Marekani yaleta ukombozi sekta elimu
ya kisasa Tanzania
*Sasa walimu wa sayansi kutoshika
chaki
Na Benjamin
Masese, Mwanza
MFUMO wa
kisasa wa ufundishaji wa masomo ya sayansi bila mwalimu kushika chaki
umezinduliwa nchini katika mikoa 10 kwa
majaribio ya wanafunzi wa kidato cha pili.
Uzinduzi huo
ulifanyika juzi jijini Mwanza katika Shule ya Sekodari ya wavulana ya Bwiru chini ya ufadhili wa taasisi kutoka Marekani iitwayo Opportunity Education Foundation inayojihusisha
na masuala ya elimu.
Akizungumza
baada ya kukabidhi vifaa kwa walimu sita wa masomo ya sayansi na wanafunzi 162 wa kidato cha pili , Meneja Programu wa
taasisi hiyo, Sadra Tetty alisema Marekani imemua kufanya majaribio Tanzania
katika mikoa 10.
Tetty
alisema vifaa vyenye mfumo huo vina mitaala yote inayofundishwa Tanzania na
inaweza kubadilishwa kadri wizara ya elimu itakavyoona inafaa au kuongeza
program nyingine.
Alisema kwa
awamu ya kwanza wameanza katika majaribio ya mikoa kumi kwa baadhi ya shule za sekondari kwa wanafunzi wa
kidato cha pili na ikiwa watafanikiwa katika mitihani yao wataendelea kufadhili
mikoa mingine.
“Tumeamua
kuwagawaia vifaa kila mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule tulizozichagua
pamoja na walimu wote wa masomo ya sayansi ikiwa lengo ni kurahisha ufundishaji
na kuboresha elimu pamoja na kukuza teknolojia.
“Shule
tulizoanza kufanya majaribio juu ya mfumo huu zipo Dar es Salaam, Mwanza,
Bukoba, Dodoma, Morogoro, Pemba, Rifiji, Arusha na Zanzibar.
“Ufadhili
huu kwa Tanzania zimetengwa Dola milioni 10 za Marekani kwa majaribio na
tutakuwa tunapita kukagua lakini matokeo yao ndio yatatoa mwelekeo sahihi kama
unaeleweka au la,”alisema.
Tetty
alisema mfumo huo umekuwa na mafanikio Marekani na hakuna mwalimu wa masomo ya
sayansi anayeandika ubaoni na chaki, na kuongeza kuwa unaondoa utegemezi kati
ya mwanafunzi na mwalimu katika kujifunza.
Alisema
vifaa hivyo huchajiwa na umeme nyakati za usiku na kutumiwa mchana wakati wa
masomo na kuwataka walimu wa masomo hayo kuvitumia kama vilivyokusudiwa
sambamba na vile vya wanafunzi.
Tetty alisema kuwa katika shule wanazofanyia
majaribio tayari walimu wa masomo hayo wamekwisha pewa mafunzo.
Kwa upande wa Mkuu wa Shule ya Bwiru, Elias Kaboja alisema amefurahishwa shule yake kuwa katika majaribio ya mfumo huo na kuongeza kwmaba utarahisisha ufundishaji.
Kwa upande wa Mkuu wa Shule ya Bwiru, Elias Kaboja alisema amefurahishwa shule yake kuwa katika majaribio ya mfumo huo na kuongeza kwmaba utarahisisha ufundishaji.
Alisema
atahakikisha anawasimamia walimu wa masomo hayo kufanikisha kile kilicholengwa
huku akiitaka Serikali kushirikiana na taasisi hiyo ili mfumo uenee nchi nzima.
Alisema
anafurahishwa kuona kila mwalimu sita amepewa vifaa hivyo na wanafunzi 162 wa
kidato cha pili wamepewa kila mmoja.
Alisema
shule yake ina wanafunzi 780 na kati ya hao 162 ni kidato cha pili waliiopewa
vifaa vya mfumo huo ambao utaanza kutumika Februari 3, mwaka huu.
Naye Mratibu
wa Programu ya mfumo huo shuleni hapo, Iluminata Pascal ambaye pia ni mwalimu
alisema uwepo wa vifaa hivyo utapunguza kazi ya uandaaji program ya kufundisha.
Hata hivyo
moja ya changamoto iliyopo katika mfumo huo ni pale ambapo itatokea mabadiliko
ya mitaala ya elimu kwani inalazimika kuingizwa katika vifaa hivyo.
Baadhi ya
wanafunzi wa kidato cha pili wa shule hiyo waliozungumza na MTANZANIA baada ya
kukabidhiwa vifaa hivyo walifurahishwa na ujio wa mfumo huo.
Miongoni mwa
wanafunzi waliozungumza ni pamoja na Igunge Zakayo, Johnson Kaihuzi na Shaban
Moshi ambao walisema wana shauku ya kutaka kuanza kuvitumia vifaa hivyo.
No comments:
Post a Comment