Itikadi, ubaguzi wa RC Ndikilo Mwanza
unahitaji dawa haraka
*Makada wa Chadema waanza kusakwa
Serikalini
Na Benjamin
Masese, Mwanza
WAKATI
tunafikiria uhasama unaoendelea kati ya wafugaji na wakulima nchini kufikia
hatua ya kuuana kama wanyama ,inaonekana wazi kuna baadhi ya viongozi wa Serikali
wanafanya kazi kwa ubaguzi na itikadi za kisiasa.
Ni jambo la hatari
kwa mustakabili wa taifa hili ikiwa hali hii itachukuliwa kirahisi ama kupuuzwa,
kulindana kutokana na itikadi za vyama vya siasa au kwa maslahi binafsi.
Migogoro ya
wafugaji na wakulima imeanza kitambo na wananchi pamoja na wabunge hasa wa upinzani wamekuwa
wakisema jambo hilo bungeni lakini Serikali imekuwa ikilichukulia ni propaganda
zao za kujitafutia umaarufu.
Bila shaka
maauji ya watu zaidi ya kumi yaliyotokea Wilaya ya Kiteto yamethihirisha na
kuonyesha sura na uhalisia wa kile
kilichokuwa kikisemwa mara kwa mara
lakini kinachukuliwa poa.
Hakuna haja
ya kuelezea kile kilichosemwa na Naibu Spika wa Bunge, Job Ndungai mbele ya
Waziri Mkuu Pinda alipotembela wananchi wa Kiteto, kwa kuwa alisema wazi baadhi
ya viongozi wa Serikali wanashiriki kwa namna moja katika mauaji hayo kwa
manufaa yao binafsi.
Wakati
tunatafakari ya wafugaji na wakulima lakini inaonekana kuna mkakati wa ubaguzi
na chuki unaendeshwa chini chini na
viongozi katika sehemu za kazi kwa kuangalia
itikadi za vyama vya siasa, mkakati huu unaweza kuwa hatari kwa ustawi wa
taifa.
Ni hali ya
kustajabisha kuona Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Evarist Ndikilo akifanya kazi kwa
ubaguzi na chuki kutokana na itikadi za vyama vya siasa.
Ubaguzi na chuki wa mkuu huyo ulidhihirika January 17
mwaka huu wakati wa hafla iliyoandaliwa
na Mamlaka ya Maji Safi na Taka Mwanza (MWAUWASA) ya kupokea hundi ya mkopo Sh
milioni 300 kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (LAPF).
Fedha hizo
zilitolewa na LAPF kwa ajili kukikopesha Chama cha Akiba na Mikopo cha Mamlaka
ya Maji Safi na Taka Mwanza (MWAUWASA-SACCOS) ambacho imekuwa mkombozi wa
watumishi wa mamlaka hiyo.
Katika hali
ambayo haikutarajiwa wageni wa LAPF waliokuwa
wametoka Dodoma na watumishi wa Mwauwasa wakiwa tayari kumpokea mgeni rasmi
ambaye ni Ndikilo, ilikuja taarifa kwa wote kwamba amepata dharura hivyo
hatafika.
Kitendo
hicho kiliwashangaza watu wengi na
kuhoji angemtuma hata mwakilishi wake kwa kuwa wageni walikuwa nje ya ukumbi wa
Gand Hall kwa ajili ya mapokezi.
Macho ya
wageni na waalikwa yalielekezwa kwenye ofisi ya Ndikilo ilipo kwa kuwa ni
karibu kutoka eneo la hafla ilipokuwa ikifanyikia sawa na mita 95 huku kila mmoja akitafsiri ajuavyo juu ya
kitendo hicho.
“Lakini wakati watu wakiondoka eneo
hilo ilidokezwa taarifa nyingine kwamba Ndikilo hakuweza kufika kwa sababu Meneja wa Saccos hiyo, Tungaraza Njugu ni kada na kiongozi mkubwa wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) hivyo hawawezi kukaa meza moja”.
Ilifafanuliwa
kwamba Meneja Njugu ambaye ni Kiongozi
wa Operesheni Kanda ya Ziwa Magharibi wa Chadema amekuwa akimtukana Ndikilo
katika majukwaa na mikutano ya kisiasa
juu ya utendaji wake, hivyo upande mmoja kuwa na chuki.
MTANZANIA
ilifunga safari kwenda ofisi ya Saccos ya Mwauwasa ili kujua kwa kina hali hiyo
ambayo viongozi ambao ni waajiriwa wa Serikali kufikia hatua ya kufanya kazi
kwa chuki kutokana na itikadi za kisiasa.
Njugu
anaanza kwa kusema anasikitishwa na kitendo kilichotokea na kuongeza kwamba
imedhihirisha Ndikilo anaongoza Mkoa wa Mwanza kwa itikadi ya kichama na
ubaguzi wa kisiasa.
Anasema
haamini kama Ndikilo ametumwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) au ndio sera ya
chama hicho katika kuongoza kwa ubaguzi wa watumishi kwa mlengo wa
itikadi za kisiasa.
Njugu
anasema taarifa ya Ndikilo kushindwa kufika eneo tukio kutokana na yeye kuwa
kada wa Chadema ilielezwa na Zacharia Membo ambaye ni Afisa Utumishi Mwauwasa.
Anasema hali
hiyo imempa wasiwasi juu ya usalama wake, ajira na mambo mengineya kifamiia kwa kuwa Ndikilo ana nafasi ya kumtendea kitu
chochote kwani ni mkuu wa mkoa na Mwenyekiti wa kamati ulinzi na usalama.
Njugu
anasema imedhihirisha wazi watumishi wa Serikali ambao ni makada wa Chadema
wapo katika hali ya kubaguliwa na inaonyesha hawana haki ya kazi au kuajiriwa
serikalini.
Anasema alipata
nafasi ya meneja wa Saccos hiyo kutokana
na elimu na utalaamu wake, hivyo kuwa kada wa Chadema si dhambi na kuongeza
kwamba kamwe hafanyi kazi kwa itikadi za
kisiasa.
Njugu
anasema kuna kila sababu ya Rais Jakaya Kikwete kufanya mabadiliko ya nafasi
hiyo ya ukuu wa mkoa kwani imedhihirisha chanzo cha madiwani watatu wa Chadema
kufukuzwa ni nguvu yake inachangia.
“Sasa hivi Ndikilo namweka kama adui wangu
namba moja katika maisha yangu, familia na ajira hivyo vyombo vya usalama
nataka vijue hivyo nikipata tatizo lolote chanzo ni chuki za kisiasa za upande
mmoja”.
Lakini
anasema kutokana na ubaguzi huo na chuki wa Ndikilo haziwezi kuwa kikwazo
katika kutekeleza majukumu yake ya kazi na kisiasa anakupokuwa nje ya Saccos.
Njugu
anasema kwa nafasi yake hiyo hajawahi kufanya upendeleo wowote dhidi ya
watumishi wa Mwauwasa na wengi wao wamejenga nyumba na kununua gari kupitia
Saccos yao.
Inaonekana
Ndikilo alikuwa na chuki dhidi ya mamlaka hiyo kwani aliwahi kulalamika mbele
ya Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) juu ya tabia ya Mkurugenzi wa Mwauwasa, Anthony
Sanga kushindwa kutoa taarifa kwake wakati Naibu Waziri wa Maji, Benilith
Mahenge alipokuja Mwanza January 3 mwaka huu.
Ni kweli
kabisa wakati Mahenge alipokuja kukabidhi vitendea kazi kwa halmashauri nne za
Geita, Ukerewe, Sengerema na Nansio hakuwapo Mkuu wa mkoa wala askari yeyote
kwa ajili ya ulinzi, hindicho ndicho kilimchomkasirisha na kuamua kumsema Sanga mbele ya RCC.
Yamekuwapo
na malalamiko dhidi ya Sanga kwamba ni miongoni mwa viongozi wababe, kiburi
sawia na Ndikilo lakini wanaoumia kutokana na uhasama huo ni wananchi
wanaohitaji huduma za kijamii.
Mhandisi
Sanga amekuwa akilalamikiwa na wananchi pamoja na waandishi wa habari Mkoa wa
Mwanza juu ya kauli zake na hata kuwatishia maisha pale wanapokuwa wakimbana
kutaka taarifa ya Mwauwasa kutokana na malalamiko ya wananchi.
Hata
wanapojaribu kuandika maswali na kuyakabidhi kwake amekuwa akiyapuuza lakini
wanapojaribu kuandika hali halisi ndipo ugomvi unapotokea na kutoa vitisho.
Mmoja wa
watumishi wa Mwauwasa ambaye hakutaka jina lake litajwe anasema ni dhahiri sasa
kuna mkakati wa kumwondoa Njugu katika nafasi ya umeneja kwa kuwa elimu yake
haikidhi viwango vya kusimamia saccos hiyo kwani imefikia kumiliki mabilioni ya
fedha.
Ni wazi sasa
kumeibuka kasumba ya kutoelewana kati ya
viongozi ngazi ya halmashauri, wilaya, mkoa na taasisi zake kutokana na itikadi
za kisiasa na kusababisha kukwama kwa shughuli za maendeleo katika maeneo
husika.
Itakumbukwa
mwishoni mwa mwaka jana mpaka sasa kumekuwapo na migogoro kadha wa kadha maeneo
mbalimbali nchini kwa viongozi wa
kulalamikiana huku kila mmoja akimtuhumu mwenzake kuingilia majukumu ya
mwenzake.
Pia
kumekuwapo na hali ya kutofautiana kauli juu ya jambo moja ambapo upande mmoja umekuwa ukidai kutenda
haki huku mwingine ukilalamika.
Tumeshuhudia
mkoani Arusha, mkuu wa mkoa huo akitofautiana kauli na Mkurugenzi wa jiji hilo
juu ya wafanya biashara wadogo katikati ya jiji hilo na kusababisha madiwani
kugawanyika katika pande mbili.
Ukiachia
hilo kumekuwapo na mgogoro kati ya Meya wa Ilemela na Mkuu wa wilaya mkoani Mwanza kwa kila
mmoja kudai kuingilia majukumu ya mwingine.
Wimbi hilo
linaonekana kuwagusa sana wakurugenzi wa Halmashauri kutofautiana na madiwani
na watendaji wengi, kwa mfano Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Hassan Hidda
amekuwa katika mgogoro na madiwani jambo ambalo linakwamisha maendeleo.
Hiyo ni
mifano michache ambayo inaonesha kuna wimbi la viongozi walioaminiwa na kupewa
dhamana ya kuwatumikia wananchi kushindwa kushirikiana na kuanza kutuhumiana.
Kwa tukio la
RC Ndikilo la kutohudhuria katika hafla hiyo zikiwa zimesalia dakika kama kumi
lilionesha sura mbaya kwa wageni waliotoka Dodoma kwa ajili kutoa mkopo kwa
Mwauwasa, mpaka sasa haijulikani wageni hao walipewa majibu gani.
Ni vema sasa
Rais Kikwete akawatazama watu wake kwa namna nyingine katika nafasi walizopewa
kuziongoza kwa kuwa wanaelekea kuleta mgawanyiko ndani ya jamii moja na taifa
moja vingine itafikia hatua ya wafugaji na wakulima.
0683608958
MWISHO.
hodi ni wewe katika haraka haja mkopo kulipia kuanza yako madeni ya kuanzisha biashara au nyumba ??? Kisha inakuja teksi kampuni una imani na relay juu ya 100% uhakika sababu hii ni kampuni ambapo i cashed mkopo wangu kwa mama yangu Stella dawa leo ili kuwasiliana na René Mikopo Firm halisi kupimwa na kuaminiwa na leo mimi nina furaha i got mkopo wangu wa $ 120,000 leo ili kupata kushikamana leo mrsstellareneloanfirm@hotmail.com} {barua pepe hapa chini na kupata jibu la matatizo yako yote kwa sababu Siwezi Kunyamaza ushuhuda huu mkubwa peke yangu binafsi ili i aliamua kuandika kwenye tovuti kwa sababu kula furaha kubwa kwa yangu moyo na leo mimi nina kuishi maisha mapya shukrani kwa wote Stella René
ReplyDeletekolochatechee
Ni wewe kuangalia kuanza mkopo biashara au kulipa
ReplyDeleteHesabu za
Hiyo ni kwa nini tuko hapa kuwasaidia wenye
Unahitaji mkopo
kwa kiwango cha 3%
wasiliana nasi leo kupitia barua pepe:
joerichardloanfirm@gmail.com
Biblia inasema: "" Luke 11:10 Kila mtu ambaye anauliza
kupokea; atafutaye hupata; na kwamba
makofi mlango wazi "kwa kamwe kuondoka
wao miss nafasi kwa sababu Yesu ni
yule jana, leo na hata milele
zaidi.Tafadhali hizi ni nia mbaya na Mungu
wakihofia watu. Wewe ni ushauri wa kujaza na kurudi
.. Maelezo hapa chini name: __________
____________ Anuani yako: ____________________
Nchi yako: ____________________ wake
Kazi: Mikopo Kiasi __________________
Inahitajika: ______________ Mikopo Muda: ______
______________ Mapato ya kila mwezi: __________________
Kiini simu: ________________ Je,
kutumika kwa ajili ya mkopo kabla ya: ________________
haraka ndani na nje ya fedha dhiki, machafuko na
ugumu kuwasiliana RichardLoan Corporation
Leo email: joerichardloanfirm@gmail.com.you
Utapata mkopo wako bila kuchelewa kuwa Apply.and
heri
I am a veteran with the world trade organization humanitarian delivery agency, an ancillary of the UN..
ReplyDeleteMrs. Bernice Clark 69 died of covid-19 related virus. Before her death she left manifold amounts with a security & finance firm in Europe for preservation. she disclosed that the trust-funds should not be left unclaimed. You are to stand as the stipendiary to late Bernice Clark.
Get back to us with your interestedness at (wldtrdeorgnztionhumangcy@gmail.com). and contact data for all other formalities which are certifiable.
Hoping to have an opulence pact with you on communal trust.