IMEGUNDULIKA kuwapo na mtandao hatari nchini unaohusisha Hazina na
Halmashauri mbalimbali kuchota mamilioni ya fedha huku wakiziandikia
kutumika katika miradi ya maendeleo.
Mtandao huo ambao umeelezwa kuwahusu viongozi ngazi ya juu wa Hazina na
Halmashauri umekuwa ukiongeza fedha za ziada kati ya Sh. Milioni 500
hadi 600 kwenye fedha halali za miradi ya maendeleo zilizoidhinishwa
kisheria na Bunge.
Tayari mtandao huo umedaiwa kufanikiwa kuidhinisha mamilioni ya fedha
katika Halmashauri tatu ambazo ni Mbarali, Korogwe Mjini na Mvomero.
Hayo yalielezwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Rajab Mohamed Mbarouk
alipokuwa akifanya majumuisho ya vikao vya kamati yake.
Mbarouk alisema kumeibika mtandao hatari wa kujichotea fedha za Serikali
kwa kusingizia zinakwenda Halmashauri lakini zinapofikishwa huko
zinawarudia wenyewe.
“Hii nchi sio masikini na hakuna sababu ya kusikia eti miradi imekwama
kwa sababu ya fedha kukosa, katika vikao vyetu tumebaini kwamba Hazina
na Halmashauri nchini zinashirikiana kula fedha za Serikali.
“Mfano halisi ni huu Halmshauri ya Mbarali katika mahesabu yamahitaji
yao yote walitakiwa kupewa Sh. milioni 70 lakini Hazina walipeleka Sh.
milioni 700.
“Fedha hizo zinapofikishwa kule zinaidhinishwa kupokelewa Sh. milioni 70
zilizokuwa zikihitajika zile zilioongezwa zinazrudi mikononi mwa
mtandao huo ambao ni katika Hazina na Halmashauri.
“Halmashauri ya Mbarali imekuwa imekuwa ikipata hati chafu mpaka leo
ninavyoongea hapa katika kuboroga kwenye mahesabu yao ya fedha
wanazopokea na jinsi wanavyozitumia.
“Kama unataka kuona mtandao huo umeota mizizi mikubwa, tumebaini
utakaswaji wa fedha umefanyika Halmashauri ya Korogwe Mjini Sh.milioni
500 huku mahitaji yao yakiwa chini ya Sh. milioni 100.
“Hivyo hivyo utakaswaji huo umefanyika Halmshauri ya Mvomero kwa
kupelekea Sh. milioni 500 ambapo mahitaji yao hayakuwa yanafikia kiasi
hicho, kama wana kamati tumechukizwa na utoroshwaji wa fedha hizo na
tutalifikisha bungeni kwa hatua zaidi.
“Cha ajabu unakuta viongozi wanaohusika katika Halmashauri hizo
wanapofanya utakaswaji huo wanawahi kuhama, mfano halisi ni aliyekuwa
Mhasibu wa Halmshauri ya Mvomero,Nassoro Mkwanda ambaye hivi sasa yupo
Halmshauri ya Kiteto kwa cheo hicho hicho,”alisema.
Mbarouk alisema kama mtandao huo hautadhibitiwa haraka taifa litaendelea
kufilisika na maendeleo ndani ya jamii yakikwama ambapo athari yake ni
uchumi kushikiliwa na wachache huku kundi kubwa ni masikini.
Mkurugenzi Kiteto amwaga machozi
Awali ya yote, Kamati ya LAAC ilikutana na viongozi wa Halmashauri ya
Wilaya ya Kiteto kupitia mahesabu yao ambapo ilikubaini ubadhirifu
mkubwa wa fedha kitendo kilimfanya Mkurugenzi halmashauri hiyo, Jane
Mutagurwa kulia ndani ya kikao.
Kugundulika kwa ubadhiri katika Halmshauri hiyo kulimfanya Mwenyekiti wa
LAAC, Mbarouk kuagiza polisi kufika hapo ili kuwaweka chini ya ulinzi
baada ya kikao kumalizika.
Kamati ilibaini Halmashauri ya Kiteto imepoteza Sh. milioni 500 ambazo
ambazo ni mapato ya kodi za mazao kutoka kwa vyama vya ushirika.
Ilibainika fedha hizo zilichukuliwa na wakala wa ukusanyaji wa ushuru
huo kwa idhini ya Halmashauri hilo kwa mkataba wao lakini wakotomea bila
kuzikabidhi.
Katika mahojiano kati ya wabunge wa kamati ya LAAC na viongozi wa
Halmashauri hiyo ilibainika kuwa kuna magari mawili ya Serikali yenye
usajili wa STK hayajulikani yalipo na anayeyamiliki licha ya kuonekana
kwenye vitabu vyao ni mali zao.
Pia ilibainika kuwa Sh. milioni 179 zimeanzwa kulipwa kwa watumishi
wanaoidai Halmashauri hiyo lakini hawajulikani kwa majina wala idara
zao.
Vile vile imegundulika kwamba Halmashauri hiyo imekutumia Sh.milioni 34
zilizotokana na mauzo ya mahindi ya msaada wa njaa iliyoikumba Wilaya ya
Kiteto na hazijawahi kurudishwa Ofisi ya Waziri Mkuu.
Ubadhirifu mwingine uliopatikana katika Halmashauri hiyo ni ujenzi wa
jiko la kisasa lililogharimu Sh. milioni 25 lakini limeshindwa kutumika
na badala wameligeuza kuwa nyumba ya mwalimu huku taarifa zao zikieleza
vitu vyote vimekwekwa kumbe ni uongo.
Hata hivyo ilibainika mamilioni ya fedha yanayotengwa na Serikali
kwemnda miradi mbalimbali ya maendeleo vijijini na mfuko wa kuwawezesha
wanawake na vijana hayawafikii ipasavyo.
Ilibainika miradi mingi ya ujenzi wa shule za msingi na Sekondari
ikiwani ya Kiperesi ikishindwa kukamilika huku fedha zilizotengwa zikiwa
zimetolewa kitendo ambacho kiliwafanywa wajumbe wa LAAC kupendekeza
kuvunjwa kwa Halmshauri hiyo.
Wakati Mkurugenzi, Mutagurwa alipotakiwa kutoa majibu ubadhiri huo
alipatwa na wasiwasi na kigugumizi kueleza wazi na kuanza kulia.
Viongozi wengine waliokuwa wamsaidia kujibu hoja ni Ofisa Mipango wa
Halmashauri hiyo,Rabson Magesa, Mwenyekiti wa Halshauri ya Wilaya ya
Kiteto, Mainge Lemalali na viongozi wengine ambao ilionekana kumsukimia
mkurugenzi wao.
Kutokana na kutokuwapo na majibu sahihi, Mbarouk alimua kuwatoa nje
viongozi wengine ispokuwa Mkurugenzi ili kuhoji peke yake ambapo
ilibainika kwamba viongozi waliomzunguka wanamhujumu huku jamii ya
wamasai wakimdharau ni jinsia yake ya kike.
Mbarouk aliamua kusiktisha mpango wa kumweka chini ya ulinzi wa polisi
baada ya kuelezwa hivyo na kuamua kuunda kamati ndogo ya kuchunguza
ubadhirifu na hali halisi ilivyo Kiteto.
Pia alipewa muda wa kuhajikisha fedha pamoja na gari mbili zinapatikana
kabla ya Disemba 31, mwaka huu ingawa aliomba kuongezewa muda hadi Juni
2014 kitendo kilichopingwa vikali.
MWISHO.
Monday, 9 September 2013
WALEMAVU WANAVYOTESEKA DAR ES SALAAM
Siri nzito ya walemavu wanavyoteseka Dar.
INASIKITISHA na kuleta huzuni ndani ya moyo wako pale unapojikuta unawapoteza wazazi wako wote huku ukikosa msaada kutoka kwa ndugu wa karibu na kuamua kujiunga na kundi la ombaomba barabarani. Baadhi ya watu wanao kuwa wakiomba msaada hasa wale walemavu wa viungo mbalimbali wa mwili wamekuwa wakileta huzuni kwa wapiti njia kutokana na ulemamavu wao ambao ni mipango ya Mungu. Sote ni mashahidi kuwa baadhi ya walemavu wa mikono, miguu, vipofu na viungo vingine wakiomba msaada kwa madereva, watembea kwa miguu na kwenye ofisi za Serikali na binafsi na maeneno mengine. Lakini wapo wengine ambao hawana tatizo lolote lakini wameamua kuingia katika kundi hilo jambo ambalo limekuwa likizua maswali ya kwamba kwanini wasijishughulishe na biashara ndogondogo. MTANZANIA Jumatatu ilifanya mahojiano na mlemavu mmoja wa miguu yote ambaye amekuwa akitembea mithili ya mnyama mwenye miguu minne wakati akiomba msaada katika kituo cha daladala Ubungo. Mlemavu huyo aliyejitambulisha kwa jina la Yusuph Said (24) mzaliwa wa Kijiji cha Mikese mkoani Morogoro anaeleza maisha anayoishi eneo la Manzese Darajani jijini Dar es Salaam ambayo ni hatari kwa usalama wa uhai wake. Said ambaye alisoma Shule ya Msingi Kitega na baadaye kujiunga na Sekondari ya Mikese zote za mkoani Morogoro anaeleza kwamba alikimbiwa na ndugu zake baada ya wazazi wake wote kufariki 2000 kutokana na maradhi mbalimbali. Akizungumza kwa huzuni ya kuwapoteza wazazi wake ambao walikuwa wanamlea kulingana na hali yake ya ulemavu alijikuta akikosa mtu wa kukaa naye kitendo kilichomfanya kukimbilia kwa shangazi yake Muhombola Salum. Said anasema alikimbilia kwa shangazi yake baada ya ndugu zake wa kuzaliwa tumbo moja kumkimbia na kuanzisha maisha yao maeneo mengina huku shughuli zao kubwa ni kuchoma mkaa porini. Anasema maisha kwa shangazi yake yalizidi kuwa magumu kutokana na kutokuwa na uwezo kwani uhakika wa kula kila siku haukuwapo ambapo alishindwa kuvumilia njaa na kukimbilia Dar es Salaam baada ya kupata taarifa kuwa walemavu wanapata msaada barabarani kwa kuombaomba. Hakika, ukimtazama Said hali yake ni vigumu kuvumilia kumsikiliza au kumwangalia kwani mwili wake unaonekana kutooga siku nyingi, nguo chafu, shuka analojifunika chafu ana anatembea nalo muda wote kwa kuhofia kumwibia. Pia inadhihirisha kabisa ameanza kuathirika kisaikolojia kutokana na mazingira anayoishi na inathihirisha wazi ameanza kutumia dawa za kulevya. Said ambaye alikataa kuweka wazi vitendo wanavyofanyiwa walemavu wanaoishi eneo la Manzese Dar es Salaam nyakati za usiku kwa kuhofia maisha yakwe, anasema anatamani kurudi nyumbani lakini anashindwa wapi atafikia. “Pale Manzese kuna masela wengi sana, wanatufanyia mambo mengi lakini siwezi kuyataja hapa naogopa na ndio maana sisi walemavu tumejitenga na banda letu. “Hii ni shuka ninayojifunika natembea nayo muda wote kwa ukiachaa unaibiwa, kuoga kwangu au kufua nguo hizi mara nyingi ninasubiri mvua inaponyesha. “Mimi nilikuwa nalelewa na wazazi wangu bila kutekeseka na walikuwa wameninunulia baiskeli lakini walipofariki iliharibika na hakuna aliyenitengenezea lakini nashukuru hadi leo naishi kwa msaada wa watu. “Ukiamua kuwahoji wapiga watu tunaolala nje watakueleza mambo mengi sana, kuna vituko tunafanyiwa sio kwmaba tunapenda ni kwa sababu huna jinsi,”anasema kwa masikitiko. Said anasema kwamba kutokana na kukaa kituoni tena juani kwa kuomba pesa abiria, madereva na makondakta amekuwa akiugua kila siku lakini baada ya kupata kiasi hutenga kwa kula chakula na kununua dawa la kutuliza maumivu. Anasema kwamba anahofia kwenda hospitali kutibiwa kwa kile alichodai hatapewa fursa ya kupata matibabu kwa sababu ya pesa na hali yake ilivyo. Anasema kwa siku inaweza kupata Sh 5,000 lakini kutokana na mazingira anayoishi hazitoshi na kuongeza kwmaba pengine hunyang’anywa na masela nyakati za usiku. Anaeleza kwamba mbali ya kunyang’anywa fedha pia kupokonywa simu jambo ambalo linamfanya kutonunua simu, nguo au kutunza fedha za ziada. Anasema kutokana na hali hiyo hulazimika kuchimba shimo na kufukia baadhi ya fedha zake anazopata kutoka kwa watu wanaoguswa na hali yake. Said aliwataja baadhi ya ndugu wa kuzaliwa ni pamoja na Oluka, Salum, Hiari, Shukuru na Hamis ambao wapo porini wakiendesha shughuli zao za kukata miti na kuchoma mkaa mkoani Morogoro. Pamoja na mambo ya Said lakini ombi lake kubw ani kuiomba Serikali kumsaidia baiskeli ya kutembelea au kumpeleka katika kituo chochote za kulelea watu wasio na uwezo. Said anasema mbali ya kumpeleka kituoni, anaomba msaada wa fedha ili kuanzisha biashara ndogo ambazo anaweza kusifanya kwa kutumia mikono ambayo haina ulemavu wowote. Ni dhahiri kwamba Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto inapaswa kutambua matatizo yanayowapata watu wanaojihusisha na ombaomba barabarani. Inagawa ni vigumu Serikali kuwachukua watu wote walio mitaani na kuwatunza lakini kuja haja ya kuchukulia uzito kwa watu wenye ulemavu hata kwa kuwapeleka katika vituo vya kulelea watu wasio na uwezo. Si kwamba walemavu wote wanapenda kukaa kwenye vituo hivyo la hasha, bali wengine wanataka kupata msaada wa fedha ili kuanzisha biashara ambayo wanaweza kuifanya kulingana na mazingira yao. Pia Serikali inapaswa kuweka wazi juu ya huduma kwa walemavu katika hospitali za umma ili waweze kupata huduma bure kwa sababu ya hali zao ambazo haziwawezeshi kupata kipato cha kujikimu, hii itasaidia pale wanapougua walemavu waweze kupata matibabu kwa sababu wana haki sawa. Walemavu wanapoachwa bila kupewa huduma ni moja ya sehemu ya kuwafanyia ukatili. Sote tunafahamu ukatili ni vitendo vya makusudi vinavyofanywa na mtu au kikundi dhidi ya mtu, watu wengine ambavyo huwa na madhara ya kimwili, kiakili na jisaikolojia. Dhana hii haimanishi kuuawa kwa binadamu pekee bali ukatili unaweza kujitokeza katika sura tofauti na maneno mbalimbali kama ukatili wa nyumbani, kiuchumi, kimila na desturi katika makabila, mahusiano ya kimapenzi, usafirishaji haramu wa binadamu, vitisho na matumizi ya kutumia nguvu. Hivyo watu walio barabarani wakiomba msaada wa kusaidia wapo katika kundi la ukatili wa kiuchumi ndio uliowafanya kuingia barabarani kujipatia riziki zao. Kwa mujibu wa Said amesema kwamba nyakati za usiku hufanyiwa vitendo vya ajabu ambavyo hakuta kuvieleza wazi, lakini kwa akili ya kawaida inadhihirisha kundi hilo linateseka sana . Ukatili unaweza kutoka katika kundi lolote ndani ya juamii ikiwa ni kwa mwanamke, mwanaume, mvulana, msichana au mototo. Ili kutambua madhara ya ukatili wa kijinsia kwa walengwa hao ni muhimu kufanya linalowezekana kuhakikisha vitendo hivyo vinatokomezwa kuanzia ngazi ya familia hadi taifa kuona kila binadamu ana haki katika hali yoyote ile. Ingawa mateso wanayopata walemavu barabarani jamii imekuwa ikiyachukulia pengine ni uamuzi wa mtu kupenda kuingia katika kundi hilo lakini sivyo ilivyo bali inalazimu kutokana na hali halisi ya maisha. Umefika wakati sasa wizara, idara, taassi na kampuni binafsi kuona kundi la walemavu ni moja ya watu wanaopaswa kusaidiwa katika kila hali kwa sababu hayo ni mapenzi ya Mungu. Pia vitendo vya baadhi ya familia kuwatelekeza watoto wanaozaliwa kwa ulemavu au kupata ulemavu wakiwa watu wakubwa ni jambo la kikatili , ni vema mlemavu akadhaminiwa kama ilivyo kwa wengine. Maoni 0769 688 300
INASIKITISHA na kuleta huzuni ndani ya moyo wako pale unapojikuta unawapoteza wazazi wako wote huku ukikosa msaada kutoka kwa ndugu wa karibu na kuamua kujiunga na kundi la ombaomba barabarani. Baadhi ya watu wanao kuwa wakiomba msaada hasa wale walemavu wa viungo mbalimbali wa mwili wamekuwa wakileta huzuni kwa wapiti njia kutokana na ulemamavu wao ambao ni mipango ya Mungu. Sote ni mashahidi kuwa baadhi ya walemavu wa mikono, miguu, vipofu na viungo vingine wakiomba msaada kwa madereva, watembea kwa miguu na kwenye ofisi za Serikali na binafsi na maeneno mengine. Lakini wapo wengine ambao hawana tatizo lolote lakini wameamua kuingia katika kundi hilo jambo ambalo limekuwa likizua maswali ya kwamba kwanini wasijishughulishe na biashara ndogondogo. MTANZANIA Jumatatu ilifanya mahojiano na mlemavu mmoja wa miguu yote ambaye amekuwa akitembea mithili ya mnyama mwenye miguu minne wakati akiomba msaada katika kituo cha daladala Ubungo. Mlemavu huyo aliyejitambulisha kwa jina la Yusuph Said (24) mzaliwa wa Kijiji cha Mikese mkoani Morogoro anaeleza maisha anayoishi eneo la Manzese Darajani jijini Dar es Salaam ambayo ni hatari kwa usalama wa uhai wake. Said ambaye alisoma Shule ya Msingi Kitega na baadaye kujiunga na Sekondari ya Mikese zote za mkoani Morogoro anaeleza kwamba alikimbiwa na ndugu zake baada ya wazazi wake wote kufariki 2000 kutokana na maradhi mbalimbali. Akizungumza kwa huzuni ya kuwapoteza wazazi wake ambao walikuwa wanamlea kulingana na hali yake ya ulemavu alijikuta akikosa mtu wa kukaa naye kitendo kilichomfanya kukimbilia kwa shangazi yake Muhombola Salum. Said anasema alikimbilia kwa shangazi yake baada ya ndugu zake wa kuzaliwa tumbo moja kumkimbia na kuanzisha maisha yao maeneo mengina huku shughuli zao kubwa ni kuchoma mkaa porini. Anasema maisha kwa shangazi yake yalizidi kuwa magumu kutokana na kutokuwa na uwezo kwani uhakika wa kula kila siku haukuwapo ambapo alishindwa kuvumilia njaa na kukimbilia Dar es Salaam baada ya kupata taarifa kuwa walemavu wanapata msaada barabarani kwa kuombaomba. Hakika, ukimtazama Said hali yake ni vigumu kuvumilia kumsikiliza au kumwangalia kwani mwili wake unaonekana kutooga siku nyingi, nguo chafu, shuka analojifunika chafu ana anatembea nalo muda wote kwa kuhofia kumwibia. Pia inadhihirisha kabisa ameanza kuathirika kisaikolojia kutokana na mazingira anayoishi na inathihirisha wazi ameanza kutumia dawa za kulevya. Said ambaye alikataa kuweka wazi vitendo wanavyofanyiwa walemavu wanaoishi eneo la Manzese Dar es Salaam nyakati za usiku kwa kuhofia maisha yakwe, anasema anatamani kurudi nyumbani lakini anashindwa wapi atafikia. “Pale Manzese kuna masela wengi sana, wanatufanyia mambo mengi lakini siwezi kuyataja hapa naogopa na ndio maana sisi walemavu tumejitenga na banda letu. “Hii ni shuka ninayojifunika natembea nayo muda wote kwa ukiachaa unaibiwa, kuoga kwangu au kufua nguo hizi mara nyingi ninasubiri mvua inaponyesha. “Mimi nilikuwa nalelewa na wazazi wangu bila kutekeseka na walikuwa wameninunulia baiskeli lakini walipofariki iliharibika na hakuna aliyenitengenezea lakini nashukuru hadi leo naishi kwa msaada wa watu. “Ukiamua kuwahoji wapiga watu tunaolala nje watakueleza mambo mengi sana, kuna vituko tunafanyiwa sio kwmaba tunapenda ni kwa sababu huna jinsi,”anasema kwa masikitiko. Said anasema kwamba kutokana na kukaa kituoni tena juani kwa kuomba pesa abiria, madereva na makondakta amekuwa akiugua kila siku lakini baada ya kupata kiasi hutenga kwa kula chakula na kununua dawa la kutuliza maumivu. Anasema kwamba anahofia kwenda hospitali kutibiwa kwa kile alichodai hatapewa fursa ya kupata matibabu kwa sababu ya pesa na hali yake ilivyo. Anasema kwa siku inaweza kupata Sh 5,000 lakini kutokana na mazingira anayoishi hazitoshi na kuongeza kwmaba pengine hunyang’anywa na masela nyakati za usiku. Anaeleza kwamba mbali ya kunyang’anywa fedha pia kupokonywa simu jambo ambalo linamfanya kutonunua simu, nguo au kutunza fedha za ziada. Anasema kutokana na hali hiyo hulazimika kuchimba shimo na kufukia baadhi ya fedha zake anazopata kutoka kwa watu wanaoguswa na hali yake. Said aliwataja baadhi ya ndugu wa kuzaliwa ni pamoja na Oluka, Salum, Hiari, Shukuru na Hamis ambao wapo porini wakiendesha shughuli zao za kukata miti na kuchoma mkaa mkoani Morogoro. Pamoja na mambo ya Said lakini ombi lake kubw ani kuiomba Serikali kumsaidia baiskeli ya kutembelea au kumpeleka katika kituo chochote za kulelea watu wasio na uwezo. Said anasema mbali ya kumpeleka kituoni, anaomba msaada wa fedha ili kuanzisha biashara ndogo ambazo anaweza kusifanya kwa kutumia mikono ambayo haina ulemavu wowote. Ni dhahiri kwamba Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto inapaswa kutambua matatizo yanayowapata watu wanaojihusisha na ombaomba barabarani. Inagawa ni vigumu Serikali kuwachukua watu wote walio mitaani na kuwatunza lakini kuja haja ya kuchukulia uzito kwa watu wenye ulemavu hata kwa kuwapeleka katika vituo vya kulelea watu wasio na uwezo. Si kwamba walemavu wote wanapenda kukaa kwenye vituo hivyo la hasha, bali wengine wanataka kupata msaada wa fedha ili kuanzisha biashara ambayo wanaweza kuifanya kulingana na mazingira yao. Pia Serikali inapaswa kuweka wazi juu ya huduma kwa walemavu katika hospitali za umma ili waweze kupata huduma bure kwa sababu ya hali zao ambazo haziwawezeshi kupata kipato cha kujikimu, hii itasaidia pale wanapougua walemavu waweze kupata matibabu kwa sababu wana haki sawa. Walemavu wanapoachwa bila kupewa huduma ni moja ya sehemu ya kuwafanyia ukatili. Sote tunafahamu ukatili ni vitendo vya makusudi vinavyofanywa na mtu au kikundi dhidi ya mtu, watu wengine ambavyo huwa na madhara ya kimwili, kiakili na jisaikolojia. Dhana hii haimanishi kuuawa kwa binadamu pekee bali ukatili unaweza kujitokeza katika sura tofauti na maneno mbalimbali kama ukatili wa nyumbani, kiuchumi, kimila na desturi katika makabila, mahusiano ya kimapenzi, usafirishaji haramu wa binadamu, vitisho na matumizi ya kutumia nguvu. Hivyo watu walio barabarani wakiomba msaada wa kusaidia wapo katika kundi la ukatili wa kiuchumi ndio uliowafanya kuingia barabarani kujipatia riziki zao. Kwa mujibu wa Said amesema kwamba nyakati za usiku hufanyiwa vitendo vya ajabu ambavyo hakuta kuvieleza wazi, lakini kwa akili ya kawaida inadhihirisha kundi hilo linateseka sana . Ukatili unaweza kutoka katika kundi lolote ndani ya juamii ikiwa ni kwa mwanamke, mwanaume, mvulana, msichana au mototo. Ili kutambua madhara ya ukatili wa kijinsia kwa walengwa hao ni muhimu kufanya linalowezekana kuhakikisha vitendo hivyo vinatokomezwa kuanzia ngazi ya familia hadi taifa kuona kila binadamu ana haki katika hali yoyote ile. Ingawa mateso wanayopata walemavu barabarani jamii imekuwa ikiyachukulia pengine ni uamuzi wa mtu kupenda kuingia katika kundi hilo lakini sivyo ilivyo bali inalazimu kutokana na hali halisi ya maisha. Umefika wakati sasa wizara, idara, taassi na kampuni binafsi kuona kundi la walemavu ni moja ya watu wanaopaswa kusaidiwa katika kila hali kwa sababu hayo ni mapenzi ya Mungu. Pia vitendo vya baadhi ya familia kuwatelekeza watoto wanaozaliwa kwa ulemavu au kupata ulemavu wakiwa watu wakubwa ni jambo la kikatili , ni vema mlemavu akadhaminiwa kama ilivyo kwa wengine. Maoni 0769 688 300
UWEZO WA NAIBU SPIKA BUNGENI
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema uwezo wa Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai katika kuongoza Bunge unahatarisha amani, kuvunjika mshikamano na umoja wa kitaifa uliopo sasa kutokana na kutokuwa na mtazamo mpana wa kufikiri.
Pia kimesema kuna ajenda ya chini chini inayoendelezwa na baadhi ya mawaziri, wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na kiti cha Spika katika kuhujumu malengo na nia ya Rais Kikwete kuwa na katiba mpya ifikapo 2015.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba alisema kitendo cha Ndugai kuamuru polisi kumtoa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe ni cha aibu na kidikteta.
Profesa Lipumba alisema kuna baadhi ya viongozi Serikali (hawakuwataja) wanaojionesha wanamsaidia Rais Kikwete lakini ndani ya moyo wao wana ajenda za siri za kumhujumu.
Alisema kuwa viongozi hao wamekuwa wakitumia udhaifu wa Ndugai kwa kumshawishi kufanya kile wanachoona kinafaa kwa lengo la kukandamiza upinzania na kuhmhujumu Rais bila yeye kujua.
Alisema kuwa hivi Sasa Tanzania inakabiliwa na changamoto za matamshi hasi yanayotolewa na viongozi na asasi za Rwanda baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa ushauri wenye mantiki kwa Rais wa Rwanda, Paul Kagame kukutana na waasi wa kikundi FDRL kitendo ambacho kimeleta hali ya sintofahamu.
Pia alisema kuwa kitendo cha baadhi ya nchi za Afrika Mashariki kufanya vikao vyao na kuitenga Tanzania huku wakizungumzia namna ya kuinua uchumi wao, kitendo ambacho kinamweka Rais Kikwete katika changamoto kubwa.
Alisema kuwa kitendo cha kiti cha Spika hasa kinapokaliwa na Ndugai kimekuwa kikiendesha Bunge kwa kupendelea Serikali kwa kadri kinavyoweza huku kikizima hoja za upinzani kwa makusudi.
“Kuna njama za wazi zinafanywa na kiti cha Spika kwa kutelekeza maoni ya wananchi na kupendelea ya Chama Cha Mapiunduzi (CCM), kwa upande wa Zanzibar hawakushirikishwa vizuri na hata wabunge wa CUF wanasema hawakushirikishwa.
“Moja ya njama za wazi ni ile ya wabunge 166 wa bunge la katiba wanaoipaswa kupendekezwa na taasisi mbalimbali na kuteuliwa na Rais, sisi CUF kinasikitishwa na mchakato unavyoendeshwa na jinsi uteuzi unavyopendekezwa.
“Hii katiba mpya itakuwa ni ya CCM sio ya Watanzania, na ombi la wabunge wa CUF ni kutaka muswada urudishwe kwa wananchi na kamati ijadili upya.
“ CUF inaendelea na juhudi za kuwasiliana na viongozi wa vyama vingine ili kuweka mkakati wa pamoja na kukabiliana na hujuma dhidi ya mchakato wa kupata katiba mpya na kuimarisha umoja wa kitaifa,”alisema.
Profesa Lipumba alisema kuwa kitendo cha Ndugai kumnyima nafasi Mbowe kinadhihirisha ni mpango mkakati wa kuminya hoja za upinzani na kutumia nguvu kumtoa nje ya Bunge hakikubaliki na amevunja sheria.
Profesa Ibrahimu alihoji kwamba angesimama Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, je asingepewa nafasi ya kusikilizwa na kuongeza kwamba baadhi ya Wabunge wa CUF akiwamo Mozza Abeid walivuliwa hijabu zao kitendo ambacho ni udhalilishaji.
Sunday, 25 August 2013
OPERESHENI YA KUONDOA POLISI WASIOFAA
Na Benjamin Masese, Dar es Salaam
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi ametembeza panga kali ndani ya Jeshi la Polisi na kuwafukuza kazi maofisa wanne huku baadhi yao wakivuliwa vyeo vyao.
Maofisa hao ni wale waliohusika kushiriki kwa namna moja au nyingine katika matukio yaliyotokea mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro na Kigoma na kulalamikiwa vikali na wananchi.
Akizungumza na Waandishi wa habari Da r es Salaam jana alisema askari hao ni wale waliohusika kutumia gari la kutuliza Ghasia (FFU) kubeba bangi mkoani Arusha na Kilimanjaro
Tukio jingine ni lile la askari mkoani Morogoro kutumia fuvu la binadamu kumbambikizia mfanyabishara kwa lengo la kupata fedha, mauaji ya mfanyabishara wa Wilaya ya Kasulu yalifanywa na askari polisi.
Tukio la Bangi
Dk. Nchimbi alisema katika sakata la tukio la bangi amemvua madaraka yote aliyokuwa nayo Mkuu wa Kikosi cha FFU Mkoa wa Arusha, Mrakibu wa Polisi, Ramadhan Giro kwa kosa la kushindwa kusimamia kikamilifu askari na maofisa walio chini yake na kusababisha kutoke tukio hilo.
Pia amemsimamisha kazi Ispekta Isaac Manoni na kushitakiwa kijeshi kwa kosa la kutumiwa kumtorosha mtuhumiwa ambaye ni polisi Edward Mwakabonga aliyekuwa dereva wa gari la FFU kitendo kilicholifedhehesha jeshi hilo.
“Katika tukio hilo kitendo cha Inspekta Salum Kingu wa kikosi cha FFU Mkoa wa Kilimanjaro kubaki kwenye gari mita 80 kutoka ilipo nyumba ya mtuhumiwa Edward alipopelekwa Moshi kukabishi vifaa vya jeshi letu kimechangia, hivyo tumempa onyo kali la kuwa makini na utendaji wake.
“Pia Inspekta Mikidadi Galilima kutotimiza wajibu wake ipasavyo katika kumshauri Mkuu wa FFU Mkoa wa Arusha juu ya ukaguzi na usimamizi wa rasilimali na kujaribu kuficha ukweli wa tukio, nimempa onyo kali Inspekta Galilima.
“Katika tukio hilo nimempandisha cheo ASP Francis Duma aliyekuwa kiongozi wa askari 14 katika kupambana kulikamata gari la FFU lililobeba bangi na kuwa Mrakibu wa Polisi,askari wengine 14 nimegiza Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP, Said Mwema kuwapandisha vyeo kwa sababu wapo ngazi yake,”alisema.
Tukio la fuvu
Dk. Nchimbi alisema amewavua madaraka yote waliyonayo Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Mvomero, Inspekta Jamal Ramadhan na Mkuu wa Kituo cha Polisi Dumila, Inspekta Juma Mpamba kutokana na kuonyesha udhaifu mkubwa katika utendaji kazi wa kushindwa kuwasimamia askari wake na kushindwa kuwakamata matapeli na hawalifu ambao ni vinara.
Dk. Nchimbi alisema kabla ya tukio la askari watatu kushirikiana na raia wawili kumbambikizia fuvu la binadamu mfanyabishara Samson Mwita, Inspekta Ramadhan alikuwa na taarifa za mpango wa tukio hilo la askari wake kushirikiana na rai kufanya kufanya hivyo lakini hakumtaarifa Inspekta Mpamba.
Alisema askari wote waliohusika na tukio hilo ambao ni Sajeti Pasua Mohamed, Sajeti Sadick Madodo Koplo Nuran Msabaha wamefukuzwa kazi na kushitakiwa kwa uhalifu waliotenda sambamba na raia wawili ambao ni Rashid Hamisi na Adamu Peter.
Kupiga na kuua raia
Dk. Nchimbi alisema Disemba 25 mwaka jana askari wa kituo kidogo cha polisi cha Heru Ushingo kilichopo Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma kwa pamoja walimpiga raia ambaye ni marehemu sasa Gasper Sigwavumba na kumweka mahabusu bila msaada wowote wa matibabu.
Alisema katika tukio marehemu alipasuka bandama kutokana na kipigo hicho na kuongeza kwamba upelelezi mbovu uliofanywa chini ya usimamizi wa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kasulu, ASP Daniel Bendarugaho kesi ya mauaji iliweza kuondolewa mahakamani.
Dk. Nchimbi alisema wakati kesi inaondolewa mahakamani askari waliohusika ambao ni Koplo Abraham Peter na PC Simon Sunday walikuwa wamefukuzwa kazi na kuwa huru jambo ambalo lilizua malalamiko.
“Kutokana na ASP Bendarugaho kutokuwa makini katika kusimamia upelelezi wa jalada husika la kesi hiyo ya mauaji tunavua madaraka na upelelezi unaanza upya ili haki itendeke,”alisema.
“Operesheni ya kulisafisha jeshi hilo itaendelea hadi litakapokuwa safi, leo hii wananchi wamekata tama kabisa na jeshi la polisi ukimwambia kitu chochote juu ya polisi haamini.
“Kwa kipindi nitakachokuwa naongoza wizara hii, nitalisafisha na Watanzania watarudisha imani kwa polisi, katika matukio haya matatu askari waliohusika moja kwa moja wamefukuzwa kazi na kushitakiwa.
“Haya ni matokeo ya uchunguzi uliofanywa na timu niliyoiunda ambapo Mwenyekiti wake alikuwa Mkurugnezi Mkuu wa Idara ya masuala ya Malalamiko Makao Makuu, Augostine Shio.
BOMBA LA GESI KUTANDAZWA LEO.26/8/2013
Bomba la gesi ya Mtwara kutandazwa leo
Na Benjamin Masese, aliyekuwa Lindi
BOMBA la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam,
linaanza kutandazwa leo likianzia mkoani Lindi.
Kutokana na hali hiyo, Serikali imeonya kwamba,
yeyote atakayethubutu kuharibu miundombinu ya bomba hilo, atachukuliwa hatua.
Taarifa hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa Nishati na
Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alipofanya ziara ya kukagua, ubora wa vifaa, rasilimali
watu na maandalizi ya miundombinu ya
kutandaza bomba hilo.
Wakati wa ziara hiyo ya siku moja, alikuwapo pia Balozi
wa China nchini, Lu Youging, viongozi mbalimbali wa Serikali na viongozi wa kampuni
zinazotandaza bomba hilo.
Profesa Muhongo alisema ameridhishwa na maandalizi
yanavyokwenda, kwa kuwa kuna vifaa vya kisasa na imara.
Kesho kutwa (leo), utandazaji wa bomba unaanza rasmi
na kwa maandalizi niliyoshuhudia, nina imani mradi huu utakamilika kabla ya Desemba
mwaka 2014.
“Naomba Watanzania wawe na imani kubwa na watoe ushirikiano
kwani utandazaji wa bomba utafanyika katika pande zote mbili, kwa maana ya nchi
kavu na baharini.
“Mradi huu ni wa gharama kubwa na kama mnakumbuka,
tulikopa fedha kutoka Benki ya Exim ambazo ni Dola za Marekani bilioni 1.2 kwa
masharti nafuu.
“Pamoja na kwamba nia yetu ni nzuri, kuna baadhi ya
watu wasiopenda maendeleo ya nchi hii, nataka kuwahakikishia Watanzania wote,
kwamba usalama wa miundombinu hii utakuwa shwari na kama mtu anataka
kushughulikiwa na Serikali, basi ajaribu kuihujumu atakiona cha mtema kuni.
“Hapa tumeshuhudia Watanzania 45 walioanza kupata
ajira kama madereva, vibarua, kampuni za usafirishaji, huu ni mwanzo tu na ikifika
sehemu ya kuhitaji watu wenye utaalamu, wataajiriwa wenye utaalamu,” alisema
Profesa Muhongo.
Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, mabomba yanayotandazwa
ni ya aina mbili yakiwamo ya inchi 36 na uzito wa tani tano na yenye inchi 24 yakiwa
na tani tatu ambayo alisema kwa ujumla wake yatadumu kwa miaka 30 na kama
yakitunzwa vizuri yatadumu hadi miaka 70.
“Tunataka ifikapo mwaka 2016, tuwe na umeme wa
megawati 3000 na mwingine wa ziada wa utakaokuwa ukiuzwa nje ya nchi ikiwamo Kenya
ambayo imeleta maombi ya kuuziwa megawati 1000,” alisema.
Pamoja na kufanya ziara hiyo juzi, Profesa Muhongo
alisema itakuwa ni endelevu na itakuwa ikihusisha waandishi wa habari.
Naye, Balozi Youging, alisema gesi ni kitega uchumi kizuri
ambacho kinaweza kuwaondoa Watanzania katika umasikini.
“China ni moja ya nchi iliyonufaika na gesi na ndio
maana raia wake ni wataalamu wa nishati hiyo, naamini upatikanaji wa gesi hapa
Tanzania, utasaidia Watanzania kuondokana na matumizi ya mkaa na kuni.
Kwa upande wake, Meneja Mradi wa Shirika la
Maendeleo ya Petroli Tanzania, Mhandisi Baltazari Thomas, alisema hadi sasa
watu 163 wamepata ajira katika awamu ya
kwanza na kati ya hao Watanzania ni 68.
Mwisho.
Rufaa dhidi ya Zombe kusikilizwa leoNa Kulwa Mzee, Dar es Salaam
MAOMBI ya Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) ya kuongezewa muda wa kukata rufaa dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na askari wenzake wanane walioachiwa huru katika shtaka la mauaji, yanatarajiwa kusikilizwa leo.
Maombi hayo yanatarajiwa kusikilizwa katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam mbele ya Jaji Aloyisius Mujuluzi.
Katika shauri hili, DPP aliwasilisha maombi ya kuomba kuongezewa muda wa kukata rufaa, baada ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, kutupilia mbali rufaa ya awali kwa sababu ilikuwa na makosa ya kisheria.
Rufaa hiyo ilitupwa baada ya kubaini kuwapo kwa dosari katika hati ya kusudio la kukata rufaa na mahakama kukataa kuamuru makosa yaliyojitokeza yafanyiwe marekebisho.
“Kusudio la kukata rufaa ndio linatengeneza rufaa yenyewe, kwa kuwa kuna makosa, hakuna rufaa iliyopo mahakamani, kama makosa yangejitokeza katika rufaa yenyewe, Mahakama ingeweza kutoa maelekezo ya kufanyiwa marekebisho, rufaa inatupwa, Jamhuri ina haki ya kuwasilisha rufaa nyingine nje ya muda, baada ya kuomba kufanya hivyo,” alisema Mwenyekiti wa Jopo la Majaji Watatu, Edward Rutakangwa.
Majaji wengine waliokuwa wakisikiliza rufaa hiyo kabla ya kutupwa ni Jaji Mbarouk Mbarouk na Bethuel Mmila ambao awali walipoketi kwa ajili ya kuanza kusikiliza rufaa iliyokatwa na DPP kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, ziliibuka hoja za dosari katika hati ya kusudio la kukata rufaa.
Zombe na wenzake walikuwa wakikabiliwa na kesi ya mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini wakazi wa Mahenge Morogoro pamoja na dereva teksi mmoja.
Kabla ya jopo la mawakili wa Serikali lililokuwa linamwakilisha DPP ambao ni Mawakili wa Serikali Wakuu, Edwin Kakolaki, Vitalis Timon, Prudence Rweyongeza na Mawakili Revocatus Mtaki na Alexander Mzikila, halijaanza kuwasilisha hoja zao za kukata rufani, Jaji Mbaraouk alilihoji jopo hilo kuhusu dosari hiyo.
“Mahakama inataka kujiridhisha juu ya kinachosomeka katika hati ya kusudio la kukata rufaa, ambayo inasema mnapinga hukumu iliyotolewa na Jaji Massati wa Mahakama ya Rufaa. Sasa hii inakuja kwetu kama marejeo au mapitio," alihoji Jaji Mbarouk.
Hata hivyo, Wakili Timon, alikiri kuhusu dosari hiyo na hivyo kuiomba Mahakama kuwaruhusu kufanya marekebisho na kisha kuendelea kusikiliza rufaa hiyo.
Jaji Rutakangwa alihoji upande wa Jamhuri kuwa hati hiyo ina dosari, kwa kuwa inaonyesha wanakata rufaa kupinga hukumu ya Jaji wa Mahakama ya Rufaa, wakati hajawahi kukaa kusikiliza shauri hilo kwa kuwa si sahihi.
Ombi la mawakili wa Serikali la kuomba kufanyia marekebisho hati hiyo, lilipingwa vikali na mawakili wanaowawakilisha Zombe na wenzake ambao ni Richard Rweyongeza, Majura Magafu na Dennis Msafiri.
Katika shauri hili, mbali na Zombe, wajibu rufani wengine ni polisi Christopher Bageni, Ahmed Makele, Jane Andrew, Koplo Emmanuel Mabula, Michael Shonza, Abeneth Saro, Rajabu Bakari na Festus Gwasab.
Serikali ilikata rufaa hiyo kupinga hukumu iliyotolewa Agosti 17, 2008 na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.
mwisho.
Nyavu haramu za Sh milioni 150
zateketezwa
Na Ahmed
Makongo, Bunda
NYAVU haramu 3,280 zenye thamani ya
zaidi ya Sh milioni 150, zimekamatwa wilayani Bunda, mkoani Mara na kuteketezwa
kwa moto.
Nyavu hizo ziliteketezwa jana kwa
usimamizi wa Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Joshua Mirumbe.
Akizungumza wakati wa shughuli hiyo,
Mirumbe alisema kuwa nyavu hizo ambazo ni pamoja na makokolo ya kuvulia
sangara, nyavu zenye matundu madogo, timba na makokolo ya dagaa, zimekamatwa na
vyombo vya dola kutokana na msako unaoendelea wilayani hapa.
Alisema kuwa msako huo unashirikisha
askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), polisi, mgambo pamoja na maofisa wa
idara ya uvuvi.
Alisema operesheni hiyo aliianzisha
mwenyewe na kwamba itakuwa endelevu kwa kuwa lengo lake ni kutokomeza wavuvi
haramu wilayani hapa.
Ili kuhakikisha uvuvi haramu
unakomeshwa wilayani hapa, aliwataka viongozi wa Serikali za vijiji, kata na Vikundi
vya Ulinzi wa Rasilimali za Ziwa Victoria (BMU), kuhakikisha wavuvi haramu
wanakamatwa.
Alisema kama uvuvi haramu utaendelea
katika baadhi ya maeneo, kitakachofuata ni kukamatwa kwa viongozi wa maeneo utakakokuwa
ukifanyika uvuvi huo.
“Hatua ifuatayo ni kukamata viongozi
wa Serikali za vijiji na kata na wale wa BMU ambao tutakuta kwenye maeneo yao
kunaendeshwa shughuli za uvuvi haramu,” alisema Mirumbe.
Aliwaonya viongozi hao kutojihusisha
na shughuli za uvuvi haramu, kwa kuwa inasemekana baadhi yao wanafadhili wavuvi
hao.
Naye, Ofisa Uvuvi wa Wilaya ya
Bunda, Stephen Ochieng, alisema nyavu hizo zilikamatwa katika Tarafa za
Kenkombo na Nansimo ambako ndiko uvuvi haramu ulikoota mizizi.
Aliongeza kwamba, wapo wavuvi haramu
ambao wamekuwa wakitumia sumu na kwamba uvuvi huo unahatarisha afya za wananchi
pamoja na kuua viumbe hai wa majini.
Aidha alitumia fursa hiyo kuwaomba
viongozi wa wilaya jirani zilizoko kwenye ziwa Victoria, kudhibiti wavuvi
haramu, kwani unapofanyika msako katika Wilaya ya Bunda, baadhi ya wavuvi hao hukimbilia
katika wilaya hizo.
Mwisho.
Thursday, 15 August 2013
LWAKATARE HOI
Polisi, Dk. Slaa jino kwa jino
Na Benjamin Masese, Dar es Salaam
WAKATI Jeshi la Polisi likiendelea kumng’ang’ania Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare kwa tuhuma za kupanga njama za kudhuru watu, imedaiwa kuwa afya ya kiongozi huyo imezidi kudhoofika.
Na Benjamin Masese, Dar es Salaam
WAKATI Jeshi la Polisi likiendelea kumng’ang’ania Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare kwa tuhuma za kupanga njama za kudhuru watu, imedaiwa kuwa afya ya kiongozi huyo imezidi kudhoofika.
Tuesday, 13 August 2013
TUJADILIANE LEO
Hivi kulingana na matukio haya yanayotokea ya ukatili kwa raia, wizi, utekaji na masuala kama hayo yanaashiria nini? tujadili, tafadhali unapochangia hapa toa hoja sio kushambulia mtu kwa itikadi na dini zako.
UKATILI HUU MPAKA LINI TANZANIA?
![]() |
Mama akipigwa na mume wake baada ya kutofautina |
![]() |
Baba akimdhibiti mke wake kwa kumkata mapanga baada ya kuona ngumi, mateke na fimbo havikutosha |
Na Benjamin Masese, Dar es Salaam
UKATILI wa kijinsia ni jambo
kubwa kwenye ajenda za haki za binadamu
kimataifa.Ukatili unaweza kuwapata wanaume na wanawake lakini mara nyingi
wanawake na watoto ndio waathirika wakubwa.
Hali hii imetokana na mifumo mbalimbali iliyopo na uhusiano wa
kijinsia ulivyo katika jamii zetu hapa nchini ambapo kundo moja hujiona ni bora
kuliko kundi lingine.
Kwa miaka mingi wanaume
wamechukuliwa kuwa katika daraja la juu kuliko mwanamke nah ii imejionyesha na
kuendelea kuonekana wazi katika nyanja
zote za kijamii, kiutamaduni, kisiasa na kiuchumi.
Mazoea hayo yamejengwa tangu
zamani huku kukiwa na ngazi za kifamilia hadi kitaifa jambo ambalo ni hatari
katika jamii nyingi Barani Afrika na sehemu nyingine duniani.
Kutokana na hali hiyoilivyo
mpaka sasa, kuna haja kubwa ya kutoa elimu juu ya ukatili katika jamii zetu
hususani vijijini kunakotokea kila siku vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake.
Bila Serikali, taasisi,
mashirika na wadau wengine wanapaswa kuungana pamoja na ili kuwaelimisha jamii
juu ya kupambana na kuzuia ukatili wa kijinsia ili kuleta mabadiliko katika
jamii.
Sote tunatambua kwamba
ukatili ni kitendo chochote anachofanyiwa binadamu na kumsababishia maumivu au
athari kimwili, kiakili au kisaikolojia.Kumekuwapo na vitendo vya ukatili vingi
tena vya kukusudia, kulazimisha, kutisha au kugofya dhidi ya wanawake kutaka
kufanya jambo au tendo la ngono bila hiari yao.
Binadamu yeyote anaweza
kufanyiwa ukatili wa aina tano
ukitegemea na utamaduni na
historia ya jamii husika. Mara nyingi
ukatili huo hufanyika kati ya wanandoa wa wapenzi lakini wanawake mara nyingi
wamekuwa wakisumbuliwa zaidi na ukatili wa kijinsia katika uhusianohuo.
Moja ya ukatili ni ule wa
kimwili ambao mtu hufanyiwa kitendo ambacho kinaumiza mwili na madhara yake
huonekana moja kwa moja na wakati
mwingine mtendewa ukatili anaweza kuhisi maumivu bila mtu mwingine kutambua
kuwa amefanyiwa ukatili wa kimwili.
Baadhi ya mifano ya ukatili
wa kimwili ni pamoja na vipigo, shambulio la kimwili, kuchomwa moto, matumizi
ya silaha, kuvutwa nywele, kusukuma, kunyonga mkono au mguu, kupigwa kichwani
na kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu yoyote ya mwili.
Pia upo ukatili wa kisaikolojia ambao mtu
anatendewa na unamsababishia maumivu
kiakili, kihisia huku mtenda kutotambua mwenzake anaathirika, mfano matusi kwa
njia ya maneno au ishara yenye lengo la kudhalilisha, vitisho na kutishia
kufanya fujo, maneno ya kufehedhesha, kudharau, kutishia kutoa siri, kuingiliwa
faragha, kutishiwa kuuawa na mengine mengi.
Vile vile kuna ukatili wa
uhusiano wa kingono ambao huambatana na
vitendo vinavyohusiana na masuala ya ngono, kwa mfano unyanyasaji wa kijinsia,
kujamiiana kwa maharimu, ubakaji ndani ya ndoa, ulawiti, utekaji na
usafirishaji wa wanawake au wanaume na
watoto kwa ajili ya ngono na vitendo vingine vya namna hiyo.
Upo ukatili wa kiuchumi ambao
humnyima fursa za kiuchumi mwanamke au mwanaume katika kujiongezea kipato na
kuchangia katika maendeleo.Aina hiyo ya
ukatili huwapata wanawake kutokana na hali yao ya kuwa tegemezi kwa wenzi wao.
Kitendo cha wanawake kuwa
tegemezi kwa wanaume kimekua kinawaathiri sana
kwani wanakosa kauli katika mali
za familia na kutoshirikishwa kwenye maamuzi ya maendeleo.
Pia kuna ukatili unaotokana
na tamaduni au mila potofu zetu hapa nchini ambazo zinakinzani na haki za
binadamu jambo linalochangia kuwapo kwa vitendo vya ukatili. Baadhi ya ukatili
wa mila potofu ni pamoja na ndoa za kushurutisha za utotoni, kutakasa wajane,
kurithi wajane, utekeaji, matambiko ya kingono kwa watoto, miiko ya chakula na
ukatili utokanao na mahari.
Kutokana na uendelezaji wa vitendo vya ukatili nchini,
kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake
Tanzania (WLAC) kimeamua kuanzisha
kampeni ya kupinga vitendo hivyo na kutoa msaada wa kisheria kwa wanawake ili kuleta usawa wa kijinsia Tanzania.
Taasisi ya WLAC ni shirika lisilo la Serikali lililoanzishwa
mwaka 1994 chini ya sheria ya makampuni sura ya 212 na pia limekuwa
likiendeleza shughuli za kitengo cha
msaada wa sheria SUWATA kilichoanzishwa
mwaka 1989.
Kati ya madhumuni ya WLAC ni
kutoa msaada wa sheria ju ya masuala yanayowakabili wanawake kama
ndoa, mirathi, mikataba, biashara, ajira, uwakilishi mahakamani na huduma
nyingine zinazofanana na hizo.
Pia imekuwa katika harakati
za kujenga mtandao wa mashirika pamoja na taasisi zenye mwelekeo unaofanana na
WLAC na kuratibu kwa pamoja shughuli za uhamasishaji umma kuhusu haki za
wanawake na watoto.
Si jambo la kificho kwani
wanawake wamekuwa katika changamoto kubwa hasa pale wanapokuwa katika ajira
rasmi na hata zisizokuwa rasmi, baadhi yao
wamekuwa wakikosa nafasi za kufanya kazi
mahali walipoomba kazi auhata katika ngazi ya familia kutokanana sababu
mbalimbali.
Katika maeneo ya kazi, uzoefu
unaonyesha wazi kuna kazi za wanawake na kazi za wanawake, wanawake
waliobahatika kupata ajira wengi utawakuta nafsi za chini zaidi kama mapokezi, uhudumu wa ofisi, kazi za usafi na katibu
mukhatsi.
Wakati mwingine baadhi ya
wanawake wamelazimika kuingia katika uhusiano wa kimapenzi na wakuu wao wa kazi
ili kupata mahitaji yao.Wanawake wa namna hiyo huishia kwenye migogoro na waume
zao au wapenzi wan a hatimaye uhusiano huo huharibika kabisa na kufukuzwa kazi.
Kazi zinazohitaji mwanamke
kusafiri sana,
kufanya kazi muda mrefu, wakati wa usikuau zinazohusisha kukutana na watu
mbalimbali mara nyingi zimesababisha migogoro katika ndoa.
Hata hivyo wanawake wengi
wamekosa fursa ya kujishughulisha ili kuongeza pato la familia, ambapo kwa wale
waliobahatika kupata ajira zisizo rasmi wengi wao wanaishi kwa masharti na
kutokuwa huru na wanapata mapato yanatokanayo nakazi wanayofanya.
Suala la ukatili lina upana
wake ambapo upo ukatili wa kijinsia unaotokana na lugha ambapo maneno
mbalimbali yamekuwa yakitumika kumwelezea mwanamke ambayo uhalisia wake ni
ukatili wa kijinsia.
Maneno hayo yamekuwa
yakitolewa katika kuelezea maumbile na tabia ya baadhi ya wanawake, matumizi ya
lugha hiyo kwa sehemu kubwa huchangia kuonyesha mfumo dume ambao ndio
unaotawala maisha ya watu ya kila siku. Matumizi ya lugha yanadhihirisha dhana
potofu kwamba kundi la wanaume lina nguvu na ni bora kuliko wanawake.
Asilimia kubwa na mazoea
yaliyopo sasa ni kwamba neno mwanamke amekuwa akichukuliwa ni kama chombo cha
kumstarehesha mwanaume, mfano kuna maneno ya kama
changundoa, sahani ya babu, namba nane, twiga na mengine kam hayo ambayo
huonesha kuwa mwanamke ni dhaifu kuliko mwanaume.
Maneno mengine yanayoendana
na hayo wakati mwingine yanaweza kutolewa dhidi ya wanaume, kwa mfano bushoke,
dume la mbegu lakini yote yameelekzwa kwa wanawake kumuonyesha mwanaume ni
bora.
Hata hivyo upo ukatili katika
vyombo vya habari na matangazo ya kibiashara, mfumo wa habari na utoaji wa
habari zenyewe umekuwa ukionesha taswira ya mwanamke kama chombo cha
kumburudisha mwanaume, mfano matangazo, picha na mziki hutumiwa na kuonyesha
wanawake kama sehemu ya matangazo ya biashara.
Kutokana na hali hiyo hivi
karibuni WLAC kupitia wanasheria wake waliandaa semina iliyohusisha wanawake na wanaume wanaojiita wanabadiliko kutoka mikoa ya Dar
es Salaam na Pwani na kutoa elimu juu ya mambo kadhaa ya ukatili wa kijinsia
nchini unaotokea katika nyanja mbalimbali ndani ya jamii.
Wanasheria wa WLAC waliokuwa
wanatoa elimu kwa wanabadiliko ni pamoja na Lilian Lwanga na Hildegard Msina
ambao walitoa ushahidi jinsi wanawake wanavyoteseka ndani ya ndoa zao pamoja na
kunyang’anywa urithi wa mme wake mara anapofariki na kuacha familia.
Kwa upande Lwanga alibainisha
kwamba katika utafiti walioufanya katika kadhaa nchini wamebaini asilimia 75 ya wananawake walio ndani ya ndoa hawana
uhuru wa kijitawala katika maisha yao
ya kila siku kutokana na kufanyiwa vitendo vya ukatili na wenzi wao.
Pia anasema walibaini wanaume
wengi vijijini wamekuwa wakivunja ndoa zao au kuwatelekeza wake wao baada ya
kujifungua watoto wenye vichwa vikubwa, midomo ya sungura na wengine wa namna ambapo
aliitaka Serikali kuchukuliwa hatua za kisheria ili kukomesha hali ya ubaguzi,
unyanyasaji na ukatili dhidi ya wanawake.
WLAC imeamua kuendesha
kampeni maalum ijulikanayo kwa jina la TUNAWEZA
kwa wanamabadiliko ili kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji nchini
ambavyo vinaonekanakuwa jambo la kawaida katika jinsia ya kike.
Lwanga anasema msaada wa kisheria unaotolewa
na WLAC umekuwa na mafanikio makubwa
kwani umeweza kuwasaidia wanawake kwa kuwawakilisha makahamani hadi kurudishiwa nyumba walizokuwa wamenyang’anywa
na ndugu wa marehemu kama urithi.
Anasema katika utafti wao
mikoani wamebaini wanawake bado wananyanyaswa, wanapigwa na waume lakini hawako tayari kuwasema kwenye vyombo vya dola
na kuongeza wameshuhudia ndoa nyingi zimevunjika kwa sababu ya mtoto kuzaliwa
na kichwa kikubwa au mdomo wa wazi yaani wa sungura.
Lwanga anasema tatizo la
watoto kukimbilia mjini na kuwa kuombaomba linatokana na ndoa kuvunjika, elimu ndogo
kwa akina mama ya kutojua sheria zinazowapa haki yao, umasikini na mila potofu.
Anasema asilimia kubwa ya
wananchi hasa wa vijini wanaishi kwa kuzingatia mila zao, hawajui mabadiliko yaliyopo, wananyanyaswa kwa njia
ya ngono, kiuchumi, kishambulio na kisaikolojia lakini hawajui namna ya
kujisaidia kisheria kwani tangu awali Serikali haijaweka misingi ya kuwalinda
wananwake na kuwapa uhuru.
Pamoja na mambo mengi ya
unyanyasaji wa wanawake, Lwanga anaitaka Serikali kuacha mazoea ya kutegemea
asasi, mashirika na ufadhili wa mataifa makubwa ya nje kuja nchini kutatua
matatizo yanayowakabili wananchi wake badala yake inapaswa kupeleka elimu
vijijini hususani katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Lwanga anasema kwamba ukatili
unaofanywa dhidi ya wanawake nchini hauwezi kuvumiliwa ambapo anawataka wanawake kuwafikisha wanaume kwenye vyombo
vya dola aple wanapotendewa vitendo vya unyanyasaji.
Anasema binadamu yeyote
anapofanyiwa ukatili humsababishia kuwa
na maumivu au athari kimwili, kiakili na kisaikolojia ambapo mwanamke anapofanyiwa
ukatili huo athari kubwa kuliko mwanaume.
Anasema hivi sasa WLAC kwa
kushirikiana na wakuu wa utekelezaji wa kampeni ya TUNAWEZA wamedhamiria
kufikisha elimu ya ukatili wa kijinsia kwa watu 1,600,000 ifikapo mwaka
2013 ikiwa lengo ni kupunguza vitendo hivyo kwa wanawake ambavyo vimeonekana
ndani ya jamii ni vitu vya kawaida.
Lwanga anasema madhumuni ya
WLAC ni kutoa msaada wa sheria juu ya masuala yanayowakabili wanawake kama ndoa, mirathi, mikataba, kusimamia kesi mahakamani,
kuendesha semina, ziara za mafunzo na kuhamasisha umma kuhusu haki za wanawake
na watoto.
Pamoja na mambo mengi , wanasheria
wa WLAC waliahidi kuendelea kutoa msaada wa kisheria mikaoni bure kwa wanawake
na watoto ikiwa lengo ni kuleta usawa wa kijinsia Tanzania.
Hivyo sasa wakati umefika kwa
Seriakli kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha vitendo vya unyanyasaji
kijinsia vinakomeshwa haraka, pia vitendo vilivyoibuka hivi karibuni vya mateka
kwa watu wanaopigania haki zao havipaswi kufumbiwa macho.
Tunapaswa kutambua kwamba
katika hali halisi binadamu wote wamezaliwa huru huru na wote ni sawa mbele ya
sheria hivyo hakuna mwenye haki ya kumfanyia mwenziwe ukatili wa aina yoyote.
Vitendo hivi vinapofanyika ni
kinyume cha sheria na mikataba mbalimbali ya haki za binadamu ambayo Tanzania
imekuwa ikiisaini ili kushirikiana na mataifa makubwa kupambana na vitendo
hivyo, sasa ni mwito kwa serikali kutekeleza mikataba hiyo kwa vitendo na sio
maneno tupu. Maoni benjaminmasese@yahoo.com,
0655/0769-688300
MWISHOOO
Wakina mama wa kabila la Wangoreme wakifurahi wakati wa sherehe
Kabila la wangoreme na wakurya mkoani Mara wanavyokuwa wakisherekea shehehe za, harusi, kutahiriwa au kukeketwa. (chanzo. BBC Swahili)
|
DAR CITY 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)