HISTORIA YA WANGOREME
Na Benjamin Masese, Dar es Salaam
MKOA wa Mara ni miongoni mikoa ya Tanzania Bara ambapo mji wa Musoma ndipo makaoa makuu ya mkoa huo.
Mara imepakana na mikoa ya Mwanza na Shinyanga upande wa Kusini, Arusha upande wa Kusini-Mashariki, Kagera upande wa Magharibi mwa Ziwa Nyanza au Viktoria na Kenya upande wa mashariki.
Idadi ya wakazi ni zaidi ya milioni mbili na makabila ni mengi kuliko mikoa yote ya Tanzania ispokuwa Jiji la Dar es Salaam.
Baadhi ya makabila
yaliyopo Mkoa wa Mara ni wajaruo, wajita, waruri, wazanaki, wakabwa, wakiroba,
wasimbati, wangoreme, wakwaya, waikoma, wanata, waisenye, waikizu, wasizaki,
wasukuma, wataturu ne mengine wengi.
Kuna wilaya
ya saba ambazo ni Bunda, Serengeti, Tarime, Rorya, Butiama, Musoma Mjini na
Musoma Vijijini.
Katika
makala ya leo nitazungumzia kabila wa Wangoreme
wanaoishi Wilaya ya Serengeti. Wangoreme wametokea Carogos nchini Ghana miaka
mingi iliyopita.
Kabila la
Wangoreme na Waikoma mzazi wao ni mmoja
aliyejulikana kwa jina la Sabayaya Wandira ambaye ni miongoni mwa msafara wa
mtandao uliokuwa ukitoka Misri kupitia Somalia hadi Kenye ambapo waliingilia
Mto Mara na kuweka makazi yao Serengeti.
Msafara
mwingine wa kabila wa Wangoreme iliingia Serengeti kupitia njia ya Mkoa wa
Manyara na baadhi yao kuweka makazi yao hapo.
Vijiji vya
kabila la Wangoreme vilivyoitengeneza Wilaya ya Serengeti ni Mugumu,Ikorongo, Borenga, Nyiboko,
Buchanchari, Nyansurumunti, Mto Mara (Ghitende), Wigero, Baranga, Sirori Simba,
Remng’orori , Mikomariro.
Vingine ni
Mto Msamo-Tirina, Manchemwero, Nyankomogo, Issenye, Rigicha, Wegete, Nata,
Rubana na kuunganisha tena Mugumu ambapo ndipo makao Makuu ya Wilaya ya
Serengeti.
Lakini
Vijiji hivyo vimevamiwa na kabila la
Wakurya wenye asili koo ya waasi kwa upande Magharibi, upande wa Kusini
pamevamiwa na Waikizu na Waisenye na upande wa Magharibi wamevamia wakurya
halisi kutoka Kenye na Tarime.
Pamoja na
uvamizi huo lakini kabila la Wangoreme wameungana na kabila la Waikizu, Wanata
na Waisenye na kuwa kitu kimoja tofauti na Wakurya wenye tabia tofauti ya
ukatili na wizi wa mifugo.
Miiko ya Wangoreme
Mtu aliyeua mwenzake- Kabila la Wangoreme wamekuwa na miiko
yao kulingana na tukio lenyewe, kwa mfano mtu aliyeua mwenzake ukiachia masuala
ya kisheria, mara nyingi ukoo wa pande zote mbili hukaa na kukubaliana fidia
ambayo ni idadi ya ng’ombe kuanzia saba na mbuzi au kondoo saba.
Baada ya
fidia hiyo hufanyika matambiko fulani ambayo huashiria kusameheana na kushiriki kula chakula pamoja.
Mwanamke aliyeshindwa kujifungua- Mwanamke aliyeshindwa kujifungua
mtoto akiwa ndani ya ndoa au nje ya ndoa (ukiacha masuala ya kiafya), mara
nyingi huadhibiwa kwa kupakwa majivu kama mchawi.
Mbali ya
majivu hayo hunyolewa nywele kwa kutumia aidha chupa, wembe,mkasi na kisu huku
akikatwa au kung’atwa kichwani na
kufanyiwa vidonda vya makusudi, pia huanza kufanya kazi kabla ya kupona.
Kuoa-Katika suala la kuoa au kuolewa mara
nyingi wazazi wa kijana ndio wanaochagua
binti wa kuoa wakati upande wa binti wazazi hufuatilia historia ya jina na
wazazi wao kama wana sifa ya kuwa ndugu wa kuoana.
Idadi halisi
wanawake wa kuona ni kuanzia wawili hadi wadi wanne inategemea utajiri wa mtu
mwenyewe na wingi wa shughuli zake.
Baada ya
kuoana, marafiki wa pande zote mbili walisiosimamia ndoa hiyo hufanyiwa
matambiko ya kupakwa mafuta ya ng’ombe usomi
ikiwa ni laana ya kutoibiana wala
kutembea na mke wa mwenzie.
Mahali za kuoa mwanamke enzi za mababu zetu
ilikuwa ni ng’ombe 80-60, enzi za baba zetu 50-30 lakini hadi sasa 20-6 ambapo thamani ya ng’ombe mmoja sasa ni
Sh 300,000- 500,000.
Wanawake
kuoana ‘nyumba ntobhu’
Suala la
wanawake kuoana ni jambo ambalo linafanywa na Kabila la Wangoreme na Wakurya,
hii hufanyika pale aidha mwanamke anapojifungua watoto wote wa kike na kuolewa
wote.
Pia hutokea
pale mwana mke anapokuwa ndani ya ndoa lakini haukufanikiwa kupata mtoto hata mmoja ambapo hulazimika kuoa mke
mwenzake na kumpa uhuru wa kuzaa na mtu yeyote au kumchagulia mwanaume ndani ya
familia au ukoo wake.
Lengo kuu la
mke kuoa mke mwenzake ni kupata mtoto wa kiume ili kuendeleza ukoo wake na
kusimamia mali zake alizonazo.
Hukumu ya Wangoreme-Ukiweka pembeni sheria, hukumu kubwa ya Wangoremaikiwa
umefanya kosa kisha unakana kukusanywa
vitu vinavyoaminiwa ni hatari kwa afya yako na kulazimishwa kuviruka, pia kuna
fuvu la kichwa cha binadamu ‘ekehore’ ambalo huwekwa maji machafu ya nguo zako
na kunyweshwa.
Kukeketwa/kutahiriwa-Enzi za mababu wetu kijana au binti
kutahiriwa-kukeketwa ni miaka 18-25 kwa kutumia kisu na wembe lakini kutokan na
mabadiliko ya teknolojia jinsia ya kike imepigwa marufuku.
Pamoja na
kupigwa marufuku bado ukeketaji unaendelea kwa jinsia ya kike na vitendo hivyo
hufanyika kati ya umri mwaka mmoja hadi mitano kwani imani ni kupunguza hamu ya
kujamiliana. Pia Wangoreme wanaamini kuoa mwanamke ambaye hajakekeketwa ni
kuleta mkosi au haramu nyumbani.
Mapigano ya ukoo-Awali kulikuwa na mapigano ya koo na
koo ambapo yalimalizwa kabisa kwa kuanzisha utaratibu kubadilisha watoto katika
pande mbili jambo hilo husimamiwa na mabalozi wa nyumba kumi.
Ni kwamba
kama mwanamke amejifungua watoto zaidi ya watatu anachukuliwa na kukabidhiwa
koo nyingine hivyo upande wa pili kitendo ambacho kimewafanya kuwa kitu kimoja
yaani ndugu wa damu.
Chakula,ufugaji-Asili ya Wangoreme ni wafugaji wa
wanyama aina ya ng’ombe, mbuzi, kondoo, kuku na ndege aina ya kuku, bata, njiwa
ambapo viumbe hivyo hutumika kama kitoweo, kitega uchumi.
Pia mazao
yanayolimwa na Wangoreme ni mahindi, mtama, mihogo, viazi vitamu, maboga, ulezi
ambapo zao kuu la biashara ni pamba,
ufuta, karanga na Tumbaku.
Mboga halisi
ya Wangoreme ni majani ya kunde,maharage, mlenda, msusa, mchicha na wakati wa
kubadilisha au kuwapo kwa mgeni ni dagaa, nyama, samaki na vitoweo vingine.
Masharti katika Chakula.
Miiko ya
wangoreme ni kwamba wamefanya mgawanyo katika suala la nyama, kwanza vijana
wametengewa kula kidali, wanawake wametengewa kula shingo, bibi miguu na baba
na wazee wengine moyo na mgongo.
Ikibainika
mmoja amekula sehemu ya nyama ya kundi fulani inaweza kuleta ugomvi mkubwa na
hata aliyekula atakwenda kuinunua dukani na atashitakiwa kwenye vikao vya
familia.
Mgeni wa
heshima anapotembela rafiki yake anachinjwa mbuzi, ng’ombe au kuku lakini moja
ya sharti ni kwamba kama amechinjiwa yeye lazima ale filigisi na asipoiona
mezani atasusa kula.
Nguo- Asili ya nguo za kabila la
Wangoreme enzi hizo zilikuwa ni ngozi za wanyama hasa mbuzi na swala ambapo zilikuwa zinaambwa na kuondolewa
nywele zote na aliyeruhusiwa kuzivaa ni kijana mwenye umri miaka 18 na
kuendelea lakini baada ya nguo kuja walianza kuvaa hadi leo.
Silaha-Silaha kubwa ya kabila la Wangoreme ni upinde na mikuki
ambapo mafunzo ya kutumia zana hizo hufanyika wakati wa jando.
Ili
kuhakikisha umekuwa hodari na mtaalamu wa silaha hizo lazima vijana hao
wanaagizwa hifadhini kuwainda wanayama na kuleta nyama nyumbani.
Msiba,wizi- Wakati wa msiba, watu wote wa jirani
na ndugu hujumuika pamoja kushiriki mazishi.
Lakini mzee anapofariki asiyekuwa na mali mara
nyingi anazikwa kama alivyozaliwa na ili kuepusha kuzikwa hivyo huwa na
utaratibu wa kuweka mtoto wake wa kike rehani kwa mtu mwenye uwezo ili ampe
ng’ombe ya kushughulikia msiba.
Mtoto
anapokuwa mkubwa ataolewa na kijana wa yule aliyetoa msaada kwa familia ya
marehemu aidha kwa kuongeza mahali nyingine au ile ya awali inategemea na
wakati uliopo.
Kwa upande wizi
unapotokea ndani ya kabila la Wangoreme lazima itapigwa baragumu ikiashiria
hatari na watu wote huondoka nyumbani na upinde, mikuki wakiwa tayari kwa lolote.
Nyumba, Vitanda-Nyumba za asili za Kabila la
Wangoreme ni msonge ambazo zinajengwa na miti lakini kwa upende wa mwezekaji
nyasi hutafutwa mtaalamu ili kuzuia maji ya mvua yasiingie ndani.
Kwa upande
wa vitanda vya asili ni kuunganishs miti kwa mfani wa kitanda cha kisasa lakini
panapotakiwa kuweka change inaambwa ngozi ya ng’ombe.
Nyimbo
Pia nyimbo
zao za asili ni zeze na ngoma aina ya mbegete, kinanda, lukana ambapo
zinapopigwa huchezeshwa mabega huku wanawake
na wanaume husogeleana kwa kukusana vifua.
Maoni -O769 688300
================
MIPAKA YA VIJIJI ITATUGHARIMU BAADAYE
Mapigano ya
mipaka ya majimbo yazuka Mara
*RC aizuia tume
ya wizara
*Asema ilienda
kinyemela
*Wassira, Dk.
Kebwe wanena
*Mipaka
yang’olewa
*Wananchi
waahidi kumwaga damu
Na Benjamin Masese, Dar es Salaam
MAJIMBO matatu ya
wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mara yameingia katika mvutano mkali wa kugombea mipaka yao huku dalili za wazi za wananchi kushika
mapanga, mishale na upinde zikianza kuonekana.
Mipaka hiyo ni ile
inayotenganisha Wilaya ya Musoma Vijijini, Serengeti, Bunda ambayo inahusisha vijiji vya Sirori
Simba(Musoma Vijijini), Remng’orori (Serengeti) na Mekomariro (Bunda).
Mgogoro wa mipaka hiyo ulianza kuibuika kwa mara ya
kwanza mwaka 1978 lakini hakuna
suluhisho lililopatikana licha ya mikutano kadhaa kufanyika ikiwahusisha viongozi
ngazi ya mkoa.
Waliovamia maeneo ya mipaka hiyo ni wafugaji, wakulima huku wakianza kuweka
makazi ya kudumu na shughuli za kijamii ambapo pande zote zikidai yuko Wilaya yake.
Dalili za
kuanza mapigano hayo zilianza kuonekana mwanzoni mwa mwezi huu baada ya
wananchi wa Wilaya ya Musoma Vijijini kung’oa mabango ambapo wananchi wa Wilaya ya Bunda wao
wakichimba mitaro na kuweka alama za mipaka inayowatenganisha na Wilaya ya Serengeti na Bunda huku wakitoleana
vitisho.
DC Serengeti
Akizungumza
na MTANZANIA juzi kwa njia ya simu, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Joshua Mirumbe alikiri kuwapo na mgogoro huo huku
akisema kuwa umeanza kushughulikiwa na ngazi zote.
“Ni kweli
upo mgogoro huo naohusisha wilaya tatu lakini kutokana na uzito wa suala hilo tayari tume imetoka
Makao Makuu ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuja kushughulikia
mipaka hiyo.
“Hivi
tunavyozungumza viongozi ngazi ya mkoa, wilaya, kata, tarafa, vijiji
wanashirikiana pamoja kuhakikisha kila mmoja anapata haki yake bila kuingia katika
mapigano,”alisema kwa ufupi.
RC Mara
Akizungumza jana kwa njia simu, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Gabriel
Tupa alikiri kuwapo na mgogoro huo huku akiwaomba wananchi kutoingia kwenye
mapigano ya wao kwa wao kwa kuwa athari yake ni kubwa.
“Mgogoro huu ni mkubwa na ndio maana watalaam kutoka makao
makuu ya Wizara ya Ardhi wameletwa ikiwa lengo ni kupata suluhisho
lisilopendelea upande mmoja.
“Hasira za wananchi zilitokana na watalaam hao kwenda kwa
wananchi bila kuwa na wakuu wa wilaya zote tatu huku wakitumia jina langu
kwamba nimewaagiza.
“Kwa kweli walikosea na ndio maana nimewasimamisha kwanza na
kuwaagiza wakuu wa wilaya wazungumze nao kwa kuwapa elimu na kuwashauri watoe
ushirikiano ili wote kwa pamoja tupate suluhisho la kudumu.
“Kikubwa ninachosema ni kwamba uamuzi wa mgogoro huu upo mikononi
mwao lakini kama wamejiandaa na mapiganoya mikuki, mishale na mapanga ni
kuongeza tatizo.
“Nawasihi watoe ushirikiano kwa kuwa kamati zote zitaundwa na wao ambapo watatoa historia yote ya mipaka
kwa tume ya wizara ili kupata taswira halisi, pia nawaomba wananchi kuwa na
subira hadi tume itakapokamilisha kazi yake,”alisema.
Mwenyekiti Remng’orori
Kwa upande
wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Remg’orori, Justen Mgaya Baritile alisema mgogoro huo umedumu kwa miaka mingi.
Baritile
alisema kuwa mipaka iliyokuwa ikitambulika tangu enzi hizo ni ile ya mwaka 1978
lakini umekuwa ukisusua kupata suluhisho la kudumu.
Alisema
baada ya mgogoro huo kuibuka tena mwaka 1996 kulifanyika mkutano katika eneo hilo la mipaka
iliyohusisha viongozi wote ngazi ya mkoa, wilaya na wananchi wa pande zote tatu
hazikuafikiana.
Licha ya
kutoafikiana katika mkutano huo, maafisa watendaji wa kata inadaiwa walisaini
makubaliano hayo bila wananchi kuiridhia.
Baritile
alisema kuwa mgogoro huo tena uliibuika mwaka 2002 ambapo kulifanyika mkutano eneo hilo hilo na
kuhudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Thomas Loi Sabaya (wakati huo), Mkuu
wa Wilaya ya Bunda, Hawa Mchopa ambaye pia alihudhuria kama Kaimu Mkuu wa mkoa
wa Mara.
Alisema
mkutano huo ulikaa Februari 28 ,2002
ambapo walipendekeza kuwa mpaka wa Bunda na Serengeti utapita kuanzia mto
mwikoma, Nyagubesi, Nyabetunguri, mlima bikaili hadi jiwe moja, Kewaiwai, Bonde
la mtemi Makongoro hadi Mto Tirina.
Mpaka kati
ya Serengeti na Musoma Vijiji walipendekeza kupita Kijiji cha Sirori Simba eneo
la Bonde la Nyagubesi, Nyabetunguri,
mlima Buruta hadi palipowekwa vibao vya Tanroad barabarani kama
ishara ya mwisho wa jimbo la Musoma
Vijijini.
Alisema kuwa
licha ya kukubaliana lakini mgogoro huo uliendelea kufukuta na kulazimika tena
kukaa mkutano Desemba 12, 2002 na kuhudhuria na viongozi wa ngazi kuanzia mkoa
hadi kijiji ambapo waliwatumia wazee maarufu na wa kale ili kutoa historia.
Hata hivyo
taarifa
Kwa Mwenyekiti (0786480194) wa Kijiji cha Sirori Simba,
Alexander Makile Nyangalesi alisema kuwa maamuzi yatakayotolewa na tume
yatakuwa ni sahihi.
Wassira
Kwa upande
wa Mbunge wa Jimbo la Bunda (CCM), Steven Wassira alikiri kuwapo na mgogoro huo
huku akienda mbali na kusema unahusisha wilaya nne yaani Serengeti, Bunda,
Butiama na Msoma Vijijini.
Wassira
ambaye ni Waziri wa Ofisi ya Rais, alisema migogoro yote ya wilaya hizo inahusu
mipaka ambayo inapaswa kutenganisha Serengeti na Bunda, Serengeti na Musoma
Vijijini na Butiama na Bunda.
Wasira
alisema kuwa mipaka ya Wilaya ya Serengeti, Bunda na Butiama inahusisha vijiji
vya Mikomariro, mahanga na Ikizu ambapo upande Musoma Vijijini na Serengeti
unahusisha kijiji cha Sirori Simba na Remng’orori.
Pamoja na
ufafanuzi wake, alisema mipaka hiyo itapata muafaka kwa kurejea historia ya
tangu watawala wa ‘machifu’ walivyokuwa
wakitawala.
Wassira
alipinga vikali juu ya tuhuma dhidi yake kwamba anawatumia matajiri
wa jimbo lake
kuendeleza mapambano ya
kumega ardhi ya Serengeti.
“Sina nia ya
kuchukua ardhi ya Serengeti, hayo ni mawazo potofu ya wenye nia mbaya na
mimi,kwanza kwenye jimbo langu sina matajiri na wananchi wangu ni wa hali ya
kawaida.
“Kwanza
mipaka ya wilaya hizo iliwekwa wakati mimi nikiwa Mkuu wa Wilaya, sasa kama nilikuwa na nia hiyo ningetumia mwanya huo, suala la
watu kunichafua kwenye mitandao ya kijamii ni ijinga, tushirikiane kupata
muafaka,”alisema.
Dk. Kebwe
Kwa upande
wa Mbunge wa Serengeti, Dk. Kebwe Steven Kebwe alisema kwa ufupi
kwamba ana imani na tume itamaliza mgogoro huo.
Kuhusu tuhuma
za wananchi wakewakidai kushindwa kuitetea ardhi yao,
alisema kuwa hatua ya tume kwenda eneo hilo
ni jitihada zake na vikao vyote vya RCC kilichokaa Oktoba 17,2012 aliwatetea
wananchi juu ya mipaka hiyo.
MWISHO
No comments:
Post a Comment