![]() |
Mama akipigwa na mume wake baada ya kutofautina |
![]() |
Baba akimdhibiti mke wake kwa kumkata mapanga baada ya kuona ngumi, mateke na fimbo havikutosha |
Na Benjamin Masese, Dar es Salaam
UKATILI wa kijinsia ni jambo
kubwa kwenye ajenda za haki za binadamu
kimataifa.Ukatili unaweza kuwapata wanaume na wanawake lakini mara nyingi
wanawake na watoto ndio waathirika wakubwa.
Hali hii imetokana na mifumo mbalimbali iliyopo na uhusiano wa
kijinsia ulivyo katika jamii zetu hapa nchini ambapo kundo moja hujiona ni bora
kuliko kundi lingine.
Kwa miaka mingi wanaume
wamechukuliwa kuwa katika daraja la juu kuliko mwanamke nah ii imejionyesha na
kuendelea kuonekana wazi katika nyanja
zote za kijamii, kiutamaduni, kisiasa na kiuchumi.
Mazoea hayo yamejengwa tangu
zamani huku kukiwa na ngazi za kifamilia hadi kitaifa jambo ambalo ni hatari
katika jamii nyingi Barani Afrika na sehemu nyingine duniani.
Kutokana na hali hiyoilivyo
mpaka sasa, kuna haja kubwa ya kutoa elimu juu ya ukatili katika jamii zetu
hususani vijijini kunakotokea kila siku vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake.
Bila Serikali, taasisi,
mashirika na wadau wengine wanapaswa kuungana pamoja na ili kuwaelimisha jamii
juu ya kupambana na kuzuia ukatili wa kijinsia ili kuleta mabadiliko katika
jamii.
Sote tunatambua kwamba
ukatili ni kitendo chochote anachofanyiwa binadamu na kumsababishia maumivu au
athari kimwili, kiakili au kisaikolojia.Kumekuwapo na vitendo vya ukatili vingi
tena vya kukusudia, kulazimisha, kutisha au kugofya dhidi ya wanawake kutaka
kufanya jambo au tendo la ngono bila hiari yao.
Binadamu yeyote anaweza
kufanyiwa ukatili wa aina tano
ukitegemea na utamaduni na
historia ya jamii husika. Mara nyingi
ukatili huo hufanyika kati ya wanandoa wa wapenzi lakini wanawake mara nyingi
wamekuwa wakisumbuliwa zaidi na ukatili wa kijinsia katika uhusianohuo.
Moja ya ukatili ni ule wa
kimwili ambao mtu hufanyiwa kitendo ambacho kinaumiza mwili na madhara yake
huonekana moja kwa moja na wakati
mwingine mtendewa ukatili anaweza kuhisi maumivu bila mtu mwingine kutambua
kuwa amefanyiwa ukatili wa kimwili.
Baadhi ya mifano ya ukatili
wa kimwili ni pamoja na vipigo, shambulio la kimwili, kuchomwa moto, matumizi
ya silaha, kuvutwa nywele, kusukuma, kunyonga mkono au mguu, kupigwa kichwani
na kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu yoyote ya mwili.
Pia upo ukatili wa kisaikolojia ambao mtu
anatendewa na unamsababishia maumivu
kiakili, kihisia huku mtenda kutotambua mwenzake anaathirika, mfano matusi kwa
njia ya maneno au ishara yenye lengo la kudhalilisha, vitisho na kutishia
kufanya fujo, maneno ya kufehedhesha, kudharau, kutishia kutoa siri, kuingiliwa
faragha, kutishiwa kuuawa na mengine mengi.
Vile vile kuna ukatili wa
uhusiano wa kingono ambao huambatana na
vitendo vinavyohusiana na masuala ya ngono, kwa mfano unyanyasaji wa kijinsia,
kujamiiana kwa maharimu, ubakaji ndani ya ndoa, ulawiti, utekaji na
usafirishaji wa wanawake au wanaume na
watoto kwa ajili ya ngono na vitendo vingine vya namna hiyo.
Upo ukatili wa kiuchumi ambao
humnyima fursa za kiuchumi mwanamke au mwanaume katika kujiongezea kipato na
kuchangia katika maendeleo.Aina hiyo ya
ukatili huwapata wanawake kutokana na hali yao ya kuwa tegemezi kwa wenzi wao.
Kitendo cha wanawake kuwa
tegemezi kwa wanaume kimekua kinawaathiri sana
kwani wanakosa kauli katika mali
za familia na kutoshirikishwa kwenye maamuzi ya maendeleo.
Pia kuna ukatili unaotokana
na tamaduni au mila potofu zetu hapa nchini ambazo zinakinzani na haki za
binadamu jambo linalochangia kuwapo kwa vitendo vya ukatili. Baadhi ya ukatili
wa mila potofu ni pamoja na ndoa za kushurutisha za utotoni, kutakasa wajane,
kurithi wajane, utekeaji, matambiko ya kingono kwa watoto, miiko ya chakula na
ukatili utokanao na mahari.
Kutokana na uendelezaji wa vitendo vya ukatili nchini,
kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake
Tanzania (WLAC) kimeamua kuanzisha
kampeni ya kupinga vitendo hivyo na kutoa msaada wa kisheria kwa wanawake ili kuleta usawa wa kijinsia Tanzania.
Taasisi ya WLAC ni shirika lisilo la Serikali lililoanzishwa
mwaka 1994 chini ya sheria ya makampuni sura ya 212 na pia limekuwa
likiendeleza shughuli za kitengo cha
msaada wa sheria SUWATA kilichoanzishwa
mwaka 1989.
Kati ya madhumuni ya WLAC ni
kutoa msaada wa sheria ju ya masuala yanayowakabili wanawake kama
ndoa, mirathi, mikataba, biashara, ajira, uwakilishi mahakamani na huduma
nyingine zinazofanana na hizo.
Pia imekuwa katika harakati
za kujenga mtandao wa mashirika pamoja na taasisi zenye mwelekeo unaofanana na
WLAC na kuratibu kwa pamoja shughuli za uhamasishaji umma kuhusu haki za
wanawake na watoto.
Si jambo la kificho kwani
wanawake wamekuwa katika changamoto kubwa hasa pale wanapokuwa katika ajira
rasmi na hata zisizokuwa rasmi, baadhi yao
wamekuwa wakikosa nafasi za kufanya kazi
mahali walipoomba kazi auhata katika ngazi ya familia kutokanana sababu
mbalimbali.
Katika maeneo ya kazi, uzoefu
unaonyesha wazi kuna kazi za wanawake na kazi za wanawake, wanawake
waliobahatika kupata ajira wengi utawakuta nafsi za chini zaidi kama mapokezi, uhudumu wa ofisi, kazi za usafi na katibu
mukhatsi.
Wakati mwingine baadhi ya
wanawake wamelazimika kuingia katika uhusiano wa kimapenzi na wakuu wao wa kazi
ili kupata mahitaji yao.Wanawake wa namna hiyo huishia kwenye migogoro na waume
zao au wapenzi wan a hatimaye uhusiano huo huharibika kabisa na kufukuzwa kazi.
Kazi zinazohitaji mwanamke
kusafiri sana,
kufanya kazi muda mrefu, wakati wa usikuau zinazohusisha kukutana na watu
mbalimbali mara nyingi zimesababisha migogoro katika ndoa.
Hata hivyo wanawake wengi
wamekosa fursa ya kujishughulisha ili kuongeza pato la familia, ambapo kwa wale
waliobahatika kupata ajira zisizo rasmi wengi wao wanaishi kwa masharti na
kutokuwa huru na wanapata mapato yanatokanayo nakazi wanayofanya.
Suala la ukatili lina upana
wake ambapo upo ukatili wa kijinsia unaotokana na lugha ambapo maneno
mbalimbali yamekuwa yakitumika kumwelezea mwanamke ambayo uhalisia wake ni
ukatili wa kijinsia.
Maneno hayo yamekuwa
yakitolewa katika kuelezea maumbile na tabia ya baadhi ya wanawake, matumizi ya
lugha hiyo kwa sehemu kubwa huchangia kuonyesha mfumo dume ambao ndio
unaotawala maisha ya watu ya kila siku. Matumizi ya lugha yanadhihirisha dhana
potofu kwamba kundi la wanaume lina nguvu na ni bora kuliko wanawake.
Asilimia kubwa na mazoea
yaliyopo sasa ni kwamba neno mwanamke amekuwa akichukuliwa ni kama chombo cha
kumstarehesha mwanaume, mfano kuna maneno ya kama
changundoa, sahani ya babu, namba nane, twiga na mengine kam hayo ambayo
huonesha kuwa mwanamke ni dhaifu kuliko mwanaume.
Maneno mengine yanayoendana
na hayo wakati mwingine yanaweza kutolewa dhidi ya wanaume, kwa mfano bushoke,
dume la mbegu lakini yote yameelekzwa kwa wanawake kumuonyesha mwanaume ni
bora.
Hata hivyo upo ukatili katika
vyombo vya habari na matangazo ya kibiashara, mfumo wa habari na utoaji wa
habari zenyewe umekuwa ukionesha taswira ya mwanamke kama chombo cha
kumburudisha mwanaume, mfano matangazo, picha na mziki hutumiwa na kuonyesha
wanawake kama sehemu ya matangazo ya biashara.
Kutokana na hali hiyo hivi
karibuni WLAC kupitia wanasheria wake waliandaa semina iliyohusisha wanawake na wanaume wanaojiita wanabadiliko kutoka mikoa ya Dar
es Salaam na Pwani na kutoa elimu juu ya mambo kadhaa ya ukatili wa kijinsia
nchini unaotokea katika nyanja mbalimbali ndani ya jamii.
Wanasheria wa WLAC waliokuwa
wanatoa elimu kwa wanabadiliko ni pamoja na Lilian Lwanga na Hildegard Msina
ambao walitoa ushahidi jinsi wanawake wanavyoteseka ndani ya ndoa zao pamoja na
kunyang’anywa urithi wa mme wake mara anapofariki na kuacha familia.
Kwa upande Lwanga alibainisha
kwamba katika utafiti walioufanya katika kadhaa nchini wamebaini asilimia 75 ya wananawake walio ndani ya ndoa hawana
uhuru wa kijitawala katika maisha yao
ya kila siku kutokana na kufanyiwa vitendo vya ukatili na wenzi wao.
Pia anasema walibaini wanaume
wengi vijijini wamekuwa wakivunja ndoa zao au kuwatelekeza wake wao baada ya
kujifungua watoto wenye vichwa vikubwa, midomo ya sungura na wengine wa namna ambapo
aliitaka Serikali kuchukuliwa hatua za kisheria ili kukomesha hali ya ubaguzi,
unyanyasaji na ukatili dhidi ya wanawake.
WLAC imeamua kuendesha
kampeni maalum ijulikanayo kwa jina la TUNAWEZA
kwa wanamabadiliko ili kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji nchini
ambavyo vinaonekanakuwa jambo la kawaida katika jinsia ya kike.
Lwanga anasema msaada wa kisheria unaotolewa
na WLAC umekuwa na mafanikio makubwa
kwani umeweza kuwasaidia wanawake kwa kuwawakilisha makahamani hadi kurudishiwa nyumba walizokuwa wamenyang’anywa
na ndugu wa marehemu kama urithi.
Anasema katika utafti wao
mikoani wamebaini wanawake bado wananyanyaswa, wanapigwa na waume lakini hawako tayari kuwasema kwenye vyombo vya dola
na kuongeza wameshuhudia ndoa nyingi zimevunjika kwa sababu ya mtoto kuzaliwa
na kichwa kikubwa au mdomo wa wazi yaani wa sungura.
Lwanga anasema tatizo la
watoto kukimbilia mjini na kuwa kuombaomba linatokana na ndoa kuvunjika, elimu ndogo
kwa akina mama ya kutojua sheria zinazowapa haki yao, umasikini na mila potofu.
Anasema asilimia kubwa ya
wananchi hasa wa vijini wanaishi kwa kuzingatia mila zao, hawajui mabadiliko yaliyopo, wananyanyaswa kwa njia
ya ngono, kiuchumi, kishambulio na kisaikolojia lakini hawajui namna ya
kujisaidia kisheria kwani tangu awali Serikali haijaweka misingi ya kuwalinda
wananwake na kuwapa uhuru.
Pamoja na mambo mengi ya
unyanyasaji wa wanawake, Lwanga anaitaka Serikali kuacha mazoea ya kutegemea
asasi, mashirika na ufadhili wa mataifa makubwa ya nje kuja nchini kutatua
matatizo yanayowakabili wananchi wake badala yake inapaswa kupeleka elimu
vijijini hususani katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Lwanga anasema kwamba ukatili
unaofanywa dhidi ya wanawake nchini hauwezi kuvumiliwa ambapo anawataka wanawake kuwafikisha wanaume kwenye vyombo
vya dola aple wanapotendewa vitendo vya unyanyasaji.
Anasema binadamu yeyote
anapofanyiwa ukatili humsababishia kuwa
na maumivu au athari kimwili, kiakili na kisaikolojia ambapo mwanamke anapofanyiwa
ukatili huo athari kubwa kuliko mwanaume.
Anasema hivi sasa WLAC kwa
kushirikiana na wakuu wa utekelezaji wa kampeni ya TUNAWEZA wamedhamiria
kufikisha elimu ya ukatili wa kijinsia kwa watu 1,600,000 ifikapo mwaka
2013 ikiwa lengo ni kupunguza vitendo hivyo kwa wanawake ambavyo vimeonekana
ndani ya jamii ni vitu vya kawaida.
Lwanga anasema madhumuni ya
WLAC ni kutoa msaada wa sheria juu ya masuala yanayowakabili wanawake kama ndoa, mirathi, mikataba, kusimamia kesi mahakamani,
kuendesha semina, ziara za mafunzo na kuhamasisha umma kuhusu haki za wanawake
na watoto.
Pamoja na mambo mengi , wanasheria
wa WLAC waliahidi kuendelea kutoa msaada wa kisheria mikaoni bure kwa wanawake
na watoto ikiwa lengo ni kuleta usawa wa kijinsia Tanzania.
Hivyo sasa wakati umefika kwa
Seriakli kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha vitendo vya unyanyasaji
kijinsia vinakomeshwa haraka, pia vitendo vilivyoibuka hivi karibuni vya mateka
kwa watu wanaopigania haki zao havipaswi kufumbiwa macho.
Tunapaswa kutambua kwamba
katika hali halisi binadamu wote wamezaliwa huru huru na wote ni sawa mbele ya
sheria hivyo hakuna mwenye haki ya kumfanyia mwenziwe ukatili wa aina yoyote.
Vitendo hivi vinapofanyika ni
kinyume cha sheria na mikataba mbalimbali ya haki za binadamu ambayo Tanzania
imekuwa ikiisaini ili kushirikiana na mataifa makubwa kupambana na vitendo
hivyo, sasa ni mwito kwa serikali kutekeleza mikataba hiyo kwa vitendo na sio
maneno tupu. Maoni benjaminmasese@yahoo.com,
0655/0769-688300
MWISHOOO
Haya kaka naona mambo yako
ReplyDeleteHaya kaka naona mambo yako
ReplyDeleteHaya kaka naona mambo yako, NASHUKURU SANA KWA KUNIONA NA KUSOMA BLOG YANGU
Delete