisha migogoro katika ndoa.

Hata hivyo wanawake wengi wamekosa fursa ya kujishughulisha ili kuongeza pato la familia, ambapo kwa wale waliobahatika kupata ajira zisizo rasmi wengi wao wanaishi kwa masharti na kutokuwa huru na wanapata mapato yanatokanayo nakazi wanayofanya.

Suala la ukatili lina upana wake ambapo upo ukatili wa kijinsia unaotokana na lugha ambapo maneno mbalimbali yamekuwa yakitumika kumwelezea mwanamke ambayo uhalisia wake ni ukatili wa kijinsia.

Maneno hayo yamekuwa yakitolewa katika kuelezea maumbile na tabia ya baadhi ya wanawake, matumizi ya lugha hiyo kwa sehemu kubwa huchangia kuonyesha mfumo dume ambao ndio unaotawala maisha ya watu ya kila siku. Matumizi ya lugha yanadhihirisha dhana potofu kwamba kundi la wanaume lina nguvu na ni bora kuliko wanawake.

Asilimia kubwa na mazoea yaliyopo sasa ni kwamba neno mwanamke amekuwa akichukuliwa ni kama chombo cha kumstarehesha mwanaume, mfano kuna maneno ya kama changundoa, sahani ya babu, namba nane, twiga na mengine kam hayo ambayo huonesha kuwa mwanamke ni dhaifu kuliko mwanaume.

Maneno mengine yanayoendana na hayo wakati mwingine yanaweza kutolewa dhidi ya wanaume, kwa mfano bushoke, dume la mbegu lakini yote yameelekzwa kwa wanawake kumuonyesha mwanaume ni bora.

Hata hivyo upo ukatili katika vyombo vya habari na matangazo ya kibiashara, mfumo wa habari na utoaji wa habari zenyewe umekuwa ukionesha taswira ya mwanamke kama chombo cha kumburudisha mwanaume, mfano matangazo, picha na mziki hutumiwa  na kuonyesha  wanawake kama sehemu ya matangazo ya biashara.




Kutokana na hali hiyo hivi karibuni WLAC kupitia wanasheria wake waliandaa semina iliyohusisha  wanawake na wanaume  wanaojiita wanabadiliko kutoka mikoa ya Dar es Salaam na Pwani na kutoa elimu juu ya mambo kadhaa ya ukatili wa kijinsia nchini unaotokea katika nyanja mbalimbali ndani ya jamii.

Wanasheria wa WLAC waliokuwa wanatoa elimu kwa wanabadiliko ni pamoja na Lilian Lwanga na Hildegard Msina ambao walitoa ushahidi jinsi wanawake wanavyoteseka ndani ya ndoa zao pamoja na kunyang’anywa urithi wa mme wake mara anapofariki na kuacha familia.

Kwa upande Lwanga alibainisha kwamba katika utafiti walioufanya katika kadhaa nchini wamebaini asilimia 75 ya wananawake walio ndani ya ndoa hawana uhuru wa kijitawala katika maisha yao ya kila siku kutokana na kufanyiwa vitendo vya ukatili na wenzi wao.

Pia anasema walibaini wanaume wengi vijijini wamekuwa wakivunja ndoa zao au kuwatelekeza wake wao baada ya kujifungua watoto wenye vichwa vikubwa, midomo ya sungura na wengine wa namna ambapo aliitaka Serikali kuchukuliwa hatua za kisheria ili kukomesha hali ya ubaguzi, unyanyasaji na ukatili dhidi ya wanawake.


WLAC imeamua kuendesha kampeni maalum ijulikanayo kwa jina la TUNAWEZA kwa wanamabadiliko ili kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji nchini ambavyo vinaonekanakuwa jambo la kawaida katika  jinsia ya kike.

 Lwanga anasema msaada wa kisheria unaotolewa na WLAC umekuwa na mafanikio makubwa  kwani umeweza kuwasaidia wanawake kwa kuwawakilisha makahamani hadi  kurudishiwa nyumba walizokuwa wamenyang’anywa na ndugu wa marehemu kama urithi.

Anasema katika utafti wao mikoani wamebaini wanawake bado wananyanyaswa, wanapigwa na waume  lakini  hawako tayari kuwasema kwenye vyombo vya dola na kuongeza wameshuhudia ndoa nyingi zimevunjika kwa sababu ya mtoto kuzaliwa na kichwa kikubwa au mdomo wa wazi yaani wa sungura.

Lwanga anasema tatizo la watoto kukimbilia mjini na kuwa kuombaomba linatokana na ndoa kuvunjika, elimu ndogo kwa akina mama ya kutojua sheria zinazowapa haki yao, umasikini na mila potofu.

Anasema asilimia kubwa ya wananchi hasa wa vijini wanaishi kwa kuzingatia mila zao, hawajui  mabadiliko yaliyopo, wananyanyaswa kwa njia ya ngono, kiuchumi, kishambulio na kisaikolojia lakini hawajui namna ya kujisaidia kisheria kwani tangu awali Serikali haijaweka misingi ya kuwalinda wananwake na kuwapa uhuru.

Pamoja na mambo mengi ya unyanyasaji wa wanawake, Lwanga anaitaka Serikali kuacha mazoea ya kutegemea asasi, mashirika na ufadhili wa mataifa makubwa ya nje kuja nchini kutatua matatizo yanayowakabili wananchi wake badala yake inapaswa kupeleka elimu vijijini hususani katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.


Lwanga anasema kwamba ukatili unaofanywa dhidi ya wanawake nchini hauwezi kuvumiliwa ambapo anawataka  wanawake kuwafikisha wanaume kwenye vyombo vya dola aple wanapotendewa vitendo vya unyanyasaji.

Anasema binadamu yeyote anapofanyiwa ukatili  humsababishia kuwa na maumivu au athari kimwili, kiakili na kisaikolojia ambapo mwanamke anapofanyiwa ukatili huo athari kubwa kuliko mwanaume.

Anasema hivi sasa WLAC kwa kushirikiana na wakuu wa utekelezaji wa kampeni ya TUNAWEZA  wamedhamiria  kufikisha elimu ya ukatili wa kijinsia kwa watu 1,600,000 ifikapo mwaka 2013 ikiwa lengo ni kupunguza vitendo hivyo kwa wanawake ambavyo vimeonekana ndani ya jamii ni vitu vya kawaida.

Lwanga anasema madhumuni ya WLAC ni kutoa msaada wa sheria juu ya masuala yanayowakabili wanawake kama ndoa, mirathi, mikataba, kusimamia kesi mahakamani, kuendesha semina, ziara za mafunzo na kuhamasisha umma kuhusu haki za wanawake na watoto.

Pamoja na mambo mengi , wanasheria wa WLAC waliahidi kuendelea kutoa msaada wa kisheria mikaoni bure kwa wanawake na watoto ikiwa lengo ni kuleta usawa wa kijinsia Tanzania.

Hivyo sasa wakati umefika kwa Seriakli kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha vitendo vya unyanyasaji kijinsia vinakomeshwa haraka, pia vitendo vilivyoibuka hivi karibuni vya mateka kwa watu wanaopigania haki zao havipaswi kufumbiwa macho.

Tunapaswa kutambua kwamba katika hali halisi binadamu wote wamezaliwa huru huru na wote ni sawa mbele ya sheria hivyo hakuna mwenye haki ya kumfanyia mwenziwe ukatili wa aina  yoyote.

Vitendo hivi vinapofanyika ni kinyume cha sheria na mikataba mbalimbali ya haki za binadamu ambayo Tanzania imekuwa ikiisaini ili kushirikiana na mataifa makubwa kupambana na vitendo hivyo, sasa ni mwito kwa serikali kutekeleza mikataba hiyo kwa vitendo na sio maneno tupu. Maoni benjaminmasese@yahoo.com, 0655/0769-688300


MWISHOOO  





Wakina mama wa kabila la Wangoreme wakifurahi wakati wa sherehe


 
A Rwandan women's group celebrates the arrival of their cows from the charity Send a Cow. Sent in by BBC News website reader Kirstine Dunhill
 

Kabila la wangoreme na wakurya mkoani Mara wanavyokuwa wakisherekea shehehe za, harusi, kutahiriwa au kukeketwa. (chanzo. BBC Swahili)

DAR CITY 2013

Mwandishi wa Habari wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Dar es Salaam City Press Club (DCPC),Benjamin Masese (kulia) akiwa na mdogo wake , Boniphace Wanka (IFM)